< Nehemia 5 >
1 Wakati huu wanaume na wake zao wakalia kilio kikuu dhidi ya ndugu zao Wayahudi.
Alors s'éleva un grand cri du peuple et de ses femmes contre leurs frères les Juifs.
2 Baadhi yao walikuwa wakisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tuko wengi. Ili tuweze kula na kuishi, ni lazima tupate nafaka.”
Car il y en avait qui disaient: « Nous, nos fils et nos filles, nous sommes nombreux. Allons chercher du blé, afin de manger et de vivre. »
3 Wengine walikuwa wakisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mashamba ya mizabibu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
Il y en avait aussi qui disaient: « Nous hypothéquons nos champs, nos vignes et nos maisons. Allons chercher du blé, à cause de la famine. »
4 Bado kukawa na wengine waliokuwa wakisema, “Ilitubidi tukope fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa ajili ya mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
Il y en avait aussi qui disaient: « Nous avons emprunté de l'argent pour le tribut du roi en utilisant nos champs et nos vignes comme garantie.
5 Ingawa sisi ni mwili na damu moja sawa na watu wa nchi yetu, na ijapo wana wetu ni wazuri kama wana wao, bado inatupasa kuwatoa wana wetu na binti zetu kwenye utumwa. Baadhi ya binti zetu wameshakuwa watumwa tayari, lakini hatuna uwezo wa kuwakomboa, kwa sababu mashamba yetu na mashamba ya mizabibu yetu ni mali ya wengine.”
Mais maintenant, notre chair est comme la chair de nos frères, nos enfants comme leurs enfants. Et voici que nous amenons nos fils et nos filles en esclavage pour les asservir, et certaines de nos filles ont été amenées en esclavage. Il n'est pas non plus en notre pouvoir d'y remédier, car d'autres hommes possèdent nos champs et nos vignes. »
6 Niliposikia kilio chao na malalamiko haya, nilikasirika sana.
J'ai été très irrité quand j'ai entendu leur cri et ces paroles.
7 Nikayatafakari katika akili yangu, nikiwalaumu wakuu na maafisa. Nikawaambia, “Mnawaonea ndugu zenu kwa kuwatoza riba!” Basi nikaitisha mkutano mkubwa ili kuwashughulikia
Alors je me consultai, je contestai avec les nobles et les chefs, et je leur dis: « Vous exigez l'usure, chacun de son frère. » Je tins une grande assemblée contre eux.
8 na kusema: “Kulingana na uwezo wetu, tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi waliokuwa wameuzwa kwa watu wasioamini. Sasa mnawauza ndugu zenu, ili wauzwe tena kwetu!” Walinyamaza kimya, kwa sababu hawakupata chochote cha kusema.
Je leur dis: « Nous avons racheté, selon notre capacité, nos frères les Juifs qui avaient été vendus aux nations; et vous, voulez-vous même vendre vos frères, et qu'ils soient vendus à nous? » Alors ils se turent, et ne trouvèrent pas un mot à dire.
9 Basi nikaendelea kusema, “Mnachokifanya si sawa. Je, haikuwapasa kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili tuepukane na shutuma za adui zetu wasioamini?
Je dis aussi: « Ce que vous faites n'est pas bien. Ne devriez-vous pas marcher dans la crainte de notre Dieu, à cause de l'opprobre des nations, nos ennemies?
10 Mimi na ndugu zangu na watu wangu tunawakopesha watu fedha na nafaka. Lakini jambo hili la kutoza riba likome!
Moi aussi, mes frères et mes serviteurs, je leur prête de l'argent et du blé. De grâce, cessons cette usure.
11 Warudishieni mara moja mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, pia riba yao mnayowatoza na sehemu ya fungu la mia la fedha, nafaka, divai mpya na mafuta.”
