< Nehemia 9 >

1 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
Now, on the twenty-fourth day of this month, were the sons of Israel gathered together, with fasting and with sackcloth, having earth upon them.
2 Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
And the seed of Israel separated themselves from all the sons of the foreigner, —and stood and made confession over their own sins, and the iniquities of their fathers.
3 Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
So they stood up in their place, and read in the book of the law of Yahweh their God, a fourth part of the day, —and, a fourth part, they were making confession and bowing themselves down, unto Yahweh their God.
4 Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
Then stood up on the platform of the Levites, Jeshua and Bani, Kadmiel, Shebaniah, Bunni, Sherebiah, Bani, Chenani, —and made outcry, with a loud voice, unto Yahweh their God.
5 Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
Then said the Levites—Jeshua and Kadmiel, Bani, Hashabneiah, Sherebiah, Hodiah, Shebaniah, Pethahiah, Stand up, bless Yahweh your God, from age to age, —Yea let them bless thy glorious Name, which is exalted above all blessing and praise.
6 Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
Thou, art Yahweh, thou alone, Thou, didst make the heavens, the heavens of heavens, and all their host, the earth and all that is thereon, the seas and all that is therein, and, thou, holdest them all in life, —and, the host of the heavens, unto thee, are bowing down.
7 “Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
Thou, art Yahweh, God, who didst choose Abram, and broughtest him forth out of Ur of the Chaldees, —and madest his name Abraham;
8 Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
and didst find his heart faithful before thee, and didst solemnize with him a covenant, to give the land of the Canaanite, the Hittite, the Amorite, and the Perizzite, and the Jebusite, and the Girgashite, —to give it unto his seed, —and didst confirm thy words, for, righteous, thou art.
9 “Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
Yea thou sawest the affliction of our fathers, in Egypt, and, their outcry, thou heardest, by the Red Sea;
10 Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
and didst grant signs and wonders against Pharaoh, and against all his servants, and against all the people of his land, for thou hadst taken note, that they ruled proudly over them, —and so thou didst make thee a name, as at this day.
11 Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
And, the sea, didst thou cleave asunder before them, and they passed through the midst of the sea, on dry ground, —whereas, their pursuers, thou didst cast into the depths like a stone, into the mighty waters,
12 Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
And, in a pillar of cloud, didst thou lead them, by day, —and in a pillar of fire, by night, to light up for them the way wherein they should go.
13 “Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
And, upon Mount Sinai, camest thou down, and spakest with them out of the heavens, —and gavest them just regulations, and faithful laws, good statutes and commandments.
14 Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
And, thy holy sabbath, didst thou make known to them, —and, commandments and statutes and a law, didst thou command them, through Moses thy servant.
15 Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
And, bread out of the heavens, didst thou give them, for their hunger, and, waters out of the cliff, didst thou bring them, for their thirst, —and badest them go in to take possession of the land, which thou hadst lifted thy hand to give them.
16 “Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
But, they and our fathers, dealt proudly, —and hardened their neck, and hearkened not unto thy commandments;
17 Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
but refused to hearken, neither kept in mind thy wonders which thou hadst done with them, but they hardened their neck, and appointed a head that they might return to their servitude, in their perverseness. But, thou, art a God of forgivenesses, gracious and full of compassion, slow to anger and abounding in lovingkindness, and didst not forsake them.
18 hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
Yea, although they made them a molten calf, and said, This, is thy God, that brought thee up out of Egypt, —and wrought great insults,
19 “Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
yet, thou, in thine abounding compassions, didst not forsake them in the desert, —the pillar of cloud, departed not from over them by day, to lead them in the way, nor the pillar of fire by night, to light up for them the way wherein they should go.
20 Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
And, thy Good Spirit, thou gavest, to instruct them, —and, thy manna, thou withheldest not from their mouth, and, water, thou gavest them, for their thirst.
21 Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
Yea, forty years, didst thou sustain them in the desert, they lacked nothing, —their mantles, waxed not old and, their feet, swelled not.
22 “Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
And thou gavest them kingdoms, and peoples, and allotted to each of them a corner, —and they took possession of the land of Sihon, and the land of the king of Heshbon, and the land of Og king of Bashan.
23 Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
Their children also, didst thou multiply, like the stars of the heavens, —and didst bring them into the land which thou hadst promised their fathers they should enter to possess;
24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
so the children entered and possessed the land, and thou subduedst before them the inhabitants of the land, the Canaanites, and deliveredst them into their hand, —with their kings, and the peoples of the land, to do with them according to their pleasure;
25 Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
and they captured fortified cities and a fat soil, and took possession of houses full of every good thing, wells digged, vineyards and oliveyards and fruit-trees, in abundance, —so they did eat and were filled and became fat, and luxuriated in thy great goodness.
26 “Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
But they murmured and rebelled against thee, and cast thy law behind their back, and, thy prophets, they slew, who testified against them that they might turn them back unto thee, —and they wrought great insults.
27 Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
Therefore didst thou deliver them into the hand of their adversaries, who distressed them, —and, in the time of their distress, they made outcry unto thee, and, thou, out of the heavens, didst hear, and, according to thine abounding compassions, gavest them saviours, that they might save them out of the hand of their adversaries.
28 “Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
But, as soon as they had rest, they again wrought wickedness before thee, —and thou didst leave them in the hand of their enemies, who bare rule over them, yet, when they again made outcry unto thee, thou, from the heavens, didst hear and didst deliver them according to thy compassions, many times;
29 “Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
and didst testify against them, to bring them back unto thy law, yet, they, dealt proudly, and hearkened not unto thy commandments, and, against thy regulations, they sinned, the which—if any son of earth shall do—then shall he live by them, —and yielded a rebellious shoulder, and, their neck, they stiffened, and hearkened not.
30 Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
And thou didst suffer many years to pass over them, and didst testify against them by thy Spirit through thy prophets, yet did they not give ear, —therefore didst thou deliver them into the hand of the peoples of the lands.
31 Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
Yet, in thine abounding compassions, thou didst not make of them an end, neither didst thou forsake them, —for, a GOD gracious and full of compassion, thou art.
32 “Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
Now, therefore, O our God—the GOD great, mighty, and fearful—keeping the covenant and the lovingkindness, let not all the trouble seem little before thee, which hath come upon us—on our kings, on our rulers, and on our priests, and on our prophets, and on our fathers, and on all thy people, —from the days of the kings of Assyria, until this day.
33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
But, thou, art righteous, as to all that hath fallen upon us, —for, faithfulness, hast thou wrought, whereas, we, have been lawless;
34 Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
and, our kings, our rulers, our priests, and our fathers, have not kept thy law, —nor given heed unto thy commandments, or unto thy testimonies, wherewith thou hast testified against them.
35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
But, they, in their kingdom, and in thine abundant goodness which thou gavest them, and in the broad and fat land which thou didst set before them, did not serve thee, neither turned they from their wicked doings.
36 “Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
Lo! we, to-day, are bondmen—even upon the land which thou gavest our fathers to eat the fruit thereof and the good thereof, lo! we, are bondmen;
37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
and, the increase thereof, aboundeth unto the kings whom thou hast set over us, for our sins, —and, over our bodies, are they bearing rule, and over our cattle, at their pleasure, and, in great distress, we are.
38 “Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”
Seeing, therefore, all this, we, are plighting our faith, and putting it in writing, —and, upon the sealed scroll, are our rulers, our Levites, our priests.

< Nehemia 9 >