< Nehemia 7 >

1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
When the wall was finished and I had set up the doors in place, and the gatekeepers and singers and Levites had been appointed,
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
I gave my brother Hanani charge over Jerusalem, along with Hananiah who had oversight of the fortress, for he was a faithful man and feared God more than many.
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
I said to them, “Do not open the gates of Jerusalem until the sun is hot. While the gatekeepers are on guard, you may shut the doors and bar them. Appoint guards from those who live in Jerusalem, some at the place of their guard station, and some in front of their own homes.”
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
Now the city was wide and large, but there were few people within it, and no houses had yet been rebuilt.
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
My God put into my heart to gather together the nobles, the officials, and the people to enroll them by their families. I found the book of the genealogy of those who returned at the first and found the following written in it.
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
“These are the people of the province who went up out of the captivity of those exiles whom Nebuchadnezzar the king of Babylon took into exile. They returned to Jerusalem and to Judah, each to his city.
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
They came with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, and Baanah. The number of the men of the people of Israel included the following.
8 wazao wa Paroshi 2,172
The descendants of Parosh, 2,172.
9 wazao wa Shefatia 372
The descendants of Shephatiah, 372.
10 wazao wa Ara 652
The descendants of Arah, 652.
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
The descendants of Pahath-Moab, through the descendants of Jeshua and Joab, 2,818.
12 wazao wa Elamu 1,254
The descendants of Elam, 1,254.
13 wazao wa Zatu 845
The descendants of Zattu, 845.
14 wazao wa Zakai 760
The descendants of Zakkai, 760.
15 wazao wa Binui 648
The descendants of Binnui, 648.
16 wazao wa Bebai 628
The descendants of Bebai, 628.
17 wazao wa Azgadi 2,322
The descendants of Azgad, 2,322.
18 wazao wa Adonikamu 667
The descendants of Adonikam, 667.
19 wazao wa Bigwai 2,067
The descendants of Bigvai, 2,067.
20 wazao wa Adini 655
The descendants of Adin, 655.
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
The descendants of Ater, of Hezekiah, 98.
22 wazao wa Hashumu 328
The descendants of Hashum, 328.
23 wazao wa Besai 324
The descendants of Bezai, 324.
24 wazao wa Harifu 112
The descendants of Hariph, 112.
25 wazao wa Gibeoni 95
The descendants of Gibeon, 95.
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
The men from Bethlehem and Netophah, 188.
27 watu wa Anathothi 128
The men from Anathoth, 128.
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
The men of Beth Azmaveth, 42.
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
The men of Kiriath Jearim, Kephirah, and Beeroth, 743.
30 watu wa Rama na Geba 621
The men of Ramah and Geba, 621.
31 watu wa Mikmashi 122
The men of Michmas, 122.
32 watu wa Betheli na Ai 123
The men of Bethel and Ai, 123.
33 watu wa Nebo 52
The men of the other Nebo, 52.
34 wazao wa Elamu 1,254
The people of the other Elam, 1,254.
35 wazao wa Harimu 320
The men of Harim, 320.
36 wazao wa Yeriko 345
The men of Jericho, 345.
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
The men of Lod, Hadid, and Ono, 721.
38 wazao wa Senaa 3,930
The men of Senaah, 3,930.
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
The priests: The descendants of Jedaiah (of the house of Jeshua), 973.
40 wazao wa Imeri 1,052
The descendants of Immer, 1,052.
41 wazao wa Pashuri 1,247
The descendants of Pashhur, 1,247.
42 wazao wa Harimu 1,017
The descendants of Harim, 1,017.
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
The Levites: The descendants of Jeshua, of Kadmiel, of Binnui, and of Hodevah, 74.
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
The singers: The descendants of Asaph, 148.
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
The gatekeepers of the descendants of Shallum, the descendants of Ater, the descendants of Talmon, the descendants of Akkub, the descendants of Hatita, the descendants of Shobai, 138.
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
The temple servants: The descendants of Ziha, the descendants of Hasupha, the descendants of Tabbaoth,
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
the descendants of Keros, the descendants of Sia, the descendants of Padon,
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
the descendants of Lebana, the descendants of Hagaba, the descendants of Shalmai,
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
the descendants of Hanan, the descendants of Giddel, the descendants of Gahar.
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
The descendants of Reaiah, the descendants of Rezin, the descendants of Nekoda,
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
the descendants of Gazzam, the descendants of Uzza, the descendants of Paseah,
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
the descendants of Besai, the descendants of Meunim, the descendants of Nephushesim.
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
The descendants of Bakbuk, the descendants of Hakupha, the descendants of Harhur,
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
the descendants of Bazluth, the descendants of Mehida, the descendants of Harsha,
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
the descendants of Barkos, the descendants of Sisera, the descendants of Temah,
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
the descendants of Neziah, the descendants of Hatipha.
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
The descendants of Solomon's servants: the descendants of Sotai, the descendants of Sophereth, the descendants of Perida,
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
the descendants of Jaala, the descendants of Darkon, the descendants of Giddel,
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
the descendants of Shephatiah, the descendants of Hattil, the descendants of Pochereth Hazzebaim, the descendants of Amon.
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
All the temple servants, and the descendants of Solomon's servants, were 392.
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
These were the people who went up from Tel Melah, Tel Harsha, Kerub, Addon, and Immer. But they could not prove that they or their ancestors' families were descendants from Israel:
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
the descendants of Delaiah, the descendants of Tobiah, and the descendants of Nekoda, 642.
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
Those who were from the priests: the descendants of Habaiah, Hakkoz, and Barzillai (who took his wife from the daughters of Barzillai of Gilead and was called by their name).
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
These sought their records among those enrolled by their genealogy, but they could not be found, so they were excluded from the priesthood as unclean.
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
Then the governor said to them that they should not be allowed to eat the priests' share of food from the sacrifices until there rose up a priest with Urim and Thummim.
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
The whole assembly together was 42,360,
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
besides their male servants and their female servants, of whom there were 7,337. They had 245 singing men and women.
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
Their horses were 736 in number, their mules, 245,
69 ngamia 435 na punda 6,720.
their camels, 435, and their donkeys, 6,720.
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
Some from among the heads of ancestors' families gave gifts for the work. The governor gave to the treasury one thousand darics of gold, 50 basins, and 530 priestly garments.
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
Some of the heads of ancestors' families gave into the treasury for the work twenty thousand darics of gold and 2,200 minas of silver.
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
The rest of the people gave twenty thousand darics of gold, and two thousand minas of silver, and sixty-seven priestly garments.
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
So the priests, the Levites, the gatekeepers, the singers, some of the people, the temple servants, and all Israel lived in their cities. By the seventh month the people of Israel were settled in their cities.”

< Nehemia 7 >