Rendez-leur, je vous prie, dès aujourd'hui, leurs champs, leurs vignes, leurs oliviers et leurs maisons, ainsi que le centième de l'argent, du blé, du vin nouveau et de l'huile que vous leur faites payer. »
12 Wakasema, “Tutawarudishia na hatutataka kitu chochote zaidi kutoka kwao. Tutafanya kama ulivyosema.” Kisha nikawaita makuhani na kuwafanya wakuu na maafisa kuapa kufanya kile walichoahidi.
Ils dirent alors: « Nous les rétablirons, et nous ne leur demanderons rien. Nous le ferons, comme tu le dis. » Puis j'appelai les sacrificateurs, et je leur fis jurer qu'ils accompliraient cette promesse.
13 Pia nikakungʼuta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkungʼute hivi kutoka nyumba yake na katika mali zake. Basi mtu wa namna hiyo akungʼutiwe nje na aachwe bila kitu!” Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza Bwana. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
Je secouai aussi mes genoux, et je dis: « Que Dieu secoue tout homme de sa maison et de son travail, qui n'accomplit pas cette promesse, qu'il soit secoué et vidé comme cela. » Toute l'assemblée dit: « Amen » et loua Yahvé. Le peuple s'est conformé à cette promesse.
14 Zaidi ya hayo, kutoka mwaka wa ishirini wa Mfalme Artashasta, wakati nilipoteuliwa kuwa mtawala wao katika nchi ya Yuda, mpaka mwaka wake wa thelathini na mbili, yaani miaka kumi na miwili, mimi wala ndugu zangu hatukula chakula ambacho kwa kawaida hupewa watawala.
De plus, depuis que j'ai été désigné pour être leur gouverneur dans le pays de Juda, depuis la vingtième année jusqu'à la trente-deuxième année du roi Artaxerxès, c'est-à-dire douze ans, moi et mes frères n'avons pas mangé le pain du gouverneur.
15 Lakini watawala wa mwanzoni, wale walionitangulia, waliwalemea watu na kuchukua kutoka kwao shekeli arobaini za fedha, pamoja na chakula na mvinyo. Wasaidizi wao pia walijifanya wakuu juu ya watu. Lakini kwa kumheshimu Mungu sikufanya hivyo.
Mais les anciens gouverneurs qui m'ont précédé étaient soutenus par le peuple, et ils prenaient de lui du pain et du vin, plus quarante sicles d'argent; oui, même leurs serviteurs régnaient sur le peuple, mais moi, je n'ai pas agi ainsi, à cause de la crainte de Dieu.
16 Badala yake, nilijitoa kwa bidii katika kazi ya ukuta huu. Watu wangu wote walikutanika pale kwa ajili ya kazi. Hatukujipatia shamba lolote.
Oui, j'ai aussi poursuivi les travaux de cette muraille. Nous n'avons pas acheté de terres. Tous mes serviteurs étaient réunis là pour l'ouvrage.
17 Zaidi ya hayo, Wayahudi na maafisa 150 walikula mezani pangu, pamoja na wale waliotujia kutoka mataifa jirani.
De plus, il y avait à ma table, parmi les Juifs et les chefs, cent cinquante hommes, sans compter ceux qui étaient venus chez nous d'entre les nations qui nous entouraient.
18 Kila siku niliandaliwa maksai mmoja, kondoo sita wazuri, na kuku, na mvinyo wa kila aina kwa wingi kila baada ya siku kumi. Licha ya mambo haya yote, sikudai chakula kilichokuwa fungu la mtawala, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana kwa watu hawa.
Or, ce qui a été préparé pour un jour, c'est un bœuf et six brebis de choix. On me préparait aussi des volailles, et une fois tous les dix jours une réserve de vin de toutes sortes. Mais pour tout cela, je n'ai pas exigé la solde du gouverneur, car la servitude était lourde pour ce peuple.
19 Unikumbuke kwa fadhili, Ee Mungu wangu, kwa yote niliyofanya kwa ajili ya watu hawa.
Souviens-toi de moi, mon Dieu, pour tout le bien que j'ai fait à ce peuple.