< Nehemia 6 >
1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
And it was just when it was heard by Sanballat and Tobiah and by Geshem the Arab and by [the] rest of enemies our that I had rebuilt the wall and not it was left in it a breach also until the time that doors not I had set up in the gates.
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
And he sent Sanballat and Geshem to me saying come! so let us meet together at Kephirim in [the] plain of Ono and they [were] planning to do to me harm.
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
And I sent! to them messengers saying a work great I [am] doing and not I am able to go down why? will it cease the work when I will let drop it and I will go down to you.
4 Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
And they sent to me according to the manner this four times and I sent back to them according to the manner this.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
And he sent to me Sanballat according to the manner this a time fifth servant his and a letter open [was] in hand his.
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
[was] written In it among the nations it has been heard and Gashmu [is] saying you and the Jews [are] planning to rebel there-fore you [are] rebuilding the wall and you [are] about to become of them king according to the words these.
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
And also prophets you have appointed to proclaim on you in Jerusalem saying a king [is] in Judah and now it will be heard by the king according to the words these and therefore come! so let us take counsel together.
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
And I sent! to him saying not it has occurred according to the words these which you [are] saying that from heart your you [are] inventing them.
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
For all of them [were] making afraid us saying they will drop hands their from the work and not it will be done and therefore strengthen hands my.
10 Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
And I I went [the] house of Shemaiah [the] son of Delaiah [the] son of Mehetabel and he [was] shut up and he said let us meet to [the] house of God to [the] middle of the temple and let us close [the] doors of the temple for [people are] coming to kill you and night [people are] coming to kill you.
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
And I said! ¿ a man like me will he flee and who? [is] like me who he will go into the temple and he will live not I will go.
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
And I recognized! and there! not God he had sent him for the prophecy he had spoken on me and Tobiah and Sanballat he had hired him.
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
So that [was] hired he so that I may be afraid and I may act thus and I will sin and it will become for them a name bad so that they may reproach me.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
Remember! O God my to Tobiah and to Sanballat according to works his these and also Noadiah the prophetess and to [the] rest of the prophets who they were making afraid me.
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
And it was complete the wall on [day] twenty and five of Elul to fifty and two day[s].
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
And it was just when they heard all enemies our and they were afraid all the nations which [were] around us and they fell exceedingly in own eyes their and they knew that from with God our it had been done the work this.
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
Also - in the days those [were] multiplying [the] nobles of Judah letters their [which were] going to Tobiah and [those] which [belonged] to Tobiah [were] coming to them.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
For many [people] in Judah [were] lords of oath to him for [was] a son-in-law he of Shecaniah [the] son of Arah and Jehohanan son his he had taken [the] daughter of Meshullam [the] son of Berekiah.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
Also good deeds his they were telling before me and words my they were sending out to him letters he sent Tobiah to make afraid me.