< Nehemia 6 >

1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
Forsothe it was doon, whanne Sanaballath hadde herd, and Tobie, and Gosem of Arabie, and oure other enemyes, that Y hadde bildide the wal, and nomore brekyng was therynne; sotheli `til to that tyme Y hadde not set leeuys of schittyng in the yatis;
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
Sanaballath, and Tobie, and Gosem of Arabie senten to me, and seiden, Come thou, and smyte we boond of pees in calues, `in o feeld; forsothe thei thouyten for to do yuel to me.
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
Therfor Y sente messangeris to hem, and Y seide, Y make a greet werk, and Y mai not go doun, lest perauenture it be doon retchelesli, whanne Y come, and go doun to you.
4 Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
Sotheli thei senten to me `bi this word bi foure tymes, and Y answeride to hem by the formere word.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
And Sanaballath sente to me the fyuethe tyme bi the formere word his child; and he hadde in his hond a pistle writun in this maner;
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
It is herd among hethene men, and Gosem seide, that thou and the Jewis thenken for to rebelle, and therfor ye bilden, and thou wolt `reise thee king on hem;
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
for which cause also thou hast set profetis, that prechen of thee in Jerusalem, and seien, A king is in Jerusalem; the king schal here these wordis; therfor come thou now, that we take counsel togidere.
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
And Y sente to hem, and seide, It is not doon bi these wordis whiche thou spekist; for of thin herte thou makist these thingis.
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
Alle these men maden vs aferd, and thouyten that oure hondis schulden ceesse fro werkis, that we schulden reste; for which cause Y coumfortide more myn hond.
10 Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
And Y entride priueli in to the hows of Samaie, sone of Dalie, the sone of Methabehel, which seide, Trete we with vs silf in the hows of God, in the myddis of the temple, and close we the yatis of the hows; for thei schulen come to sle thee, `and thei schulen come `bi niyt to sle thee.
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
And Y seide, Whether ony man lijk me fledde, and who as Y schal entre in to the temple, and schal lyue?
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
Y schal not entre. And Y vndurstood that God `hadde not sent hym, but `he spak as profesiynge to me; and Tobie and Sanaballath `hadden hirid hym for meede.
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
For he hadde take prijs, that Y schulde be aferd, and do, and that Y schulde do synne; and thei schulden haue yuel, which thei schulden putte to me with schenschip.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
Lord, haue mynde of me, for Tobye and Sanaballath, bi siche werkis `of hem; but also of Noadie, the profete, and of othere profetis, that maden me aferd.
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
Forsothe the wal was fillid in the fyue and twentithe dai of the monethe Ebul, in two and fifti daies.
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
Sotheli it was doon, whanne alle oure enemyes hadden herd, that alle hethene men dredden, that weren in oure cumpas, and thei felden doun with ynne hem silf, and wiste, that this work was maad of God.
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
But also in tho daies many pistlis of the principal men of Jewis weren sent to Tobie, and camen fro Tobie to hem.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
For many men weren in Judee, and hadden his ooth; for he hadde weddid the douyter of Sechenye, the sone of Rotel; and Johannam, his sone, hadde take the douyter of Mosallam, sone of Barachie.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
But also thei preisiden hym bifor me, and telden my wordis to hym; and Tobie sente lettris, for to make me aferd.

< Nehemia 6 >