< Nehemia 8 >

1 watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Sheria ya Mose, ambacho Bwana aliamuru kwa ajili ya Israeli.
Wówczas zebrał się cały lud jak jeden mąż na placu, który [był] przed Bramą Wodną, i powiedział do Ezdrasza, uczonego w Piśmie, aby przyniósł księgę Prawa Mojżesza, które PAN nadał Izraelowi.
2 Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
Wtedy Ezdrasz, kapłan, przyniósł Prawo przed zgromadzenie mężczyzn i kobiet oraz wszystkich, którzy mogli słuchać i rozumieć, [a działo się] to pierwszego dnia siódmego miesiąca.
3 Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko mpaka adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Sheria.
I czytał je przed tym placem, który znajdował się przed Bramą Wodną, od rana aż do południa, przed mężczyznami i kobietami oraz tymi, którzy mogli zrozumieć; a uszy całego ludu były skupione na księdze Prawa.
4 Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume alisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwepo Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
Ezdrasz, uczony w Piśmie, stanął na drewnianym podwyższeniu, które przygotowano na ten cel, a obok niego, po prawej stronie, stali: Mattitiasz, Szema, Ananiasz, Uriasz, Chilkiasz i Maasejasz, a po lewej [stronie]: Pedajasz, Miszael, Malkiasz, Chaszum, Chaszbadana, Zachariasz [i] Meszullam.
5 Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
Ezdrasz otworzył księgę na oczach całego ludu – gdyż stał wyżej niż on – a gdy ją otworzył, cały lud powstał.
6 Ezra akamsifu Bwana, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Bwana hali nyuso zao zikigusa ardhi.
I Ezdrasz błogosławił PANU, wielkiemu Bogu, a cały lud, podnosząc ręce, odpowiadał: Amen! Amen! Potem skłonili głowy i oddali pokłon PANU, padając twarzą ku ziemi.
7 Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafunza ile Sheria: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
Także Jeszua, Bani, Szerebiasz, Jamin, Akkub, Szabbetaj, Hodiasz, Maasejasz, Kelita, Azariasz, Jozabad, Chanan, Pelajasz i Lewici nauczali lud prawa. A lud stał na swoim miejscu.
8 Walisoma kutoka kile Kitabu cha Sheria ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
Czytali więc z księgi Prawa Bożego wyraźnie i wyjaśniali znaczenie tak, żeby zrozumiano to, co czytali.
9 Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Sheria.
Potem Nehemiasz, to [jest] Tirszata, i Ezdrasz, kapłan i uczony w Piśmie, oraz Lewici, którzy nauczali lud, powiedzieli do całego ludu: Ten dzień jest poświęcony PANU, waszemu Bogu. Nie smućcie się ani nie płaczcie. Cały lud bowiem płakał, słuchając słowa Prawa.
10 Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”
I powiedział im: Idźcie, jedzcie tłuste potrawy i pijcie słodki napój, i poślijcie porcje tym, którzy sobie [nic] nie przygotowali. Dzień ten jest bowiem święty dla naszego PANA. Dlatego nie smućcie się, gdyż radość PANA jest waszą siłą.
11 Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
A Lewici uspokajali cały lud, mówiąc: Uciszcie się, bo ten dzień jest święty. Nie smućcie się.
12 Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
Rozszedł się więc cały lud, aby jeść i pić, aby rozsyłać porcje i radować się bardzo, gdyż zrozumiał słowa, które mu ogłoszono.
13 Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa mbari zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Sheria.
Następnego dnia naczelnicy rodów całego ludu, kapłani i Lewici zebrali się wokół Ezdrasza, uczonego w Piśmie, aby zrozumieć słowa Prawa.
14 Wakakuta imeandikwa katika ile Sheria, ambayo Bwana aliiamuru kupitia kwa Mose, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
I znaleźli przepis w Prawie, które PAN nadał przez Mojżesza, aby synowie Izraela mieszkali w szałasach podczas święta siódmego miesiąca;
15 na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Enendeni katika nchi ya mlima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
I aby ogłoszono i obwieszczono we wszystkich ich miastach i w Jerozolimie: Wejdźcie na górę i przynieście gałęzie oliwne, gałęzie sosnowe i gałęzie mirtowe, gałęzie palmowe i gałęzie drzew gęstych, abyście czynili szałasy, jak jest napisane.
16 Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji na uwanja wa Lango la Efraimu.
Lud więc wyszedł i przyniósł [je], i czynił sobie szałasy, każdy na swoim dachu, na swoich dziedzińcach, na dziedzińcach domu Bożego, na placu Bramy Wodnej i na placu Bramy Efraima.
17 Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni mpaka siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
Całe zgromadzenie, wszyscy, którzy powrócili z niewoli, uczynili szałasy i mieszkali w nich, gdyż synowie Izraela nie czynili tego od dni Jozuego, syna Nuna, aż do tego dnia. I panowała wielka radość.
18 Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.
I [Ezdrasz] czytał z księgi Prawa Bożego każdego dnia, od pierwszego dnia aż do ostatniego. Przez siedem dni obchodzili święto, a dnia ósmego [odbyło się] uroczyste zgromadzenie według zwyczaju.

< Nehemia 8 >