< Hesabu 1 >
1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
U Sinajskoj pustinji, u Šatoru sastanka, reče Jahve Mojsiju prvoga dana drugoga mjeseca, druge godine po izlasku iz zemlje egipatske:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
“Obavite popis sve zajednice izraelske po rodovima i porodicama, navodeći imena svih muškaraca, glavu po glavu.
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
Od dvadeset godina naviše, za borbu sposobne u Izraelu, ti i Aron pobilježite prema njihovim jedinicama.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Neka s vama bude po jedan čovjek od svakoga plemena, glavari svoga pradjedovskog doma.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Ovo su imena ljudi koji će vam pomagati: Elisur, sin Šedeurov, za pleme Rubenovo;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
Šelumiel, sin Surišadajev, za pleme Šimunovo;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
Nahšon, sin Aminadabov, za pleme Judino;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
Netanel, sin Suarov, za pleme Jisakarovo;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
Eliab, sin Helonov, za pleme Zebulunovo.
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Za Josipove sinove: Elišama, sin Amihudov, za pleme Efrajimovo; Gamliel, sin Pedahsurov, za pleme Manašeovo;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
Abidan, sin Gidonijev, za pleme Benjaminovo;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
Ahiezer, sin Amišadajev, za pleme Danovo;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
Pagiel, sin Okranov, za pleme Ašerovo;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
Elijasaf, sin Deuelov, za pleme Gadovo;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Ahira, sin Enanov, za pleme Naftalijevo.”
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
To bijahu sazivači zajednice, knezovi pradjedovskih plemena i glavari rodova izraelskih.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Mojsije i Aron onda uzmu one ljude što su po imenu bili određeni
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
te prvoga dana drugoga mjeseca sazovu svu zajednicu. Tada se u popis prema rodovima i porodicama po redu unosio broj osoba starijih od dvadeset godina.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Kako je Jahve naredio Mojsiju, tako ih je on pobilježio u Sinajskoj pustinji.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo Rubena, Izraelova prvorođenca, prema njegovim rodovima i porodicama, pribilježiše, glavu po glavu, imena svih muškaraca od dvadeset godina naviše, svih za borbu sposobnih.
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
Popisanih od Rubenova plemena bilo je četrdeset i šest tisuća i pet stotina.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Bili su popisani Šimunovi potomci prema njihovim rodovima i porodicama: pribilježiše se, glava po glava, imena svih muškaraca od dvadeset godina naviše, svih za borbu sposobnih.
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
Popisanih od Šimunova plemena bilo je pedeset i devet tisuća i tri stotine.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Gadovih prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
Popisanih od Gadova plemena bilo je četrdeset i pet tisuća i šest stotina i pedeset.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Judinih prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
Popisanih od Judina plemena bilo je sedamdeset i četiri tisuće i šest stotina.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Jisakarovih prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
Popisanih od Jisakarova plemena bilo je pedeset i četiri tisuće i četiri stotine.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Zebulunovih prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
Popisanih od Zebulunova plemena bilo je pedeset i sedam tisuća i četiri stotine.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Josipovi sinovi: Kad se utvrdi potomstvo sinova Efrajimovih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
Popisanih od Efrajimova plemena bilo je četrdeset tisuća i pet stotina.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Manašeovih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
Popisanih od Manašeova plemena bilo je trideset i dvije tisuće i dvjesta.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Benjaminovih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
Popisanih od Benjaminova plemena bilo je trideset i pet tisuća i četiri stotine.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Danovih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
Popisanih od Danova plemena bilo je šezdeset i dvije tisuće i sedam stotina.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Ašerovih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
Popisanih od Ašerova plemena bila je četrdeset i jedna tisuća i pet stotina.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Kad se utvrdi potomstvo sinova Naftalijevih, prema njihovim rodovima i porodicama, pribilježiše se, glava po glava, imena onih od dvadeset godina i više, svih za borbu sposobnih.
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
Popisanih od Naftalijeva plemena bilo je pedeset i tri tisuće i četiri stotine.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
To su oni koje popisaše Mojsije i Aron sa dvanaest knezova izraelskih, po jedan na svaki pradjedovski dom.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Bili su popisani svi Izraelci, prema pradjedovskim domovima, od dvadeset godina i više, svi za borbu sposobni u Izraelu.
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
Bilo je, dakle, svih popisanih šest stotina i tri tisuće i pet stotina i pedeset.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Među te nisu se ubrojili Levijevci prema svojem pradjedovskom plemenu.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Jahve je, naime, rekao Mojsiju:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
“Nipošto nemoj popisivati Levijeva plemena niti ga unosi u popis Izraelaca.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Nego ti sam odredi Levijevce za službu u Prebivalištu svjedočanstva; za sav njegov namještaj i sve što na nj spada; neka oni nose Prebivalište i sav njegov namještaj; neka oni u njemu poslužuju i oko njega tabore.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Kad se Prebivalište mora premještati, neka ga Levijevci rastave; a kad se s Prebivalištem treba utaboriti, neka ga Levijevci opet podignu. Svjetovnjak koji bi mu se primakao neka se pogubi.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Neka Izraelci logoruju svatko u svome taboru; svatko kod svoje zastave, po četama.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Levijevci neka borave oko Prebivališta svjedočanstva, da se gnjev ne obori na izraelsku zajednicu. Neka tako Levijevci stražu straže oko Prebivališta svjedočanstva.”
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Izraelci učine kako je Jahve Mojsiju naredio. U svemu tako urade.