< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Yahvé parla à Moïse dans le désert de Sinaï, dans la tente de la Rencontre, le premier jour du second mois, la deuxième année après leur sortie du pays d'Égypte, et il dit:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
« Recense toute l'assemblée des enfants d'Israël, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre de leurs noms, tous les mâles, un par un,
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui sont en état de porter les armes en Israël. Toi et Aaron, vous les compterez selon leurs divisions.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Il y aura avec vous un homme de chaque tribu, chacun à la tête de la maison de ses pères.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Voici les noms des hommes qui se tiendront à vos côtés: De Reuben: Elizur, fils de Shedeur.
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
De Siméon: Shelumiel, fils de Zurishaddai.
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
De Juda: Nahshon, fils d'Amminadab.
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
D'Issachar: Nethanel, fils de Zuar.
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
De Zabulon: Eliab, fils de Helon.
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Des fils de Joseph: d'Éphraïm: Élischama, fils d'Ammihud; de Manassé: Gamaliel, fils de Pedahzur.
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
De Benjamin: Abidan, fils de Gideoni.
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
De Dan: Ahiezer, fils d'Ammishaddai.
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
d'Asher: Pagiel, fils d'Ochran.
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
De Gad: Eliasaph, fils de Deuel.
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Pour Nephtali: Ahira, fils d'Enan. »
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Voici les appelés de l'assemblée, les princes des tribus de leurs pères; ils étaient les chefs des milliers d'Israël.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Moïse et Aaron prirent ces hommes qui sont mentionnés par leur nom.
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
Ils convoquèrent toute l'assemblée le premier jour du second mois, et ils déclarèrent leurs ancêtres selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, un par un.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse, celui-ci les compta dans le désert de Sinaï.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Ruben, premiers-nés d'Israël, selon leurs générations, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, un par un, tous les mâles depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient en état de porter les armes.
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
Ceux de la tribu de Ruben dont on fit le dénombrement furent quarante-six mille cinq cents.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On fit le dénombrement des fils de Siméon, selon leurs générations, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms, un par un, tous les mâles depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient en état de porter les armes.
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
On fit le dénombrement des fils de la tribu de Siméon: cinquante-neuf mille trois cents.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Gad, selon leurs générations, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient en état de porter les armes.
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
On compta quarante-cinq mille six cent cinquante hommes de la tribu de Gad.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Des fils de Juda, selon leurs générations, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
ceux de la tribu de Juda dont on fit le dénombrement furent soixante-quatorze mille six cents.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils d'Issacar, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient en état de porter les armes.
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
On fit le dénombrement des fils de la tribu d'Issacar: cinquante-quatre mille quatre cents.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Zabulon, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
ceux de la tribu de Zabulon dont on fit le dénombrement furent cinquante-sept mille quatre cents.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Joseph: des fils d'Éphraïm, selon leurs générations, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
ceux de la tribu d'Éphraïm dont on fit le dénombrement furent quarante mille cinq cents.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Manassé, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
ceux de la tribu de Manassé dont on fit le dénombrement furent trente-deux mille deux cents.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Benjamin, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms depuis l`âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
ceux de la tribu de Benjamin dont on fit le dénombrement furent trente-cinq mille quatre cents.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Dan, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
ceux de la tribu de Dan dont on fit le dénombrement furent soixante-deux mille sept cents.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils d`Aser, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant les noms depuis l`âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
ceux de la tribu d'Aser dont on fit le dénombrement furent quarante et un mille cinq cents.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
On enregistra les fils de Nephthali, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, d'après le nombre des noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres à faire la guerre:
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
ceux de la tribu de Nephthali dont on fit le dénombrement furent cinquante-trois mille quatre cents.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Ce sont là ceux dont Moïse et Aaron firent le compte, et les douze hommes qui furent princes d'Israël, chacun pour sa maison de pères.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Tous ceux des enfants d'Israël qui furent comptés selon leurs maisons de pères, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui étaient en état de porter les armes en Israël -
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
tous ceux qui furent comptés furent six cent trois mille cinq cent cinquante.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Mais les Lévites, selon la tribu de leurs pères, ne furent pas comptés parmi eux.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Car Yahvé avait parlé à Moïse, en disant:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
« Tu ne compteras pas la tribu de Lévi et tu ne la recenseras pas parmi les enfants d'Israël;
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
mais tu établiras les Lévites sur le tabernacle du témoignage, sur tout son mobilier et sur tout ce qui lui appartient. Ils porteront le tabernacle et tous ses ustensiles; ils en prendront soin et camperont autour de lui.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Lorsque le tabernacle devra être déplacé, les Lévites le descendront; et lorsque le tabernacle devra être dressé, les Lévites le dresseront. L'étranger qui s'approchera sera mis à mort.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Les enfants d'Israël dresseront leurs tentes, chacun selon son camp, chacun selon sa bannière, selon leurs divisions.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Les Lévites camperont autour de la tente du Témoignage, afin qu'il n'y ait pas de colère sur l'assemblée des enfants d'Israël. Les Lévites seront responsables du Tabernacle du Témoignage. »
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Les enfants d'Israël firent ainsi. Ils firent tout ce que Yahvé avait ordonné à Moïse.

< Hesabu 1 >