< Nehemia 7 >

1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
Wakati ukuta ulipomalizika na milango nimekwisha kuisimamisha, na walinzi wa malango na waimbaji na Walawi walikuwa wamechaguliwa,
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
nikampa ndugu yangu Hanani kuwa na amri juu ya Yerusalemu, pamoja na Hanania ambaye alikuwa msimamizi wa kijiji, kwa kuwa alikuwa mwaminifu na alimuogopa Mungu zaidi kuliko wengi.
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
Nami nikawaambia, Msifungue malango ya Yerusalemu mpaka jua litakapokuwa kali. Wakati walinzi wa mlango wanalinda, unaweza kufunga milango na kuikaza. Chagua walinzi kutoka kwa wale wanaoishi Yerusalemu, wengine mahali pa kituo chao cha ulinzi, na wengine mbele ya nyumba zao wenyewe.
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
Sasa jiji lilikuwa pana na kubwa, lakini kulikuwa na watu wachache ndani yake, na hakuna nyumba zilizojengwa tena.
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
Mungu wangu aliweka moyoni mwangu, kuwakusanya pamoja wakuu, maafisa, na watu kuwaandikisha katika familia zao. Nilipata Kitabu cha kizazi cha wale ambao walirudi kwanza na nikaona kwamba imeandikwa humo.
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
Hawa ndio watu wa jimbo ambao walikwenda kutoka kwenye uhamisho wa wale waliohamishwa ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwachukua mateka. Wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenda kwenye mji wake.
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
Walikuja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana. Idadi ya wana wa Israeli ilikuwa.
8 wazao wa Paroshi 2,172
Wana wa Paroshi, 2, 172.
9 wazao wa Shefatia 372
Wana wa Shefatia, 372.
10 wazao wa Ara 652
Wana wa Ara, 652.
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
Wana wa Pahath Moabu,
12 wazao wa Elamu 1,254
kwa wana wa Yeshua na Yoabu, 2, 818.
13 wazao wa Zatu 845
Wana wa Elamu, 1, 254.
14 wazao wa Zakai 760
Wana wa Zatu, 845. Wana wa Zakai, 760.
15 wazao wa Binui 648
Wana wa Binnui, 648.
16 wazao wa Bebai 628
Wana wa Bebai, 628.
17 wazao wa Azgadi 2,322
Wana wa Azgadi, 2, 322.
18 wazao wa Adonikamu 667
Wana wa Adonikamu, 667.
19 wazao wa Bigwai 2,067
Wana wa Bigwai, 2, 067.
20 wazao wa Adini 655
Wana wa Adini, 655.
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
Wana wa Ateri, wa Hezekia, 98.
22 wazao wa Hashumu 328
Wana wa Hashumu, 328.
23 wazao wa Besai 324
Wana wa Besai, 324.
24 wazao wa Harifu 112
Wana wa Harifu, 112.
25 wazao wa Gibeoni 95
Wana wa Gibeoni, 95.
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
Watu kutoka Bethlehemu na Netofa, 188.
27 watu wa Anathothi 128
Watu wa Anathothi, 128.
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
Watu wa Beth Azmaweth, 42.
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
Watu wa Kiriath Yearimu, Kefira, na Beerothi, 743.
30 watu wa Rama na Geba 621
Watu wa Rama na Geba, 621.
31 watu wa Mikmashi 122
Watu wa Mikmasi, 122.
32 watu wa Betheli na Ai 123
Watu wa Betheli na Ai, 123.
33 watu wa Nebo 52
Watu wa Nebo, 52.
34 wazao wa Elamu 1,254
Watu wa Elamu wa pili, 1, 254.
35 wazao wa Harimu 320
Watu wa Harimu, 320.
36 wazao wa Yeriko 345
Watu wa Yeriko, 345.
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
Watu wa Lodi, Hadidi, na Ono, 721.
38 wazao wa Senaa 3,930
Watu wa Senaa, 3, 930.
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
makuhani Wana wa Yedaya (wa nyumba ya Yeshua), 973.
40 wazao wa Imeri 1,052
Wana wa Imeri, 1, 052.
41 wazao wa Pashuri 1,247
Wana wa Pashuri, 1, 247.
42 wazao wa Harimu 1,017
Wana wa Harimu, 1, 017.
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
Walawi, wana wa Yeshua, wa Kadmieli, wa Binui, wa Hodavia, 74.
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
Waimbaji wana wa Asafu; 148.
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
Waliofungua mlango wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni; wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai, 138.
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
Watumishi wa Hekalu wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi,
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni,
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai,
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
wana wa wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari.
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
Wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda,
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea,
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
wana wa Besai, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu.
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
Wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri,
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
wana wa Baslith, wana wa Mehida, wana wa Harsha,
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema,
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
Wana wa Sulemani, wana wa Sotai, wana wa Sofeereth, wana wa Peruda,
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli,
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokerethi Sebaimu, wana wa Amoni.
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
Watumishi wote wa hekalu, na wana wa watumishi wa Sulemani, walikuwa 392.
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
Hawa ndio watu waliokwenda kutoka Tel Mela, Tel harsha, Kerub, Addon, na Imeri. Lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba wao au jamaa za baba zao walikuwa wana wa Israeli,
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
wana wa Delaya, wana wa Tobia, na wana wa Nekoda, 642.
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
Na kutoka kwa makuhani Wana wa Habaya, Hakosi, na Barzilai ( akamchukua mkewe kutoka kwa binti za Barzilai wa Gileadi na akaitwa kwa jina lao).
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
Hawa walitafuta rekodi zao kati ya waliojiunga na kizazi chao, lakini hawakuweza kupatikana, kwa hivyo waliondolewa katika ukuhani kama walio najisi.
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
Naye mkuu wa gavana akawaambia wasiruhusiwe kula chakula cha makuhani kutoka kwenye dhabihu mpaka atakapoinuka kuhani mwenye Urimu na Thumimu.
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
Kusanyiko lote lilikuwa 42, 360,
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
isipokuwa watumishi wao wa kiume na watumishi wao wa kike, ambao walikuwa 7, 337. Walikuwa na wanaume na wanawake wa kuimba 245.
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
Farasi zao zilikuwa 736 kwa idadi, nyumbu zao, 245,
69 ngamia 435 na punda 6,720.
ngamia zao, 435, na punda zao, 6, 720.
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
Baadhi ya wakuu wa familia za baba zao walitoa zawadi kwa ajili ya kazi. Gavana alitoa sadaka ya darkoni elfu ya dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 ya makuhani.
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
Baadhi ya wakuu wa familia za baba zao waliwapa katika hazina kwa kazi darkroni elfu ishirini za dhahabu na mane 2, 200 za fedha.
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
Watu wengine waliwapa darkoni za dhahabu ishirini elfu, na dhahabu elfu mbili za fedha, na mavazi sitini na saba kwa makuhani.
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
Basi makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, watu wengine, watumishi wa hekalu, na Israeli wote waliishi katika miji yao. Hata mwezi wa saba watu wa Israeli walikuwa wakiishi katika miji yao.”

< Nehemia 7 >