< Nehemia 7 >

1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
Now when the wall was built and I had set up the doors, and the gatekeepers and the singers and the Levites were appointed,
2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
I put my brother Hanani, and Hananiah the governor of the fortress, in charge of Jerusalem; for he was a faithful man and feared God above many.
3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
I said to them, “Do not let the gates of Jerusalem be opened until the sun is hot; and while they stand guard, let them shut the doors, and you bar them; and appoint watches of the inhabitants of Jerusalem, everyone in his watch, with everyone near his house.”
4 Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
Now the city was wide and large; but the people were few therein, and the houses were not built.
5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
My God put into my heart to gather together the nobles, and the rulers, and the people, that they might be listed by genealogy. I found the book of the genealogy of those who came up at the first, and I found this written in it:
6 Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
These are the children of the province who went up out of the captivity of those who had been carried away, whom Nebuchadnezzar the king of Babylon had carried away, and who returned to Jerusalem and to Judah, everyone to his city,
7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
who came with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, and Baanah. The number of the men of the people of Israel:
8 wazao wa Paroshi 2,172
The children of Parosh: two thousand one hundred seventy-two.
9 wazao wa Shefatia 372
The children of Shephatiah: three hundred seventy-two.
10 wazao wa Ara 652
The children of Arah: six hundred fifty-two.
11 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
The children of Pahathmoab, of the children of Jeshua and Joab: two thousand eight hundred eighteen.
12 wazao wa Elamu 1,254
The children of Elam: one thousand two hundred fifty-four.
13 wazao wa Zatu 845
The children of Zattu: eight hundred forty-five.
14 wazao wa Zakai 760
The children of Zaccai: seven hundred sixty.
15 wazao wa Binui 648
The children of Binnui: six hundred forty-eight.
16 wazao wa Bebai 628
The children of Bebai: six hundred twenty-eight.
17 wazao wa Azgadi 2,322
The children of Azgad: two thousand three hundred twenty-two.
18 wazao wa Adonikamu 667
The children of Adonikam: six hundred sixty-seven.
19 wazao wa Bigwai 2,067
The children of Bigvai: two thousand sixty-seven.
20 wazao wa Adini 655
The children of Adin: six hundred fifty-five.
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
The children of Ater: of Hezekiah, ninety-eight.
22 wazao wa Hashumu 328
The children of Hashum: three hundred twenty-eight.
23 wazao wa Besai 324
The children of Bezai: three hundred twenty-four.
24 wazao wa Harifu 112
The children of Hariph: one hundred twelve.
25 wazao wa Gibeoni 95
The children of Gibeon: ninety-five.
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
The men of Bethlehem and Netophah: one hundred eighty-eight.
27 watu wa Anathothi 128
The men of Anathoth: one hundred twenty-eight.
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
The men of Beth Azmaveth: forty-two.
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
The men of Kiriath Jearim, Chephirah, and Beeroth: seven hundred forty-three.
30 watu wa Rama na Geba 621
The men of Ramah and Geba: six hundred twenty-one.
31 watu wa Mikmashi 122
The men of Michmas: one hundred twenty-two.
32 watu wa Betheli na Ai 123
The men of Bethel and Ai: one hundred twenty-three.
33 watu wa Nebo 52
The men of the other Nebo: fifty-two.
34 wazao wa Elamu 1,254
The children of the other Elam: one thousand two hundred fifty-four.
35 wazao wa Harimu 320
The children of Harim: three hundred twenty.
36 wazao wa Yeriko 345
The children of Jericho: three hundred forty-five.
37 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
The children of Lod, Hadid, and Ono: seven hundred twenty-one.
38 wazao wa Senaa 3,930
The children of Senaah: three thousand nine hundred thirty.
39 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
The priests: The children of Jedaiah, of the house of Jeshua: nine hundred seventy-three.
40 wazao wa Imeri 1,052
The children of Immer: one thousand fifty-two.
41 wazao wa Pashuri 1,247
The children of Pashhur: one thousand two hundred forty-seven.
42 wazao wa Harimu 1,017
The children of Harim: one thousand seventeen.
43 Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
The Levites: the children of Jeshua, of Kadmiel, of the children of Hodevah: seventy-four.
44 Waimbaji: wazao wa Asafu 148
The singers: the children of Asaph: one hundred forty-eight.
45 Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
The gatekeepers: the children of Shallum, the children of Ater, the children of Talmon, the children of Akkub, the children of Hatita, the children of Shobai: one hundred thirty-eight.
46 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
The temple servants: the children of Ziha, the children of Hasupha, the children of Tabbaoth,
47 wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
the children of Keros, the children of Sia, the children of Padon,
48 wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
the children of Lebana, the children of Hagaba, the children of Salmai,
49 wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
the children of Hanan, the children of Giddel, the children of Gahar,
50 wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
the children of Reaiah, the children of Rezin, the children of Nekoda,
51 wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
the children of Gazzam, the children of Uzza, the children of Paseah,
52 wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
the children of Besai, the children of Meunim, the children of Nephushesim,
53 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
the children of Bakbuk, the children of Hakupha, the children of Harhur,
54 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
the children of Bazlith, the children of Mehida, the children of Harsha,
55 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
the children of Barkos, the children of Sisera, the children of Temah,
56 wazao wa Nesia na Hatifa.
the children of Neziah, and the children of Hatipha.
57 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
The children of Solomon’s servants: the children of Sotai, the children of Sophereth, the children of Perida,
58 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
the children of Jaala, the children of Darkon, the children of Giddel,
59 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
the children of Shephatiah, the children of Hattil, the children of Pochereth Hazzebaim, and the children of Amon.
60 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
All the temple servants and the children of Solomon’s servants were three hundred ninety-two.
61 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
These were those who went up from Tel Melah, Tel Harsha, Cherub, Addon, and Immer; but they could not show their fathers’ houses, nor their offspring, whether they were of Israel:
62 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
The children of Delaiah, the children of Tobiah, the children of Nekoda: six hundred forty-two.
63 Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
Of the priests: the children of Hobaiah, the children of Hakkoz, the children of Barzillai, who took a wife of the daughters of Barzillai the Gileadite, and was called after their name.
64 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
These searched for their genealogical records, but could not find them. Therefore they were deemed disqualified and removed from the priesthood.
65 Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
The governor told them not to eat of the most holy things until a priest stood up to minister with Urim and Thummim.
66 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
The whole assembly together was forty-two thousand three hundred sixty,
67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
in addition to their male servants and their female servants, of whom there were seven thousand three hundred thirty-seven. They had two hundred forty-five singing men and singing women.
68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
Their horses were seven hundred thirty-six; their mules, two hundred forty-five;
69 ngamia 435 na punda 6,720.
their camels, four hundred thirty-five; their donkeys, six thousand seven hundred twenty.
70 Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
Some from among the heads of fathers’ households gave to the work. The governor gave to the treasury one thousand darics of gold, fifty basins, and five hundred thirty priests’ garments.
71 Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
Some of the heads of fathers’ households gave into the treasury of the work twenty thousand darics of gold, and two thousand two hundred minas of silver.
72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
That which the rest of the people gave was twenty thousand darics of gold, plus two thousand minas of silver, and sixty-seven priests’ garments.
73 Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
So the priests, the Levites, the gatekeepers, the singers, some of the people, the temple servants, and all Israel lived in their cities. When the seventh month had come, the children of Israel were in their cities.

< Nehemia 7 >