< Nehemia 9 >

1 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
Or, au vingt-quatrième jour de ce mois, les enfants d’Israël s’assemblèrent dans le jeûne, dans des sacs, et ayant de la terre sur eux.
2 Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
Et la race des enfants d’Israël fut séparée de tout fils étranger; et ils se tinrent debout, et ils confessaient leurs péchés et les iniquités de leurs pères.
3 Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
Ainsi ils se levèrent pour se tenir debout, ils lurent dans le volume de la loi du Seigneur leur Dieu quatre fois dans le jour, et quatre fois ils confessaient leurs péchés et adoraient le Seigneur leur Dieu.
4 Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
Or sur l’estrade des Lévites se levèrent Josué, Bani, Cedmihel, Sabania, Bonni, Sarébias, Bani et Chanani, et ils crièrent avec une voix forte vers le Seigneur leur Dieu.
5 Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
Et les Lévites Josué, Cedmihel, Bonni, Hasebnia, Sérébia, Odaïa, Sebnia, Phathahia, dirent: Levez-vous; bénissez le Seigneur votre Dieu depuis l’éternité jusqu’à l’éternité; qu’ils bénissent donc le nom sublime de votre gloire en toute bénédiction et louange.
6 Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
C’est vous-même, Seigneur, vous seul qui avez fait le ciel, et le ciel des cieux, et toute leur milice; la terre, et tout ce qui est en elle; les mers, et tout ce qui est en elles; et c’est vous qui vivifiez toutes choses, et l’armée du ciel vous adore.
7 “Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
C’est vous-même, Seigneur Dieu, qui avez choisi Abram, qui l’avez retiré du feu des Chaldéens, et qui lui avez donné le nom d’Abraham.
8 Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
Et vous avez trouvé son cœur fidèle devant vous, et vous avez fait avec lui alliance pour lui donner la terre du Chananéen, de l’Héthéen, de l’Amorrhéen, du Phérézéen, du Jébuséen et du Gergéséen, pour la donner à sa postérité; et vous avez accompli vos paroles, parce que vous êtes juste.
9 “Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
Et vous avez vu l’affliction de nos pères en Égypte, et vous avez entendu leur cri sur la mer Rouge.
10 Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
Et vous avez fait éclater des signes et des merveilles sur Pharaon, et sur tous ses serviteurs, et sur tout le peuple de ce pays; car vous avez connu qu’ils avaient agi insolemment contre eux, et vous vous êtes fait un nom comme il est encore en ce jour.
11 Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
Et vous avez divisé la mer devant eux, et ils ont passé au milieu de la mer à sec; et ceux qui les poursuivaient, vous les avez jetés au fond, comme une pierre dans de grandes eaux.
12 Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
Et dans une colonne de nuée, vous avez été leur guide pendant le jour, et dans une colonne de feu pendant la nuit, afin que leur apparût la voie dans laquelle ils entraient.
13 “Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
Vous êtes descendu aussi sur la montagne de Sinaï, et vous avez parlé avec eux du haut du ciel; et vous leur avez donné des ordonnances justes et une loi de vérité, des cérémonies et des bons préceptes.
14 Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
Et vous leur avez montré votre sabbat sanctifié, et vous leur avez prescrit et des commandements et des cérémonies, et une loi, par l’entremise de Moïse, votre serviteur.
15 Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
Vous leur avez donné aussi un pain du ciel dans leur faim, et vous avez fait jaillir de l’eau d’une pierre pour eux, lorsqu’ils avaient soif; et vous leur avez dit qu’ils entreraient, pour la posséder, dans la terre sur laquelle vous avez levé la main, jurant que vous la leur donneriez.
16 “Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
Mais eux et nos pères ont agi insolemment; ils ont rendu leur cou inflexible, et ils n’ont pas écouté vos commandements.
17 Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
Et ils n’ont pas voulu entendre, et ils ne se sont pas souvenus de vos merveilles que vous aviez faites pour eux; ils ont même rendu leur cou inflexible; et ils ont établi un chef, pour retourner à leur servitude comme par rébellion. Mais vous, Dieu propice, clément et miséricordieux, ayant de la longanimité et une abondante miséricorde, vous ne les avez point abandonnés,
18 hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
Lors même qu’ils se firent un veau jeté en fonte, et qu’ils dirent: C’est là votre Dieu qui vous a tirés de l’Egypte, et qu’ils firent de grands blasphèmes.
19 “Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
Mais vous, dans vos miséricordes sans nombre, vous ne les avez point abandonnés dans le désert; la colonne de nuée ne se retira point d’eux pendant le jour pour les conduire dans leur voie, ni la colonne de feu pendant la nuit pour leur montrer le chemin par lequel ils devaient marcher.
20 Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
Et vous leur avez donné votre bon esprit pour les enseigner, vous n’avez pas retiré votre manne de leur bouche, et vous leur avez donné de l’eau dans leur soif.
