< Nehemia 3 >

1 Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
E levantou-se Eliasib, o sumo sacerdote, com os seus irmãos, os sacerdotes, e edificaram a porta do gado, a qual consagraram; e levantaram as suas portas: e até a torre de Meah consagraram, e até a torre de Hananel.
2 Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
E junto a ele edificaram os homens de Jericó: também ao seu lado edificou Zaccur, filho de Imri.
3 Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
E a porta do peixe edificaram os filhos de Senaa; a qual emadeiraram, e levantaram as suas portas com as suas fechaduras e os seus ferrolhos.
4 Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
E ao seu lado reparou Meremoth, filho de Urias, o filho de Kós; e ao seu lado reparou Mesullam, filho de Berechias, o filho de Mesezabel; e ao seu lado reparou Zadok, filho de Baana.
5 Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
E ao seu lado repararam os tekoitas: porém os seus ilustres não meteram o seu pescoço ao serviço de seu senhor.
6 Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
E a porta velha repararam-na Joiada, filho de Paseah, e Mesullam, filho de Besodias: estes a emadeiraram, e levantaram as suas portas com as suas fechaduras e os seus ferrolhos.
7 Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
E ao seu lado repararam Melatias, o gibeonita, e Jadon, meronothita, homens de Gibeon e Mispah, até ao assento do governador de aquém do rio.
8 Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
Ao seu lado reparou Uziel, filho de Harhaias, um dos ourives; e ao seu lado reparou Hananias, filho dum dos boticários; e deixaram a Jerusalém até ao muro largo.
9 Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
E ao seu lado reparou Rephaias, filho de Hur, maioral de metade de Jerusalém.
10 Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
E ao seu lado reparou Jedaias, filho de Harumaph, e defronte de sua casa; e ao seu lado reparou Hattus, filho de Hasabneias.
11 Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
A outra porção reparou Malchias, filho de Harim, e Hasub, filho de Pahathmoab: como também a torre dos fornos.
12 Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
E ao seu lado reparou Sallum, filho de Lohes, maioral da outra meia parte de Jerusalém, ele e suas filhas.
13 Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
A porta do vale reparou-a Hanun e os moradores de Zanoah: estes a edificaram, e lhe levantaram as portas com as suas fechaduras e os seus ferrolhos, como também mil côvados no muro, até à porta do monturo.
14 Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
E a porta do monturo reparou-a Malchias, filho de Rechab, maioral do distrito de Beth-cherem: este a edificou, e lhe levantou as portas com as suas fechaduras e os seus ferrolhos.
15 Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
E a porta da fonte reparou-a Sallum, filho de Col-hose, maioral do distrito de Mispah: este a edificou, e a cobriu, e lhe levantou as portas com as suas fechaduras e os seus ferrolhos, como também o muro do viveiro de Selah, ao pé do jardim do rei, e até aos degraus que descem da cidade de David.
16 Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
Depois dele edificou Nehemias, filho de Azbuk, maioral da metade de Beth-zur, até defronte dos sepulcros de David, e até ao viveiro artificial, e até à casa dos varões.
17 Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
Depois dele repararam os levitas, Rehum, filho de Bani: ao seu lado reparou Hasabias, maioral da metade de Keila, no seu distrito.
18 Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
Depois dele repararam seus irmãos, Bavai, filho de Henadad, maioral da outra meia parte de Keila.
19 Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
Ao seu lado reparou Ezer, filho de Josué, maioral de Mispah, outra porção, defronte da subida à casa das armas, à esquina.
20 Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
Depois dele reparou com grande ardor Baruch, filho de Zabbai, outra medida, desde a esquina até à porta da casa de Eliasib, o sumo sacerdote.
21 Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
Depois dele reparou Meremoth, filho de Urias, o filho de Kos, outra porção, desde a porta da casa de Eliasib, até à extremidade da casa de Eliasib.
22 Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
E depois dele repararam os sacerdotes que habitavam na campina.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
Depois reparou Benjamin e Hasub, defronte da sua casa: depois dele reparou Azarias, filho de Maaseias, o filho de Ananias, junto à sua casa.
24 Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
Depois dele reparou Binnui, filho de Henadad, outra porção, desde a casa d'Azarias até à esquina, e até ao canto.
25 Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
Palal, filho de Uzai, defronte da esquina, e a torre que sai da casa real superior, que está junto ao pátio da prisão: depois dele Pedaias, filho de Parós.
26 na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
E os nethineos que habitavam em Ophel, até defronte da porta das águas, para o oriente, e até à torre alta.
27 Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
Depois repararam os tekoitas outra porção, defronte da torre grande e alta, e até ao muro d'Ophel.
28 Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
Desde acima da porta dos cavalos repararam os sacerdotes, cada um defronte da sua casa.
29 Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
Depois deles reparou Zadok, filho de Immer, defronte de sua casa: e depois dele reparou Semaias, filho de Sechanias, guarda da porta oriental.
30 Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
Depois dele reparou Hananias, filho de Selemias, e Hanun, filho de Zalaph, o sexto, outra porção: depois dele reparou Mesullam, filho de Berechias, defronte da sua câmara.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
Depois dele reparou Malchias, filho dum ourives, até à casa dos nethineos e mercadores, defronte da porta de Miphkad, e até à câmara do canto.
32 Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.
E entre a câmara do canto e a porta do gado, repararam os ourives e os mercadores.

< Nehemia 3 >