< Nehemia 13 >

1 Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
У то време чита се књига Мојсијева народу, и у њој се нађе написано да не улази Амонац ни Моавац у сабор Божји до века;
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
Јер не сретоше синове израиљеве с хлебом и водом, него најмише на њих Валама да их прокуне, али Бог наш обрати ону клетву у благослов.
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
А кад чуше тај закон одлучише од Израиља све туђинце.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
А пре тога Елијасив свештеник, који беше над клетима дома Бога нашег, опријатељи се с Товијом,
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
И начини му велику клет, где се пре остављаху дари и кад и судови и десетак од жита, вина и уља, одређени Левитима и певачима и вратарима, и приноси за свештенике.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
А кад то све биваше, не бејах у Јерусалиму, јер тридесет друге године Артаксеркса, цара вавилонског, вратих се к цару, и после неколико година измолих се опет у цара.
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
И кад дођох у Јерусалим, видех зло што учини Елијасив ради Товије начинивши му клет у трему дома Божјег.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
И би ми врло мрско, те избацих све покућство Товијино напоље из клети.
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
И заповедих, те очистише клети; и унесох у њих опет посуђе дома Божјег, даре и кад.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
Потом дознах да се Левитима нису давали делови, те су се разбегли сваки на своју њиву и Левити и певачи, који рађаху посао.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
И укорих старешине и рекох: Зашто је остављен дом Божји? И сабрах их опет и поставих на њихово место.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
И сви Јудејци доносише десетке од жита и вина и уља у спреме.
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
И поставих настојнике над спремама, Селмију свештеника и Садока књижевника, и између Левита Федају, и уз њих Анана, сина Захура сина Матанијиног, јер се за верне држаху; и беше им посао делити браћи својој.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
Помени ме, Боже мој, зато, и немој избрисати добра мојих која учиних дому Бога свог и служби његовој.
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
У то време видех у Јудеји где газе у кацама у суботу и носе снопове натоваривши на магарце, и вино, грожђе и смокве и свакојаке товаре, и носе у Јерусалим у суботу, и прекорих их онај дан кад продаваху житак.
16 Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
И Тирци који живљаху у Јерусалиму доношаху рибу и свакојаки трг и продаваху у суботу синовима Јудиним у Јерусалиму.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
Зато прекорих главаре јудејске и рекох им: Какво је то зло што чините те скврните суботу?
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
Нису ли тако чинили оци ваши, те Бог наш пусти на нас и на овај град све ово зло? И ви још умножавате гнев на Израиља скврнећи суботу.
19 Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
И кад дође сен на врата јерусалимска уочи суботе, заповедих те затворише врата, и заповедих да их не отварају до после суботе; и поставих неколико својих момака на вратима да се не уноси никакав товар у суботу.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
И преноћише трговци и који продаваху свакојаки трг иза Јерусалима једном и другом.
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
И опоменух их и рекох им: Зашто ноћујете око зида? Ако још једном то учините, уложићу на вас. Од тада не долазише у суботу.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
А Левитима заповедих да се очисте и да дођу и чувају врата да буде свет дан суботни. И за ово помени ме, Боже мој, и опрости ми по великој милости својој.
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
Још видех у то време Јудејце који се беху оженили Азоћанкама, Амонкама и Моавкама.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
И синови њихови говораху пола азотски, и не умеху говорити јудејски него језиком и једног и другог народа.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
Зато их карах и псовах, и неке између њих бих и чупах, и заклех их Богом да не дају кћери своје синовима њиховим нити да узимају кћери њихове за синове своје или за себе.
26 Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
Није ли тим згрешио Соломун, цар Израиљев, ако и не беше у многим народима цара њему равног и мио беше Богу свом и Бог га беше поставио царем над свим Израиљем? Па опет га навратише на грех жене туђинке.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
А вама ли ћемо допустити да чините то све велико зло и грешите Богу нашем узимајући жене туђинке?
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
И од синова Јојаде, сина Елијасива поглавара свештеничког, један беше зет Санавалату Ороњанину, ког отерах од себе.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
Помени их, Боже мој, што оскрвнише свештенство и завет свештенички и левитски.
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
И тако их очистих од свих туђинаца, и опет поставих редове свештеничке и левитске, сваког на посао његов,
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
И да се доносе дрва за жртве на рокове, и првине. Помени ме, Боже мој, на добро.

< Nehemia 13 >