21 Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
Pendant quarante ans vous les avez nourris dans le désert, et rien ne leur a manqué: leurs vêtements ne vieillirent pas, et leurs pieds ne furent pas déchirés.
22 “Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
Et vous leur avez donné des royaumes et des peuples, et vous leur avez distribué des lots, et ils possédèrent la terre de Séhon, et la terre du roi d’Hésébon, et la terre d’Og, roi de Basan.
23 Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
Et vous avez multiplié leurs fils comme les étoiles du ciel, et vous les avez conduits dans la terre dont vous aviez dit à leurs pères qu’ils y entreraient et la posséderaient.
24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
Et les fils sont venus, et ils ont possédé la terre; et vous avez humilié devant eux les habitants de cette terre, les Chananéens, et vous les avez livrés en leur main, eux et leurs rois, et les peuples de cette terre, pour qu’ils leur fissent comme il leur plairait.
25 Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
C’est pourquoi ils prirent des villes fortifiées et une terre fertile, et ils possédèrent des maisons pleines de toute sorte de biens, des citernes faites par d’autres, des vignes, des plants d’oliviers, et beaucoup d’arbres portant des fruits; et ils ont mangé et ils ont été rassasiés, et ils se sont engraissés, et ils ont abondé en délices par votre grande bonté.
26 “Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
Mais ils vous ont provoqué au courroux; ils se sont retirés de vous; ils ont rejeté votre loi derrière eux, tué vos prophètes qui les conjuraient de revenir à vous, et ils ont fait de grands blasphèmes.
27 Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
Et vous les avez livrés à la main de leurs ennemis, qui les ont opprimés. Et dans le temps de leur tribulation, ils ont crié vers vous, et vous les avez entendus du ciel; et, selon vos miséricordes sans nombre, vous leur avez donné des sauveurs pour les sauver de la main de leurs ennemis.
28 “Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
Et, lorsqu’ils ont été en repos, ils ont de nouveau fait le mal en votre présence; et vous les avez délaissés dans la main de leurs ennemis, qui s’en sont rendus maîtres; ils se sont ensuite tournés vers vous et ont crié vers vous, et vous les avez exaucés du ciel, et vous les avez délivrés dans vos miséricordes, en bien des temps divers.
29 “Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
De plus, vous les avez pressés de venir à votre loi; mais ils ont agi insolemment; ils n’ont pas écouté vos commandements, et ils ont péché contre vos ordonnances dans lesquelles l’homme qui les pratiquera, trouvera la vie; mais ils ont tourné l’épaule en arrière; ils ont rendu leur cou inflexible, et n’ont pas écouté.
30 Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
Vous les avez attendus pendant bien des années, et vous les avez pressés par votre esprit, par l’entremise de vos prophètes; mais ils n’ont pas écouté, et vous les avez livrés en la main des peuples de la terre.
31 Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
Mais, dans vos miséricordes innombrables, vous ne les avez point exterminés ni abandonnés, parce que vous êtes un Dieu de miséricorde et de clémence.
32 “Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
Maintenant donc, notre Dieu, le grand, le fort, le terrible, qui gardez l’alliance et la miséricorde, ne détournez point de votre face tout le mal qui nous a accablés, nous, nos rois, nos princes, nos prêtres, nos prophètes, nos pères, et tout votre peuple, depuis les jours du roi d’Assur jusqu’à ce jour.
33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
Pour vous, vous êtes juste dans tout ce qui vous est venu sur nous; car vous avez accompli la vérité, mais nous, nous avons agi avec impiété.
34 Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
Nos rois, nos princes, nos prêtres et nos pères n’ont pas pratiqué votre loi, et n’ont pas écouté vos commandements et vos décrets que vous leur avez intimés.
35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
Et même au milieu de leurs royaumes, et malgré la grande bonté que vous leur avez témoignée, et dans la terre très étendue et fertile que vous leur avez livrée, ils ne vous ont pas servi, et ils ne sont pas revenus de leurs inclinations très mauvaises.
36 “Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
Voilà que nous-mêmes aujourd’hui nous sommes esclaves, ainsi que la terre que vous aviez donnée à vos pères, afin qu’ils en mangeassent le pain et qu’ils jouissent des biens qui sont en elles, et nous-mêmes, nous sommes esclaves dans cette terre.
37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
Et ses fruits se multiplient pour les rois que vous avez placés sur nous à cause de nos péchés, et ils dominent sur nos corps et sur nos bêtes, selon leur volonté, et nous sommes dans une grande tribulation.
38 “Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”
À cause donc de toutes ces choses, nous-mêmes nous faisons une alliance, nous l’écrivons, et nos princes, nos Lévites et nos prêtres la signent.

< Nehemia 9 >