< Nehemia 7 >
1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
城壁が築かれて、とびらを設け、さらに門衛、歌うたう者およびレビびとを任命したので、
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
わたしは、わたしの兄弟ハナニと、城のつかさハナニヤに命じて、エルサレムを治めさせた。彼は多くの者にまさって忠信な、神を恐れる者であったからである。
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
わたしは彼らに言った、「日の暑くなるまではエルサレムのもろもろの門を開いてはならない。人々が立って守っている間に門を閉じさせ、貫の木を差せ。またエルサレムの住民の中から番兵を立てて、おのおのにその所を守らせ、またおのおのの家と向かい合う所を守らせよ」。
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
町は広くて大きかったが、その内の民は少なく、家々はまだ建てられていなかった。
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
時に神はわたしの心に、尊い人々、つかさおよび民を集めて、家系によってその名簿をしらべようとの思いを起された。わたしは最初に上って来た人々の系図を発見し、その中にこのようにしるしてあるのを見いだした。
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
バビロンの王ネブカデネザルが捕え移した捕囚のうち、ゆるされてエルサレムおよびユダに上り、おのおの自分の町に帰ったこの州の人々は次のとおりである。
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
彼らはゼルバベル、エシュア、ネヘミヤ、アザリヤ、ラアミヤ、ナハマニ、モルデカイ、ビルシャン、ミスペレテ、ビグワイ、ネホム、バアナと一緒に帰ってきた者たちである。そのイスラエルの民の人数は次のとおりである。
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
パハテ・モアブの子孫すなわちエシュアとヨアブの子孫は二千八百十八人。
18 wazao wa Adonikamu 667
アドニカムの子孫は六百六十七人。
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
ヒゼキヤの家のアテルの子孫は九十八人。
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
ベツレヘムおよびネトパの人々は百八十八人。
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
ベテ・アズマウテの人々は四十二人。
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
キリアテ・ヤリム、ケピラおよびベエロテの人々は七百四十三人。
30 watu wa Rama na Geba 621
ラマおよびゲバの人々は六百二十一人。
32 watu wa Betheli na Ai 123
ベテルおよびアイの人々は百二十三人。
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
ロド、ハデデおよびオノの人々は七百二十一人。
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
祭司では、エシュアの家のエダヤの子孫が九百七十三人。
41 wazao wa Pashuri 1,247
パシュルの子孫が一千二百四十七人。
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
レビびとでは、エシュアの子孫すなわちホデワの子孫のうちのカデミエルの子孫が七十四人。
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
歌うたう者では、アサフの子孫が百四十八人。
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
門衛では、シャルムの子孫、アテルの子孫、タルモンの子孫、アックブの子孫、ハテタの子孫およびショバイの子孫合わせて百三十八人。
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
宮に仕えるしもべでは、ジハの子孫、ハスパの子孫、タバオテの子孫、
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
ケロスの子孫、シアの子孫、パドンの子孫、
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
レバナの子孫、ハガバの子孫、サルマイの子孫、
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
ハナンの子孫、ギデルの子孫、ガハルの子孫、
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
レアヤの子孫、レヂンの子孫、ネコダの子孫、
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
ガザムの子孫、ウザの子孫、パセアの子孫、
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
ベサイの子孫、メウニムの子孫、ネフセシムの子孫、
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
バクブクの子孫、ハクパの子孫、ハルホルの子孫、
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
バヅリテの子孫、メヒダの子孫、ハルシャの子孫、
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
バルコスの子孫、シセラの子孫、テマの子孫、
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
ネヂアの子孫およびハテパの子孫。
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
ソロモンのしもべであった者たちの子孫では、ソタイの子孫、ソペレテの子孫、ペリダの子孫、
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
ヤアラの子孫、ダルコンの子孫、ギデルの子孫、
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
シパテヤの子孫、ハッテルの子孫、ポケレテ・ハッゼバイムの子孫、アモンの子孫。
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
宮に仕えるしもべたちとソロモンのしもべであった者たちの子孫とは合わせて三百九十二人。
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
テルメラ、テルハレサ、ケルブ、アドンおよびインメルから上って来た者があったが、その氏族と、血統とを示して、イスラエルの者であることを明らかにすることができなかった。その人々は次のとおりである。
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
すなわちデラヤの子孫、トビヤの子孫、ネコダの子孫であって、合わせて六百四十二人。
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
また祭司のうちにホバヤの子孫、ハッコヅの子孫、バルジライの子孫がある。バルジライはギレアデびとバルジライの娘たちのうちから妻をめとったので、その名で呼ばれた。
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
これらの者はこの系図に載った者のうちに、自分の籍をたずねたが、なかったので、汚れた者として祭司の職から除かれた。
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
総督は彼らに告げて、ウリムとトンミムを帯びる祭司の起るまでは、いと聖なる物を食べてはならぬと言った。
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
会衆は合わせて四万二千三百六十人であった。
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
このほかに男女の奴隷が七千三百三十七人、歌うたう者が男女合わせて二百四十五人あった。
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
その馬は七百三十六頭、その騾馬は二百四十五頭、
69 ngamia 435 na punda 6,720.
そのらくだは四百三十五頭、そのろばは六千七百二十頭であった。
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
氏族の長のうち工事のためにささげ物をした人々があった。総督は金一千ダリク、鉢五十、祭司の衣服五百三十かさねを倉に納めた。
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
また氏族の長のうちのある人々は金二万ダリク、銀二千二百ミナを工事のために倉に納めた。
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
その他の民の納めたものは金二万ダリク、銀二千ミナ、祭司の衣服六十七かさねであった。
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
こうして祭司、レビびと、門衛、歌うたう者、民のうちのある人々、宮に仕えるしもべたち、およびイスラエルびとは皆その町々に住んだ。イスラエルの人々はその町々に住んで七月になった。