< Nehemia 9 >

1 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
Forsothe in the foure and twentithe dai of this monethe, the sones of Israel camen togidere in fastyng,
2 Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
and in sackis, and `erthe was on hem. And the seed of the sones of Israel was departid fro ech alien sone. And thei stoden bifor the Lord, and knoulechiden her synnes, and the wickidnessis of her fadris.
3 Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
And thei risiden togidere to stonde; and thei redden in the book of the lawe of `her Lord God fouresithis in the dai, and fouresithis in the niyt; thei knoulechiden, and herieden `her Lord God.
4 Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
Forsothe `thei risiden on the degree, of dekenes, Jesuy, and Bany, Cedynyel, Remmy, Abany, Sarabie, Bany, and Chanany.
5 Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
And the dekenes crieden with grete vois to her Lord God. And Jesue, and Cedyniel, Bonny, Assebie, Serebie, Arabie, Odaie, Sebua, and Facaia, seiden, Rise ye, and blesse ye `youre Lord God fro without bigynnyng and til in to with outen ende; and blesse thei the hiye name of thi glorie in al blessyng and preysyng.
6 Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
And Esdras seide, Thou thi silf, Lord, art aloone; thou madist heuene and the heuene of heuenes, and al the oost of tho heuenes; thou madist the erthe and alle thingis that ben there ynne; `thou madist the sees and alle thingis that ben in tho; and thou quikenyst alle these thingis; and the oost of heuene worschipith thee.
7 “Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
Thou thi silf art the Lord God, that chesidist Abram, and leddist hym out of the fier of Caldeis, and settidist his name Abraham;
8 Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
and foundist his herte feithful bifor thee, and thou hast smyte with hym a boond of pees, that thou woldist yyue to hym the lond of Cananei, of Ethei, of Euey, and of Ammorrei, and of Pherezei, and of Jebuzei, and of Gergesei, that thou woldist yyue it to his seed; and thou hast fillid thi wordis, for thou art iust.
9 “Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
And thou hast seyn the turment of oure fadris in Egipt, and thou herdist the cry of hem on the reed see.
10 Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
And thou hast youe signes and grete wondris in Farao, and in alle hise seruauntis, and in al the puple of that lond; for thou knowist, that thei diden proudli ayens oure fadris; and thou madist to thee a name, as also in this dai.
11 Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
And thou departidist the see bifor hem, and thei passiden thorou the `myddis of the see in the drie place; forsothe thou castidist doun the pursueris of hem into depthe, as a stoon in strong watris.
12 Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
And in a piler of cloude thou were the ledere of hem bi dai, and in a piler of fier bi nyyt, that the weie, bi which thei entriden, schulde appere to hem.
13 “Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
Also thou camest doun at the hil of Synai, and spakist with hem fro heuene, and thou yauest to hem riytful domes, and the lawe of trewthe, cerymonyes, and goode comaundementis.
14 Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
And thou schewidist to hem an halewid sabat; and thou comaundidist `to hem comaundementis, and cerymonyes, and lawe, in the hond of Moises, thi seruaunt.
15 Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
Also thou yauest to hem breed fro heuene in her hungur; and thou leddist out of the stoon watir to hem thirstinge; and thou seidist to hem, that thei schulden entre, and haue in possessioun the lond, on which lond thou reisidist thin hond, that thou schuldist yyue it to hem.
16 “Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
But `thei and oure fadris diden proudli, and maden hard her nollis, and herden not thi comaundementis.
17 Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
And thei nolden here; and thei hadden not mynde of thi merueils, which thou haddist do to hem; and thei maden hard her nollis; and thei yauen the heed, that thei `weren al turned to her seruage as bi strijf; but thou art God helpful, meke, and merciful, abidynge longe, `ether pacient, and of myche merciful doyng, and forsokist not hem;
18 hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
and sotheli whanne thei hadden maad to hem a yotun calf, as bi strijf, and hadden seid, This is thi God, that `ledde thee out of Egipt, and thei diden grete blasfemyes.
19 “Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
But thou in thi many mercyes leftist not hem in deseert; for a piler of cloude yede not awei fro hem bi the dai, that it schulde lede hem in to the weie; and a piler of fier yede not awei `fro hem bi nyyt, that it schulde schewe to hem the weie, bi which thei schulden entre.
