< Nehemia 13 >
1 Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
Na ta dan so brali Mojzesovo knjigo v občinstvu ljudstva in v njej je bilo najdeno zapisano, da naj Amónec in Moábec na veke ne bi prišla v Božjo skupnost,
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
ker niso srečali Izraelovih otrok s kruhom in vodo, temveč so zoper njih najeli Bileáma, da bi jih preklel. Vendar je naš Bog prekletstvo obrnil na blagoslov.
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
Pripetilo se je torej, ko so slišali postavo, da so se od Izraela ločile vse mešane množice.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
Pred tem je bil duhovnik Eljašíb, ki je imel nadzor nad sobo hiše našega Boga, zbližan k Tobiju
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
in zanj pripravil veliko sobo, kjer so vnaprej položili jedilne daritve, kadilo, posode, desetine od žita, novega vina in olja, kar je bilo zapovedano, da naj bo dano Lévijevcem, pevcem in vratarjem ter darove duhovnikom.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
Toda v vsem tem času nisem bil v Jeruzalemu, kajti v dvaintridesetem letu babilonskega kralja Artakserksa sem prišel h kralju in po določenih dneh sem od kralja prejel dovoljenje za odhod
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
in prišel sem v Jeruzalem in razumel zlo, ki ga je Eljašíb storil Tobiju, s tem, da mu je pripravil sobo na dvorih Božje hiše.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
To me je boleče užalostilo, zato sem iz sobe vrgel ven vse Tobijeve gospodinjske stvari.
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
Potem sem zapovedal in očistili so sobe. Tja sem ponovno prinesel posode iz Božje hiše, z jedilno daritvijo in kadilom.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
Zaznal sem, da jim niso bili dani deleži Lévijevcev, kajti Lévijevci in pevci, ki so opravljali delo, so pobegnili vsak k svojemu polju.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
Potem sem se pričkal s poveljniki in rekel: »Zakaj je Božja hiša zapuščena?« Zbral sem jih skupaj in jih postavil na njihov kraj.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
Potem je ves Juda prinesel desetino od žita, novega vina in olja v zakladnice.
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
Postavil sem zakladnike nad zakladnicami: duhovnika Šelemjája, pisarja Cadóka in izmed Lévijevcev Pedajá. Poleg njih je bil Hanán, sin Zahúrja, sinú Matanjá, kajti bili so šteti zveste in njihova služba je bila, da razdeljujejo svojim bratom.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
»Spomni se me, oh moj Bog, glede tega in ne izbriši mojih dobrih dejanj, ki sem jih storil za hišo svojega Boga in za njene službe.«
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
V tistih dneh sem na šabat videl v Judu nekatere tlačiti vinske stiskalnice, prinašati snope in natovarjati osle kakor tudi vino, grozdje, fige in vse vrste bremen, ki so jih na šabatni dan prinesli v Jeruzalem. Pričeval sem zoper njih na dan, na katerega so prodajali živež.
16 Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
Tam notri so prebivali tudi možje iz Tira, ki so prinašali ribe in vse vrste blaga in na šabatni dan prodajali Judovim otrokom in v Jeruzalemu.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
Potem sem se pričkal z Judovimi plemiči in jim rekel: »Kakšno zlo je to, ki ga delate in oskrunjate šabatni dan?
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
Mar niso tako počeli vaši očetje in ali ni naš Bog privedel vsega tega zla nad nas in nad to mesto? Vendar nad Izrael prinašate več besa z oskrunitvijo šabata.«
19 Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
Pripetilo se je, ko so jeruzalemska velika vrata pred šabat pričenjala temneti, da sem zapovedal, naj se velika vrata zapro in jih zadolžil, da naj ne bodo odprta, dokler ne mine šabat in nekatere izmed svojih služabnikov sem postavil pri velikih vratih, da na šabatni dan ne bi bilo noter privedeno nobeno breme.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
Tako so trgovci in prodajalci vseh vrst blaga enkrat ali dvakrat prenočili zunaj Jeruzalema.
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
Potem sem pričeval zoper njih in jim rekel: »Zakaj prenočujete okoli obzidja? Če boste ponovno storili tako, bom svoje roke položil na vas.« Od tistega časa naprej niso več prihajali na šabat.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
Lévijevcem sem zapovedal, da naj se očistijo in da naj pridejo in varujejo velika vrata, da posvetijo šabatni dan. »Spomni se me, oh moj Bog, tudi glede tega in prizanesi mi glede na veličino svojega usmiljenja.«
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
V tistih dneh sem videl tudi Jude, ki so poročili žene iz Ašdóda, iz Amóna in iz Moába
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
in njihovi otroci so govorili pol v ašdódskem jeziku in niso mogli govoriti judovskega jezika, temveč glede na jezik vsakega ljudstva.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
Pričkal sem se z njimi in jih preklel in udaril nekatere izmed njih, izpulil njihove lase in jih primoral, da so prisegli pri Bogu, rekoč: »Svojih hčera ne boste dajali njihovim sinovom niti ne boste jemali njihovih hčera za svoje sinove ali zase.«
26 Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
Mar ni Salomon, Izraelov kralj, grešil s temi stvarmi? Pa vendar med mnogimi narodi ni bilo nobenega kralja, podobnega njemu, ki je bil ljubljen od svojega Boga in ga je Bog postavil [za] kralja nad vsem Izraelom. Kljub temu so celo njemu tuje žene povzročile, da je grešil.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
Mar naj potem prisluhnemo vam, da bi delali vso to veliko zlo, da grešimo zoper svojega Boga v poročanju tujih žena?
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
Eden izmed sinov Jojadája, sin vélikega duhovnika Eljašíba, je bil zet Horónca Sanbaláta, zato sem ga pregnal od sebe.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
»Spomni se jih, oh moj Bog, ker so omadeževali duhovništvo in zavezo duhovništva in Lévijevcev.«
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
Tako sem jih očistil vseh tujcev in določil straže duhovnikov in Lévijevcev, vsakega pri svojem poslu
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
in za dar lesa, ob določenih časih in za prve sadove. »Spominjaj se me, oh moj Bog, za vselej.«