< Nehemia 3 >

1 Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
and to arise: rise Eliashib [the] priest [the] great: large and brother: male-relative his [the] priest and to build [obj] gate [the] Sheep (Gate) they(masc.) to consecrate: consecate him and to stand: stand door his and till Tower (of the Hundred) [the] (Tower of) the Hundred to consecrate: consecate him till tower (Tower of) Hananel
2 Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
and upon hand: themselves his to build human Jericho and upon hand: themselves his to build Zaccur son: child Imri
3 Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
and [obj] gate [the] Fish (Gate) to build son: child [the] Senaah they(masc.) to lay beams him and to stand: stand door his bolt his and bar his
4 Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Meremoth son: child Uriah son: child Hakkoz and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Meshullam son: child Berechiah son: child Meshezabel and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Zadok son: child Baana
5 Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen [the] Tekoa and great their not to come (in): come neck their in/on/with service lord their
6 Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
and [obj] gate [the] (Gate of) Yeshanah to strengthen: strengthen Joiada son: child Paseah and Meshullam son: child Besodeiah they(masc.) to lay beams him and to stand: stand door his and bolt his and bar his
7 Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Melatiah [the] Gibeonite and Jadon [the] Meronothite human Gibeon and [the] Mizpah to/for throne: seat governor side: beside [the] River
8 Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
upon hand: themselves his to strengthen: strengthen Uzziel son: child Harhaiah to refine and upon hand: themselves his to strengthen: strengthen Hananiah son: type of [the] perfumer and to restore Jerusalem till [the] (Broad) Wall [the] Broad
9 Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Rephaiah son: child Hur ruler half district Jerusalem
10 Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
and upon hand: themselves their to strengthen: strengthen Jedaiah son: child Harumaph and before house: home his and upon hand: themselves his to strengthen: strengthen Hattush son: child Hashabneiah
11 Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
measure second to strengthen: strengthen Malchijah son: child Harim and Hasshub son: child Pahath-moab Pahath-moab and [obj] Tower (Of the Ovens) [the] (Tower of) the Ovens
12 Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
and upon hand: themselves his to strengthen: strengthen Shallum son: child Hallohesh ruler half district Jerusalem he/she/it and daughter his
13 Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
[obj] gate [the] Valley (Gate) to strengthen: strengthen Hanun and to dwell Zanoah they(masc.) to build him and to stand: stand door his bolt his and bar his and thousand cubit in/on/with wall till gate [the] Dung (Gate)
14 Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
and [obj] gate [the] Dung (Gate) to strengthen: strengthen Malchijah son: child Rechab ruler district Beth-haccherem Beth-haccherem he/she/it to build him and to stand: stand door his bolt his and bar his
15 Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
and [obj] gate [the] Fountain (Gate) to strengthen: strengthen Shallum son: child Col-hozeh Col-hozeh ruler district [the] Mizpah he/she/it to build him and to cover him (and to stand: stand *Q(K)*) door his bolt his and bar his and [obj] wall pool [the] Shelah to/for garden [the] king and till [the] step [the] to go down from city David
16 Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
after him to strengthen: strengthen Nehemiah son: child Azbuk ruler half district Beth-zur Beth-zur till before grave David and till [the] pool [the] to make and till house: home [the] mighty man
17 Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
after him to strengthen: strengthen [the] Levi Rehum son: child Bani upon hand: themselves his to strengthen: strengthen Hashabiah ruler half district Keilah to/for district his
18 Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
after him to strengthen: strengthen brother: male-relative their Bavvai son: child Henadad ruler half district Keilah
19 Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
and to strengthen: strengthen upon hand: themselves his Ezer son: child Jeshua ruler [the] Mizpah measure second from before to ascend: rise [the] weapon [the] corner
20 Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
after him to be incensed to strengthen: strengthen Baruch son: child (Zaccai *Q(K)*) measure second from [the] corner till entrance house: home Eliashib [the] priest [the] great: large
21 Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
after him to strengthen: strengthen Meremoth son: child Uriah son: child Hakkoz measure second from entrance house: home Eliashib and till limit house: home Eliashib
22 Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
and after him to strengthen: strengthen [the] priest human [the] talent
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
after him to strengthen: strengthen Benjamin and Hasshub before house: home their after him to strengthen: strengthen Azariah son: child Maaseiah son: child Ananiah beside house: home his
24 Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
after him to strengthen: strengthen Binnui son: child Henadad measure second from house: home Azariah till [the] corner and till [the] corner
25 Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
Palal son: child Uzai from before [the] corner and [the] tower [the] to come out: issue from house: home [the] king [the] high which to/for court [the] guardhouse after him Pedaiah son: child Parosh
26 na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
and [the] temple servant to be to dwell in/on/with Ophel till before gate [the] Water (Gate) to/for east and [the] tower [the] to come out: issue
27 Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
after him to strengthen: strengthen [the] Tekoa measure second from before [the] tower [the] great: large [the] to come out: issue and till wall [the] Ophel
28 Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
from upon gate [the] Horse (Gate) to strengthen: strengthen [the] priest man: anyone to/for before house: home his
29 Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
after him to strengthen: strengthen Zadok son: child Immer before house: home his and after him to strengthen: strengthen Shemaiah son: child Shecaniah to keep: guard gate [the] East (Gate)
30 Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
(after him *Q(K)*) to strengthen: strengthen Hananiah son: child Shelemiah and Hanun son: child Zalaph [the] sixth measure second after him to strengthen: strengthen Meshullam son: child Berechiah before chamber his
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
(after him *Q(K)*) to strengthen: strengthen Malchijah son: descendant/people [the] goldsmith till house: home [the] temple servant and [the] to trade before gate [the] Muster (Gate) and till upper room [the] corner
32 Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.
and between upper room [the] corner to/for gate [the] Sheep (Gate) to strengthen: strengthen [the] to refine and [the] to trade

< Nehemia 3 >