< Nehemia 6 >

1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
Бысть же егда услыша Санаваллат и Товиа и Гисам Аравийский и прочии врази наши, яко создах стену, и не остася в них скважня: и аз даже до времене онаго дверий не поставих во вратех:
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
и посла Санаваллат и Гисам ко мне, глаголюща: прииди, и соберемся вкупе в весех на поли Оно (глаголемем). Тии же помышляста мне сотворити злое.
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
И послах к нима послов, глаголя: дело велико аз творю и не могу снити, да не престанет дело: егда же совершу е, взыду к вама.
4 Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
И посласта ко мне, якоже глагол сей, четырижды, и послах к нима по сим.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
И присла ко мне Санаваллат пятое отрока своего, и послание отверсто в руку его, и бе написано в нем:
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
во языцех услышано есть, и Гисам рече, яко ты и Иудее мыслите отступити, сего ради ты созидаеши стену, и ты да будеши им в царя:
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
и к сим пророки поставил еси себе, да будеши во Иерусалиме царем над Иудою: и ныне возвестятся царю словеса сия: и сего ради ныне прииди, да сотворима совет вкупе.
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
И послах к нему, глаголя: не сотворися по словесем сим, якоже ты глаголеши, зане от сердца твоего ты лжеши в сих:
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
яко вси страшат нас, глаголюще: ослабеют руцы их от дела сего, и не сотворится: и ныне укрепих руки моя.
10 Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
И аз внидох в дом Семеа сына Далаиева, сына Метавеилева, и той заключен, и рече: да соберемся в дом Божий посреде его и заключим двери его, яко приходят нощию, да убиют тя.
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
И рекох: кто есть муж, яков аз, и убежит? Или кто яко аз, иже внидет в дом, и жив будет? Не вниду.
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
И уразумех, и се, Бог не посла его: яко пророчествова слово на мя.
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
И Товиа и Санаваллат наяста на мя народ, да устрашуся, и сотворю тако, и согрешу, и да буду им во имя зло, яко да поносят ми.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
Помяни, Боже, Товию и Санаваллата по делом их сим, и Ноадиа пророка и прочих пророк, иже страшаху мя.
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
И совершися стена в двадесять пятый месяца Елула в пятьдесят и два дни.
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
И бысть егда услышаша вси врази наши, и убояшася вси языцы, иже окрест нас, и нападе страх велик пред очи их, и познаша, яко от Господа Бога нашего совершено бысть дело сие.
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
И во дни оны от многих державных Иудиных послания прихождаху к Товии, и Товиина (послания) прихождаху к ним.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
Мнози бо во Иудеи кляшася ему, яко зять бе Сехении сына Ираева: и Ионафан сын его поя дщерь Месулама сына Варахиина в жену.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
И словеса его быша глаголющии ко мне, и словеса моя быша износящии ему. И послание посла Товиа, да устрашит мене.

< Nehemia 6 >