< Nehemia 9 >

1 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
同月二十四日,以色列子民都聚集起來,守齋禁食,穿粗毛衣,頭上頂著灰土。
2 Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
以色列的苗裔,同一切外方人的子孫分開之後,便站起來,坦白承認自己的罪過。和祖先的罪惡。
3 Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
他們各站在自己的地方,三小時之久,誦讀他們天主的法律書;又三小時之久,承認了自己的罪過,跪拜了上主,他們的天主。
4 Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
肋未人耶叔亞、彼奴依、卡德米耳、舍巴尼雅、步尼、舍勒彼雅、巴尼、和革納尼,站在高處,大聲呼號上主,他們的天主。
5 Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
隨後肋未人耶叔亞、卡德米耳、巴尼、哈沙彼雅、曷狄雅、舍巴尼雅、培塔希雅說道:「起來! 你們應讚頌上主我們的天主,從永遠直到永遠! 」眾人便讚頌他光榮的聖名,因此名遠超一切稱頌和讚美。
6 Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
厄斯德拉祈禱說:「唯獨你是上主,是你創造了天,天上的天,和天上的一切軍旅,地和地上的一切,海和海中的一切,是你使一切生存;天上的軍旅常在你前跪拜。
7 “Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
上主,你就是那揀選亞巴郎,領他離開加色丁烏爾,給他起名叫阿貝辣罕的天主。
8 Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
你見他的心對你忠實,就與他立約,把客納罕人、赫特人、阿摩黎人、培黎齊人、耶步斯人和基爾加士人的土地,賜給了他的後裔;你履行了你的諾言,因為你是正義的。
9 “Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
你垂顧了我們祖先在埃及的困苦,俯聽了他們在紅海旁的呼聲,
10 Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
遂對法郎和他所有的臣僕,以及他國內所有的民眾,行了奇蹟異能,因為你知道,他們怎樣任性傲慢地,對待了我們的祖先,因而你獲得了大名,直至今日。
11 Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
你在我們祖先面前,分開了海,使他們在海中乾地路過,卻把追趕他們的人,拋入深淵,有如把一塊石頭拋入怒潮。
12 Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
日間你用雲柱領導,夜間你用火柱光照他們所走的路。
13 “Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
你降臨西乃山上,從天上向他們施救,賜給了他們公正的條例、真理的法律、美好的規矩及誡命;
14 Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
你令他們知道,你神聖的安息日,藉著你的僕人梅瑟,向他們頒佈了規矩、誡命和法律。
15 Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
你從天上賜下食物,給他們充飢;使岩石中流出清泉,給他們解渴;命令他們去佔領,。你曾舉手誓許賜與他們的土地。
16 “Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
但是他們,我們的祖先,任性妄為,硬著脖子,不肯聽從你的命令。
17 Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
他們拒絕聽命,忘卻了你在他們中間所行的奇蹟,硬著脖子,立了首領,要回到埃及去當奴隸。但你是寬大為懷,仁愛慈悲,緩於忿怒,富於慈愛的天主,並未拋棄他們;
18 hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
甚至連他們鑄了一個牛犢說:「這是領你出埃及的天主! 」犯了褻瀆的大罪時,
19 “Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
你因你無限的仁慈,也沒有將他們拋棄在曠野中;日間在路上領導他們的雲柱,夜間為他們光照道路的火柱,仍沒有離開他們。
20 Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
你賜下你溫和的風,使他們甦醒,並沒有將「瑪納」扣住,不給他們充飢,仍賜下了水為他們解渴。
21 Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
四十年之久,你在曠野照顧他們,使他們一無所缺;他們的衣服沒有穿破,他們的腳也沒有腫脹。
22 “Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
你將各國和眾民交給了他們,將各個角落分給了他們,他們遂佔領了赫市朋王息紅,和巴商王敖格的土地。
23 Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
你使他們的子孫繁衍,有如天上的繁星,領他們道你誓許與他們的祖先,要去佔領的土地,
24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
他們的子孫便去佔領了那地方;你使那地方的居民客納罕人,屈服在他們面前,將他們的君王和地方上的人民,交在他們的手中,任他們隨意處置。
25 Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
他們攻取了堅固的城池,和肥沃的土地,奪得了滿藏寶物的房舍、掘好的井、葡萄園、橄欖園和豐富的果林;他們都吃得飽滿,身體肥胖,安逸享樂,這都是因你無量的慈善。
26 “Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
但是,他們竟抗命背叛了你,將你的法律置諸背後,殺了那些警戒他們,勸他們歸順於你的先知;他們竟犯了這褻瀆的大罪,
27 Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
因此你把他們交在仇人的手中,受人迫害。他們遭遇迫害時,一呼求你,你就由天上俯聽了他們,照你無限的仁慈,打發救援者,由仇人手中救出他們;
28 “Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
然而他們一享平安,便又去做惡背叛你,因此你又把他們拋在他們敵人手中,受他們的管轄;幾時他們再回心轉意呼號你,你就再由天上俯聽他們,照你無限的仁慈拯救他們。
29 “Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
你曾警告他們轉向你的法律,但是他們仍恣意妄行,不聽從你的命令,違反你的典章,-人若遵行,必因此而生活,-扭轉倔強的肩膀,硬著脖子,不願服從。
30 Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
你多年來容忍他們,藉先知和以你的精神,警戒他們,但他們仍不聽從,所以你將他們交在異方人民手中。
31 Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
但因你無限的仁慈,你沒有消滅他們,也沒有拋棄他們,因為你是博愛仁慈的天主。
32 “Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
現在,我們的天主! 遵守信約,保持仁愛,偉大、全能和可畏的天主! 請不要把我們、我們的君王、我們的首長、我們的司祭、我們的先知、我們的祖先和你的全民眾,從亞述王時代直到今日所遭遇的一切迫害,看作小事。
33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
你使這一切降在我們身上,是公義的,因為你所行的是忠義,而我們所行的是邪惡。
34 Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
我們的君王、我們的首領、我們的司祭和我們的祖先,實在都沒有遵行你的法律,也沒有聽從你的命令和你警戒他們的勸告。
35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
他們在你賜給他們的國土上和許多幸福中,在你擺在他們面前的廣大而肥沃的土地上,並沒有侍奉你,也沒有放棄他們的惡行。
36 “Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
我們今天竟成了奴隸! 看,我們在你賞給我們祖先吃那裏的果實和出產的土地上,作了奴隸!
37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
為了我們的罪過,那豐富的出產歸於你派定來管轄我們的君王,他們隨意處置了我們的肉體和我們的牲畜;我們實在是處在極大的困苦中! 」
38 “Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”
鑑於這一切,我們立了盟約,也寫了出來;我們的族長、我們的肋未人和司祭,也在上面蓋了印。

< Nehemia 9 >