< Nehemia 7 >
1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
When the wall had been rebuilt and I had set the doors in place, the gatekeepers, singers, and Levites were appointed.
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
Then I put my brother Hanani in charge of Jerusalem, along with Hananiah the commander of the fortress, because he was a faithful man who feared God more than most.
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
And I told them, “Do not open the gates of Jerusalem until the sun is hot. While the guards are on duty, keep the doors shut and securely fastened. And appoint the residents of Jerusalem as guards, some at their posts and some at their own homes.”
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
Now the city was large and spacious, but there were few people in it, and the houses had not yet been rebuilt.
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
Then my God put it into my heart to assemble the nobles, the officials, and the people to be enrolled by genealogy. I found the genealogical register of those who had first returned, and I found the following written in it:
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
These are the people of the province who came up from the captivity of the exiles carried away to Babylon by Nebuchadnezzar its king. They returned to Jerusalem and Judah, each to his own town,
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
accompanied by Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, and Baanah. This is the count of the men of Israel:
the descendants of Parosh, 2,172;
the descendants of Shephatiah, 372;
the descendants of Arah, 652;
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
the descendants of Pahath-moab (through the line of Jeshua and Joab), 2,818;
the descendants of Elam, 1,254;
the descendants of Zattu, 845;
the descendants of Zaccai, 760;
the descendants of Binnui, 648;
the descendants of Bebai, 628;
the descendants of Azgad, 2,322;
18 wazao wa Adonikamu 667
the descendants of Adonikam, 667;
the descendants of Bigvai, 2,067;
the descendants of Adin, 655;
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
the descendants of Ater (through Hezekiah), 98;
the descendants of Hashum, 328;
the descendants of Bezai, 324;
the descendants of Hariph, 112;
the descendants of Gibeon, 95;
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
the men of Bethlehem and Netophah, 188;
the men of Anathoth, 128;
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
the men of Beth-azmaveth, 42;
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
the men of Kiriath-jearim, Chephirah, and Beeroth, 743;
30 watu wa Rama na Geba 621
the men of Ramah and Geba, 621;
the men of Michmash, 122;
32 watu wa Betheli na Ai 123
the men of Bethel and Ai, 123;
the men of the other Nebo, 52;
the descendants of the other Elam, 1,254;
the descendants of Harim, 320;
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
the men of Lod, Hadid, and Ono, 721;
and the descendants of Senaah, 3,930.
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
The priests: the descendants of Jedaiah (through the house of Jeshua), 973;
the descendants of Immer, 1,052;
41 wazao wa Pashuri 1,247
the descendants of Pashhur, 1,247;
and the descendants of Harim, 1,017.
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
The Levites: the descendants of Jeshua (through Kadmiel, through the line of Hodevah ), 74.
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
The singers: the descendants of Asaph, 148.
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
The gatekeepers: the descendants of Shallum, the descendants of Ater, the descendants of Talmon, the descendants of Akkub, the descendants of Hatita, and the descendants of Shobai, 138 in all.
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
The temple servants: the descendants of Ziha, the descendants of Hasupha, the descendants of Tabbaoth,
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
the descendants of Keros, the descendants of Sia, the descendants of Padon,
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
the descendants of Lebanah, the descendants of Hagabah, the descendants of Shalmai,
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
the descendants of Hanan, the descendants of Giddel, the descendants of Gahar,
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
the descendants of Reaiah, the descendants of Rezin, the descendants of Nekoda,
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
the descendants of Gazzam, the descendants of Uzza, the descendants of Paseah,
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
the descendants of Besai, the descendants of Meunim, the descendants of Nephushesim,
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
the descendants of Bakbuk, the descendants of Hakupha, the descendants of Harhur,
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
the descendants of Bazlith, the descendants of Mehida, the descendants of Harsha,
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
the descendants of Barkos, the descendants of Sisera, the descendants of Temah,
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
the descendants of Neziah, and the descendants of Hatipha.
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
The descendants of the servants of Solomon: the descendants of Sotai, the descendants of Sophereth, the descendants of Perida,
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
the descendants of Jaala, the descendants of Darkon, the descendants of Giddel,
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
the descendants of Shephatiah, the descendants of Hattil, the descendants of Pochereth-hazzebaim, and the descendants of Amon.
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
The temple servants and descendants of the servants of Solomon numbered 392 in all.
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
The following came up from Tel-melah, Tel-harsha, Cherub, Addon, and Immer, but could not prove that their families were descended from Israel:
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
the descendants of Delaiah, the descendants of Tobiah, and the descendants of Nekoda, 642 in all.
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
And from among the priests: the descendants of Hobaiah, the descendants of Hakkoz, and the descendants of Barzillai (who had married a daughter of Barzillai the Gileadite and was called by their name).
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
These men searched for their family records, but they could not find them and so were excluded from the priesthood as unclean.
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
The governor ordered them not to eat the most holy things until there was a priest to consult the Urim and Thummim.
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
The whole assembly numbered 42,360,
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
in addition to their 7,337 menservants and maidservants, as well as their 245 male and female singers.
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
They had 736 horses, 245 mules,
69 ngamia 435 na punda 6,720.
435 camels, and 6,720 donkeys.
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
Some of the heads of the families contributed to the project. The governor gave to the treasury 1,000 darics of gold, 50 bowls, and 530 priestly garments.
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
And some of the heads of the families gave to the treasury for the project 20,000 darics of gold and 2,200 minas of silver.
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
The rest of the people gave a total of 20,000 darics of gold, 2,000 minas of silver, and 67 priestly garments.
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
So the priests, Levites, gatekeepers, singers, and temple servants, along with some of the people and the rest of the Israelites, settled in their own towns. And by the seventh month the Israelites had settled in their towns.