20 Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
And thou yauest to hem thi good Spirit, that tauyte hem; and thou forbedist not thin aungels mete fro her mouth, and thou yauest to hem water in thirst.
21 Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
Fourti yeer thou feddist hem in deseert, and no thing failide to hem; her clothis wexiden not elde, and her feet weren not hirt.
22 “Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
And thou yauest to hem rewmes, and puplis; and thou departidist lottis, `ether eritagis, to hem, and thei hadden in possessioun the lond of Seon, and the lond of the kyng of Esebon, and the lond of Og, kyng of Basan.
23 Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
And thou multipliedist the sones of hem, as the sterris of heuene; and thou brouytist hem to the lond, of which thou seidist to her fadris, that thei schulden entre, and holde it in possessioun.
24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
And the sones of Israel camen, and hadden the lond in possessioun; and bifor hem thou madist low the dwellers of the lond, Cananeis; and thou yauest hem in to the hondis of the sones of Israel, and the kyngis of hem, and the puplis of the lond, that thei diden to hem, as it pleside hem.
25 Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
And thei token citees maad strong, and fat erthe; and thei hadden in possessioun housis fulle of alle goodis, cisternes maad of othere men, vineris, and places of olyues, and many apple trees. And thei eeten, and weren fillid, and weren maad fat; and hadden plentee of ritchessis `in thi greet goodnesse.
26 “Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
Sotheli thei terriden thee to wrathfulnesse, and yeden awei fro thee, and castiden awei thi lawe bihynde her backis; and thei killiden thi prophetis, that witnessiden to hem, that thei schulden turne ayen to thee; and thei diden grete blasfemyes.
27 Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
And thou yauest hem in to the hond of her enemyes; and thei turmentiden hem; and in the tyme of her tribulacioun thei crieden to thee; and thou herdist them fro heuyn, and bi thi many merciful doyngis thou yauest hem sauyours, that sauyden hem fro the hond of her enemyes.
28 “Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
And whanne thei hadden restid, thei turneden ayen to do yuel in thi siyt; and thou forsokist hem in the hond of her enemyes, and enemyes hadden hem in possessioun; and thei weren conuertid, and thei crieden to thee; forsothe thou herdist hem fro heuene, and delyueridist hem `in thi mercies in many tymes.
29 “Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
And thou witnessidist to hem, that thei schulden turne ayen to thi lawe; but thei diden proudli, and herden not thin heestis, and synneden in thi domes, whiche a man that schal do schal lyue in tho; and thei yauen the schuldre goynge awei, and thei maden hard her nol.
30 Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
And thou drowist along many yeeris on hem, and thou witnessidist to hem in thi Spirit bi the hond of thi prophetis; and thei herden not; and thou yauest hem in to the hond of the puplis of londis.
31 Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
But in thi mercies ful manye thou madist not hem in to wastyng, nethir thou forsokist hem; for thou art God of merciful doynges, and meke.
32 “Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
Now therfor, oure Lord God, greet God, strong, and ferdful, kepynge couenaunt and merci, turne thou not awei thi face in al the trauel that foond vs, oure kyngis, and oure princes, and oure fadris, and oure preestis, and oure profetis, and al thi puple, fro the daies of kyng Assur til to this dai.
33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
And thou art iust in alle thingis, that camen on vs, for thou didist trewthe to vs; but we han do wickidli.
34 Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
Oure kyngis, and oure princes, oure prestis, and fadris `diden not thi lawe; and thei perseyueden not thin heestis and witnessyngis, whiche thou witnessidist in hem.
35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
And thei in her good rewmes, and in thi myche goodnesse, which thou yauest to hem, and in the largest lond and fat, whych thou haddist youe in the siyt of hem, serueden not thee, nether turneden ayen fro her werste studies.
36 “Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
Lo! we `vs silf ben thrallis to dai; and the lond which thou yauest to oure fadris, that thei schulden ete the breed therof, and the goodis that ben therof, `is thral; and we `vs silf ben thrallis, `ethir boonde men, in that lond.
37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
And the fruytis therof ben multiplied to kyngis, whiche thou hast set on vs for oure synnes; and thei ben lordis of oure bodies, and of oure beestis, bi her wille, and we ben in greet tribulacioun.
38 “Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”
Therfor on alle these thingis we `vs silf smyten and writen boond of pees, and oure princes, oure dekenes, and oure prestis aseelen.

< Nehemia 9 >