< Nehemia 5 >

1 Wakati huu wanaume na wake zao wakalia kilio kikuu dhidi ya ndugu zao Wayahudi.
Et il y eut un grand cri du peuple et de leurs femmes, contre les Juifs leurs frères.
2 Baadhi yao walikuwa wakisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tuko wengi. Ili tuweze kula na kuishi, ni lazima tupate nafaka.”
Et les uns disaient: Nous sommes en grand nombre avec nos fils et nos filles, vendons-en; puis nous achèterons du blé, et nous mangerons, et nous vivrons.
3 Wengine walikuwa wakisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mashamba ya mizabibu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
Et d'autres disaient: Engageons nos champs, nos vignes, nos maisons; puis, nous achèterons du blé, et nous mangerons.
4 Bado kukawa na wengine waliokuwa wakisema, “Ilitubidi tukope fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa ajili ya mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
D'autres encore disaient: Nous avons emprunté de l'argent pour les impôts du roi, sur nos champs, et nos vignes, et nos maisons.
5 Ingawa sisi ni mwili na damu moja sawa na watu wa nchi yetu, na ijapo wana wetu ni wazuri kama wana wao, bado inatupasa kuwatoa wana wetu na binti zetu kwenye utumwa. Baadhi ya binti zetu wameshakuwa watumwa tayari, lakini hatuna uwezo wa kuwakomboa, kwa sababu mashamba yetu na mashamba ya mizabibu yetu ni mali ya wengine.”
Et maintenant, notre chair est comme la chair de nos frères; nos fils sont comme leurs fils, et nous traitons nos fils et nos filles comme des esclaves; et il y a de nos filles qui sont servantes, et nous n'avons pas le pouvoir de les racheter; car les nobles possèdent nos champs et nos vignes.
6 Niliposikia kilio chao na malalamiko haya, nilikasirika sana.
Et j'eus une grande affliction, quand j'ouïs leur clameur et ces discours;
7 Nikayatafakari katika akili yangu, nikiwalaumu wakuu na maafisa. Nikawaambia, “Mnawaonea ndugu zenu kwa kuwatoza riba!” Basi nikaitisha mkutano mkubwa ili kuwashughulikia
Et je tins conseil en mon cœur, et je combattis les nobles et les princes, et je leur dis: Un homme peut-il demander à son frère ce que vous demandez? Et je convoquai contre eux une grande assemblée.
8 na kusema: “Kulingana na uwezo wetu, tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi waliokuwa wameuzwa kwa watu wasioamini. Sasa mnawauza ndugu zenu, ili wauzwe tena kwetu!” Walinyamaza kimya, kwa sababu hawakupata chochote cha kusema.
Et je leur dis: Nous avons, de nos dons volontaires, racheté nos frères les Juifs qui avaient été vendus aux gentils, et vous vendez vos frères; mais vous seront-ils livrés? Et ils gardèrent le silence, et ils ne trouvèrent pas un mot à dire.
9 Basi nikaendelea kusema, “Mnachokifanya si sawa. Je, haikuwapasa kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili tuepukane na shutuma za adui zetu wasioamini?
Et je dis: Elle n'est pas bonne l'action que vous faites; ce n'est pas ainsi que vous vous soustrairez, par la crainte de Dieu, aux outrages des nations, vos ennemies.
10 Mimi na ndugu zangu na watu wangu tunawakopesha watu fedha na nafaka. Lakini jambo hili la kutoza riba likome!
Or, mes frères, mes parents et moi-même, nous leurs avons prêté de l'argent et du blé; eh bien! renonçons à rien exiger d'eux.
11 Warudishieni mara moja mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, pia riba yao mnayowatoza na sehemu ya fungu la mia la fedha, nafaka, divai mpya na mafuta.”
Rendez-leur dès aujourd'hui leurs champs, leurs vignes, leurs oliviers et leurs maisons; et apportez-leur du blé, du vin et de l'huile pour prix de l'argent.
