< Nehemia 6 >
1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
Pripetilo se je torej, ko so Sanbalát, Tobija, Arabec Gešem in ostali izmed naših sovražnikov slišali, da sem zgradil obzidje in da v njem ni ostalo nobene vrzeli (čeprav ob tistem času nisem postavil duri na velika vrata)
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
da sta Sanbalát in Gešem poslala k meni, rekoč: »Pridi, skupaj se srečajmo v eni izmed vasi, na ravnini Onó.« Toda mislila sta mi storiti vragolijo.
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
K njima sem poslal poslance, rekoč: »Jaz opravljam veliko delo, tako da ne morem priti dol. Zakaj bi delo prenehalo, medtem ko ga zapustim in pridem dol k vama?«
4 Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
Vendar sta štirikrat poslala k meni na ta način, jaz pa sem jima odgovoril na isti način.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
Potem je Sanbalát petič k meni poslal svojega služabnika na podoben način, z odprtim pismom v svoji roki,
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
v katerem je bilo zapisano: »Med pogani se govori in Gašmu pravi to, da se ti in Judje mislite upreti, kajti zaradi tega razloga gradiš obzidje, da bi lahko postal njihov kralj, glede na te besede.
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
Določil si tudi preroke, da o tebi oznanjajo v Jeruzalemu, rekoč: › Tam je kralj v Judu.‹ In sedaj bo to sporočeno kralju, glede teh besed. Pridite torej sedaj in skupaj sprejmimo nasvet.«
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
Potem sem poslal k njemu, rekoč: »Tukaj se niso storile nobene takšne stvari, kot ti praviš, temveč si jih hlinil iz svojega lastnega srca.«
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
Kajti oni vsi so nas prestrašili, rekoč: »Njihove roke bodo oslabele od dela, da to ne bo končano.« Sedaj torej, oh Bog, okrepi moje roke.
10 Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
Zatem sem prišel v hišo Šemajája, sinú Delajája, sinú Mehetabéla, ki je bil zaprt. Rekel je: »Skupaj se srečajva v hiši Boga, znotraj templja in zapriva vrata templja, kajti prišli bodo, da te ubijejo. Da, ponoči bodo prišli, da te ubijejo.«
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
Rekel sem: »Ali naj bi takšen človek, kakor sem jaz, bežal? In kdo je tam, ki bi kakor sem jaz, šel v tempelj, da reši svoje življenje? Ne bom šel noter.«
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
Glej, zaznal sem, da ga ni poslal Bog, temveč, da je to prerokbo proglasil zoper mene, kajti najela sta ga Tobija in Sanbalát.
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
Zato je bil najet, da bi bil jaz prestrašen in tako storil in grešil in da bi lahko imela stvar za hudobno poročilo, da bi me lahko grajala.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
Moj Bog, misli na Tobija in Sanbaláta glede na ta njuna dela in na prerokinjo Noádjo in ostale preroke, ki so me hoteli postaviti v strah.
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
Tako je bilo obzidje končano petindvajseti dan meseca elúla, v dvainpetdesetih dneh.
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
Pripetilo se je, da ko so vsi naši sovražniki slišali o tem in so vsi pogani, ki so bili okoli nas, videli te stvari, so bili zelo potrti v svojih lastnih očeh, kajti zaznali so, da je bilo to delo izvršeno od našega Boga.
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
Poleg tega so v tistih dneh Judovi plemiči poslali mnogo pisem Tobiju in pisma od Tobija so prihajala k njim.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
Kajti v Judu so bili mnogi, ki so mu prisegli, ker je bil zet Aráhovega sina Šehanjája in njegov sin Johanán je vzel hčer Berehjájevega sina Mešuláma.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
Pred menoj so poročali tudi njegova dobra dejanja in mu izrekli moje besede. In Tobija je pošiljal pisma, da me postavi v strah.