< Nehemia 7 >

1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
Now after the wall was built, and I had set up the doors, and numbered the porters and singing men, and Levites:
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
I commanded Hanani my brother, and Hananias ruler of the house of Jerusalem, (for he seemed as a sincere man, and one that feared God above the rest, )
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
And I said to them: Let not the gates of Jerusalem be opened till the sun be hot. And while they were yet standing by, the gates were shut, and barred: and I set watchmen of the inhabitants of Jerusalem, every one by their courses, and every mall over against his house.
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
And the city was very wide and great, and the people few in the midst thereof, and the houses were not built.
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
But God had put in my heart, and I assembled the princes and magistrates, and common people, to number them: and I found a book of the number of them who came up at first, and therein it was found written:
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
These are the children of the province, who came up from the captivity of them that had been carried away, whom Nabuchodonosor the king of Babylon had carried away, and who returned into Judea, every one into his own city.
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
Who came with Zorobabel, Josue, Nehemias, Azarias, Raamias, Nahamani, Mardochai, Belsam, Mespharath, Begoia, Nahum, Baana. The number of the men of the people of Israel:
8 wazao wa Paroshi 2,172
The children of Pharos, two thousand one hundred seventy-two.
9 wazao wa Shefatia 372
The children of Sephatia, three hundred seventy-two.
10 wazao wa Ara 652
The children of Area, six hundred fifty-two.
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
The children of Phahath Moab of the children of Josue and Joab, two thousand eight hundred eighteen.
12 wazao wa Elamu 1,254
The children of Elam, one thousand two hundred fifty-four.
13 wazao wa Zatu 845
The children of Zethua, eight hundred forty-five.
14 wazao wa Zakai 760
The children of Zachai, seven hundred sixty.
15 wazao wa Binui 648
The children of Bannui, six hundred forty-eight.
16 wazao wa Bebai 628
The children of Bebai, six hundred twenty-eight.
17 wazao wa Azgadi 2,322
The children of Azgad, two thousand three hundred twenty-two.
18 wazao wa Adonikamu 667
The children of Adonicam, six hundred sixty-seven.
19 wazao wa Bigwai 2,067
The children of Beguai, two thousand sixty-seven.
20 wazao wa Adini 655
The children of Adin, six hundred fifty-five.
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
The children of Ater, children of Hezechias, ninety-eight.
22 wazao wa Hashumu 328
The children of Hasem, three hundred twenty-eight.
23 wazao wa Besai 324
The children of Besai, three hundred twenty-four.
24 wazao wa Harifu 112
The children of Hareph, a hundred and twelve.
25 wazao wa Gibeoni 95
The children of Gabaon, ninety-five.
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
The children of Bethlehem, and Netupha, a hundred eighty-eight.
27 watu wa Anathothi 128
The men of Anathoth, a hundred twenty-eight.
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
The men of Bethazmoth, forty-two.
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
The men of Cariathiarim, Cephira, and Beroth, seven hundred forty-three.
30 watu wa Rama na Geba 621
The men of Rama and Geba, six hundred twenty-one.
31 watu wa Mikmashi 122
The men of Machmas, a hundred twenty-two.
32 watu wa Betheli na Ai 123
The men of Bethel and Hai, a hundred twenty-three.
33 watu wa Nebo 52
The men of the other Nebo, fifty-two.
34 wazao wa Elamu 1,254
The men of the other Elam, one thousand two hundred fifty-four.
35 wazao wa Harimu 320
The children of Harem, three hundred and twenty.
36 wazao wa Yeriko 345
The children of Jericho, three hundred forty-five.
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
The children of Led, of Hadid and One, seven hundred twenty-one.
38 wazao wa Senaa 3,930
The children of Senaa, three thousand nine hundred thirty.
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
The priests: the children of Idaia in the house of Josue, nine hundred and seventy-three.
40 wazao wa Imeri 1,052
The children of Emmer, one thousand fifty-two.
41 wazao wa Pashuri 1,247
The children of Phashur, one thousand two hundred forty-seven.
42 wazao wa Harimu 1,017
The children of Arem, one thousand and seventeen. The Levites:
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
The children of Josue and Cedmihel, the sons
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
Of Oduia, seventy-four. The singing men:
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
The children of Asaph, a hundred forty-eight.
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
The porters: the children of Sellum, the children of Ater, the children of Telmon, the children of Accub, the children of Hatita, the children of Sobai: a hundred thirty-eight.
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
The Nathinites: the children of Soha, the children of Hasupha, the children of Tebbaoth,
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
The children of Ceros, the children of Siaa, the children of Phadon, the children of Lebana, the children of Hagaba, the children of Selmai,
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
The children of Hanan, the children of Geddel, the children of Gaher,
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
The children of Raaia, the children of Rasin, the children of Necoda,
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
The children of Gezem, the children of Asa, the children of Phasea,
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
The children of Besai, the children of Munim, the children of Nephussim,
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
The children of Bacbuc, the children of Hacupha, the children of Harhur,
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
The children of Besloth, the children of Mahida, the children of Harsa,
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
The children of Bercos, the children of Sisara, the children of Thema,
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
The children of Nasia, the children of Hatipha,
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
The children of the servants of Solomon, the children of Sothai, the children of Sophereth, the children of Pharida,
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
The children of Jahala, the children of Darcon, the children of Jeddel,
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
The children of Saphatia, the children of Hatil, the children of Phochereth, who was born of Sabaim, the son of Amon.
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
All the Nathinites, and the children of the servants of Solomon, three hundred ninety-two.
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
And these are they that came up from Telmela, Thelharsa, Cherub, Addon, and Emmer: and could not shew the house of their fathers, nor their seed, whether they were of Israel.
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
The children of Dalaia, the children of Tobia, the children of Necoda, six hundred forty-two.
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
And of the priests, the children of Habia, the children of Accos, the children of Berzellai, who took a wife of the daughters of Berzellai the Galaadite, and he was called by their name.
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
These sought their writing in the record, and found it not: and they were cast out of the priesthood.
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
And Athersatha said to them, that they should not eat of the holies of holies, until there stood up a priest learned and skillful.
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
All the multitude as it were one man, forty-two thousand three hundred sixty,
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
Beside their menservants and womenservants, who were seven thousand three hundred thirty-seven: and among them singing men, and singing women, two hundred forty-five.
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
Their horses, seven hundred thirty-six: their mules two hundred forty-five:
69 ngamia 435 na punda 6,720.
Their camels, four hundred thirty-five, their asses, six thousand seven hundred and twenty.
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
And some of the heads of the families gave unto the work. Athersatha gave into the treasure a thousand drama of gold, fifty bowls, and five hundred and thirty garments for priests.
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
And some of the heads of families gave to the treasure of the work, twenty thousand drama of gold, and two thousand two hundred pounds of silver.
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
And that which the rest of the people gave, was twenty thousand drama of gold, and two thousand pounds of silver, and sixty-seven garments for priests.
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
And the priests, and the Levites, and the porters, and the singing men, and the rest of the common people, and the Nathinites, and all Israel dwelt in their cities.

< Nehemia 7 >