< Nehemia 3 >
1 Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
Og Eliasib, Ypperstepræsten, og hans Brødre, Præsterne, gjorde sig rede og byggede Faareporten; de helligede den og indsatte dens Døre, de helligede den indtil Meas Taarn, indtil Hananeels Taarn.
2 Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
Og Jerikos Mænd byggede ved Siden af ham; og Sakur, Imris Søn, byggede ved Siden af dem igen.
3 Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
Men Senaas Børn byggede Fiskeporten; de tømrede den og indsatte dens Døre med dens Laase og dens Stænger.
4 Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
Og Meremoth, en Søn af Uria, Hakkoz's Søn, istandsatte et Stykke ved Siden af dem; og Mesullam, en Søn af Berekia, Mesesabeels Søn, istandsatte et Stykke ved Siden af dem; og Zadok, Baenas Søn, istandsatte et Stykke ved Siden af dem.
5 Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
Og ved Siden af dem istandsatte de af Thekoa et Stykke; men de store iblandt dem bøjede ikke deres Hals til Arbejde for deres Herre.
6 Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
Og den gamle Port istandsatte Jojada, Paseas Søn, og Mesullam, Besodias Søn; de tømrede den og indsatte dens Døre med dens Laase og dens Stænger.
7 Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
Og Gibeoniten Melathia og Meronothiten Jadon, Mændene af Gibeon og Mizpa istandsatte et Stykke ved Siden af dem, indtil Boligen for Landshøvdingen paa denne Side Floden.
8 Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
Ved hans Side istandsatte Ussiel, Harhajas Søn, en af Guldsmedene, et Stykke; og ved hans Side istandsatte Hanania, en Salvehandler, et Stykke; og de gjorde Jerusalem fast indtil den brede Mur.
9 Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
Og ved Siden at dem istandsatte Refaja, Hurs Søn, Øversten over Halvdelen af Jerusalems Kreds, et Stykke.
10 Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
Og ved Siden af dem istandsatte Jedaja, Harumafs Søn, et Stykke, og det tværs over for sit Hus; og ved hans Side istandsatte Hattus, Hasabenjas Søn, et Stykke.
11 Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
Malkia, Harims Søn, og Hasub, Pahath-Moabs Søn, istandsatte en anden Strækning, tilmed Ovntaarnet.
12 Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
Og ved Siden af ham istandsatte Sallum, Lohes's Søn, Øversten for den halve Del af Jerusalems Kreds, han og hans Døtre, et Stykke.
13 Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
Dalporten istandsatte Hanun og Indbyggerne af Sanoa; de byggede den og indsatte dens Døre, med dens Laase og dens Stænger, og tusinde Alen paa Muren indtil Møgporten.
14 Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
Men Malkia, Rekabs Søn, Øversten for Beth-Kerems Kreds, istandsatte Møgporten; han byggede den og indsatte dens Døre med dens Laase og Stænger.
15 Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
Men Kildeporten istandsatte Sallum, Kol-Koses Søn, Øversten for Mizpas Kreds; han byggede den og tækkede den og indsatte dens Døre med dens Laase og dens Stænger; tilmed Muren ved Sela Dam hen imod Kongens Have og indtil Trapperne, som gaa ned fra Davids Stad.
16 Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
Efter ham istandsatte Nehemia, Asbuks Søn, Øversten for den halve Del af Bethzurs Kreds, et Stykke, indtil tværs over for Davids Grave og indtil den Dam, som var anlagt, og indtil de vældiges Hus.
17 Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
Efter ham istandsatte af Leviterne, Rehum, Banis Søn, et Stykke; ved Siden af ham istandsatte Hasabia, Øversten for den halve Del af Kej-Iks Kreds, et Stykke for sin Kreds.
18 Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
Efter ham istandsatte af deres Brødre Bavaj, Henadads Søn, et Stykke; han var Øverste for den anden halve Del af Kejlas Kreds.
19 Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
Og ved Siden af ham istandsatte Eser, Jesuas Søn, den Øverste i Mizpa, en anden Strækning tværs over for, hvor man gaar op til Rustkammeret ved Hjørnet.
20 Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
Efter ham istandsatte Baruk, Sabbajs Søn, med Iver en anden Strækning, fra Hjørnet indtil Ypperstepræsten Eliasibs Hus's Dør.
21 Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
Efter ham istandsatte Meremothj en Søn af Uria, Hakkoz's Søn, en anden Strækning, fra Eliasibs Hus's Dør og indtil Enden af Eliasibs Hus.
22 Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
Og efter ham istandsatte Præsterne, Mændene fra Sletten, et Stykke.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
Efter dem istandsatte Benjamin og Hasub et Stykke tværs over for deres Hus; efter ham istandsatte Asaria, en Søn af Maeseja, Ananias Søn, et Stykke ved sit Hus.
24 Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
Efter ham istandsatte Bennuj, Henadads Søn, en anden Strækning, fra Asarias Hus indtil Krogen og indtil Hjørnet.
25 Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
Palal, Ussajs Søn, byggede tværs over for Krogen og Taarnet, som springer frem fra Kongens høje Hus, og som er ved Vagtens Forgaard; efter ham byggede Pedaja, Pareos's Søn.
26 na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
— Og de livegne boede i Ofel indtil tværs over for Vandporten imod Østen og til det Taarn, som springer frem. —
27 Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
Efter ham istandsatte de af Thekoa en anden Strækning tværs over for det store fremspringende Taarn og indtil Ofels Mur.
28 Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
Fra Hesteporten istandsatte Præsterne et Stykke, hver tværs over for sit Hus.
29 Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
Efter dem istandsatte Zadok, Immers Søn, et Stykke, tværs over for sit Hus; efter ham istandsatte Semaja, Sekanjas Søn, som tog Vare paa Østerporten, et Stykke.
30 Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
Efter ham istandsatte Hanania, Selemias Søn, og Hanun, Zalafs sjette Søn, en anden Strækning; efter dem istandsatte Mesullam, Berekias Søn, et Stykke, tværs over for sit Kammer.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
Efter ham istandsatte Malkia, Guldsmedens Søn, et Stykke indtil de livegnes og Kræmmernes Hus, tværs over for Befalingsmandsporten og indtil Opgangen ved Hjørnet.
32 Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.
Og imellem Opgangen ved Hjørnet og Faareporten istandsatte Guldsmedene og Kræmmerne et Stykke.