< Nehemia 3 >

1 Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
Тогава първосвещеникът Елиасив и братята му свещениците станаха та съградиха овчата порта; те я осветиха и поставиха вратите й, дори до кулата Мея я осветиха, до кулата Ананеил.
2 Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
И до него градяха Ерихонските мъже. И до тях градеше Закхур, Имриевият син.
3 Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
А рибната порта съградиха Сенаевите синове, които, като положиха гредите й, поставиха и вратите й, ключалките й и лостовете й.
4 Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
До тях поправяше Меримот, син на Урия, Акосовият син. До него поправяше Месулам, син на Варахия, Месизавеиловият син. До него поправяше Садок, Ваанаевият син.
5 Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
И до него поправяха текойците; но големците им не се впрегнаха в делото на своя Господ.
6 Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
И старата порта поправиха Иодай, Фасеевият син и Месулам, Весодиевият син, който, като положиха гредите й, поставиха и вратите й, ключалките и лостовете й.
7 Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
До тях гаваонецът Мелатия и меронотецът Ядон, мъже от Гаваон и от Масфа, поправяше до седалището на областния управител отсам реката.
8 Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
До тях поправяше Озиил, Арахиевият син, един от златарите. До него поправяше Анания, един от аптекарите; и те укрепиха Ерусалим до широката стена.
9 Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
До него поправяше Рафаия, Оровият син, началник на половината от Ерусалимския окръг.
10 Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
До тях поправяше, срещу къщата си, Едаия, Арумафовият син. До него поправяше Хатус, Асаваниевият син.
11 Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
А Мелхия, Харимовият син, и Асув, Фаат-моавовият син, поправяха друга част и кулата на пещите.
12 Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
И до тях поправяше, заедно с дъщерите си, Селум, Алоисовият син, началник на половината от Ерусалимския окръг
13 Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
Портата на долината поправиха Анун и жителите на Заноя, които, като я съградиха, поставиха и вратите й, ключалките й и лостовете й; поправиха и хиляда лакти от стената до портата на бунището.
14 Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
А портата на бунището поправи Мелхия, Рихавовият син, началник на Вет-акаремския окръг; и той, като я съгради, постави и вратите й, ключалките й и лостовете й.
15 Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
А портата на извора поправи Селун, Холозеевият син, началник на Масафския окръг, който като я съгради и покри, постави и вратите й, ключалките й и лостовете й; поправи и стената на силоамския водоем при царската градина, дори до стъпалата, които слизат от Давидовия град.
16 Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
След него поправяше Неемия Азвуковият син, началник на половината от Вет-сурския окръг, до мястото срещу Давидовите гробища, и до направения водоем, и до къщата на силните мъже.
17 Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
След него поправяха левитите начело с Реума, Ваниевият син. До него поправяше Асавия, началник на половината от Кеилския окръг, за своя окръг.
18 Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
След него поправяха братята им, начело с Вавая, Инададовият син, началник на другата половина от Кеилския окръг.
19 Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
До него, Есер, Исусовият син, началник на Масфа, поправяше друга част, срещу нагорнището към оръжейницата при ъгъла на стената.
20 Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
След него Варух, Заваевият син, поправяше ревностно друга част, от ъгъла до вратата на къщата на първосвещеник Елиасива.
21 Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
След него, Меримот, син на Урия, Акосовия син, поправяше друга част, от вратата на Елиасивовата къща.
22 Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
След него поправяха свещениците, които живееха в тая околност.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
След тях поправяха Вениамин и Асув срещу къщата си. След тях поправяше поправяше Азария, син на Маасия, Ананиевият син, при къщата си.
24 Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
След него, Вануй, Инададовият син, поправяше друга част, от къщата на Азария до къта, дори до ъгъла на стената.
25 Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
Фалал Узаевият син поправяше срещу ъгъла и кулата, която се издава от горната царска къща, която бе при двора на стражата; и след него поправяше Фадаия, Фаросовият син.
26 na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
(А нетинимите живееха в Офил до мястото срещу портата на водата на изток, и до издадената кула).
27 Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
След него текойците поправяха друга част срещу голямата издадена кула и до стената на Офил.
28 Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
Над конската порта поправяха свещениците, всеки срещу къщата си.
29 Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
След тях поправяше Садок, Емировият син, срещу къщата си. След него поправяше вратарят на източната порта Семаия, Сеханиевият син.
30 Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
След него, Анания, Селемиевият син и Анун, шестият син на Салафа, поправяха друга част. След тях поправяше Масулам, Варахиевият син, срещу стаята си.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
След него поправяше Мелхия, син на златаря, до къщата на нетинимите и на търговците, срещу вратата на Мифкада и до нагорнището при ъгъла.
32 Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.
А между нагорнището, при ъгъла и овчата порта, поправяха златарите и търговците.

< Nehemia 3 >