12 Wakasema, “Tutawarudishia na hatutataka kitu chochote zaidi kutoka kwao. Tutafanya kama ulivyosema.” Kisha nikawaita makuhani na kuwafanya wakuu na maafisa kuapa kufanya kile walichoahidi.
Et ils dirent: Nous rendrons tout; nous ne leur demanderons rien, et nous ferons ce que tu dis. Et j'appelai les prêtres, et je les adjurai de faire selon cette parole.
13 Pia nikakungʼuta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkungʼute hivi kutoka nyumba yake na katika mali zake. Basi mtu wa namna hiyo akungʼutiwe nje na aachwe bila kitu!” Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza Bwana. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Et je secouai mon manteau, et je dis: Que Dieu ainsi secoue hors de sa maison et de son jardin tout homme qui n'accomplira pas cette parole; que cet homme soit ainsi secoué et vide. Et toute l'Église dit: Amen. Et ils louèrent le Seigneur, et le peuple fit comme il avait été dit.
14 Zaidi ya hayo, kutoka mwaka wa ishirini wa Mfalme Artashasta, wakati nilipoteuliwa kuwa mtawala wao katika nchi ya Yuda, mpaka mwaka wake wa thelathini na mbili, yaani miaka kumi na miwili, mimi wala ndugu zangu hatukula chakula ambacho kwa kawaida hupewa watawala.
Depuis le jour où le roi m'avait commandé d'être leur chef en la terre de Juda: de la vingtième à la trente-deuxième année du règne d'Arthasastha, pendant douze ans, ni moi ni mes frères nous ne mangeâmes de vivres extorqués d'eux.
15 Lakini watawala wa mwanzoni, wale walionitangulia, waliwalemea watu na kuchukua kutoka kwao shekeli arobaini za fedha, pamoja na chakula na mvinyo. Wasaidizi wao pia walijifanya wakuu juu ya watu. Lakini kwa kumheshimu Mungu sikufanya hivyo.
Et toutes les extorsions dont mes devanciers les grevaient avant moi, leur avaient enlevé jusqu'à leur dernier argent; ils leur prenaient pour le pain et le vin quarante sicles par jour; et leurs agents avaient toute autorité sur le peuple; et moi je ne fis pas ainsi, en face de la crainte de Dieu.
16 Badala yake, nilijitoa kwa bidii katika kazi ya ukuta huu. Watu wangu wote walikutanika pale kwa ajili ya kazi. Hatukujipatia shamba lolote.
Et, pendant la réédification des murailles, je ne leur extorquai rien, je n'achetai point de champ, non plus qu'aucun de ceux que j'avais rassemblés pour cette œuvre.
17 Zaidi ya hayo, Wayahudi na maafisa 150 walikula mezani pangu, pamoja na wale waliotujia kutoka mataifa jirani.
Et les Juifs, au nombre de cent cinquante, et ceux des gentils qui venaient d'alentour auprès de nous, mangeaient à ma table.
18 Kila siku niliandaliwa maksai mmoja, kondoo sita wazuri, na kuku, na mvinyo wa kila aina kwa wingi kila baada ya siku kumi. Licha ya mambo haya yote, sikudai chakula kilichokuwa fungu la mtawala, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana kwa watu hawa.
Et tous les jours on m'amenait un bœuf, six brebis de choix et un chevreau. Et, tous les dix jours, il me venait pour nous tous une ample provision de vin; et, avec tout cela, je ne pris jamais de vivres par extorsion, parce que la servitude avait été pesante pour le peuple.
19 Unikumbuke kwa fadhili, Ee Mungu wangu, kwa yote niliyofanya kwa ajili ya watu hawa.
Souvenez-vous de moi, mon Dieu, pour mon bien, à cause de tout ce que j'ai fait en faveur de ce peuple.

< Nehemia 5 >