< Nehemia 13 >

1 Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
Onegoż dnia czytano w księgach Mojżeszowych, tak, iż lud słyszał. I znaleziono w nich napisane, że nie miał wchodzić Ammonitczyk i Moabczyk do zgromadzenia Bożego, aż na wieki;
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
Przeto, iż nie zaszli synom Izraelskim z chlebem i z wodą; owszem najęli przeciwko nim Balaama, aby ich przeklinał; ale obrócił Bóg nasz ono przeklęstwo w błogosławieństwo.
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
A gdy usłyszeli zakon, odłączyli wszystek lud pospolity od Izraela.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
Ale się przedtem Elijasyb kapłan, przełożony nad skarbnicą domu Boga naszego, spowinowacił z Tobijaszem;
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
I zbudował mu gmach wielki, kędy przedtem odkładano dary, kadzidło, i naczynia, i dziesięciny zboża, moszczu, i oliwy świeżej, opatrzenie Lewitom, i śpiewakom, i odźwiernym, także ofiary podnoszone kapłańskie.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
Ale przy tem wszystkiem nie byłem w Jeruzalemie; albowiem roku trzydziestego i wtórego Artakserksesa, króla Babilońskiego, przyszedłem do króla, a po wyjściu kilku lat uprosiłem się u króla.
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
A gdym przyszedł do Jeruzalemu, wyrozumiałem to złe, które uczynił Elijasyb kwoli Tobijaszowi, iż mu zbudował gmach w sieniach domu Bożego.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
Co mi się bardzo nie podobało: przetoż wyrzuciłem wszystkie naczynia domu Tobijaszowego precz z onegoż gmachu;
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
I rozkazałem oczyścić one gmachy, i wniosłem tam zaś nacznia domu Bożego, dary i kadzidło.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
Nadtom się dowiedział, że działy Lewitom nie były oddawane, a iż się Lewitowie i śpiewacy, którzy pilnowali pracy, rozbiegli, każdy do roli swojej.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
Przetoż zgromiłem przełożonych, mówiąc: Przeczże opuszczamy dom Boży? A tak zebrawszy ich, postawiłem ich na miejscach ich.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
A wszystek Juda przynosili dziesięciny zboża, i moszczu, i świeżej oliwy do skarbu.
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
I postanowiłem podskarbich nad skarbmi: Selemijasza kapłana, i Sadoka nauczonego w Piśmie, i Fadajasza z Lewitów, a przy nich Hanana, syna Zachurowego, syna Matanijaszowego, bo ich za wiernych miano; a ich powinność była, działy rozdawać braciom swym.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
Wspomnij na mię o Boże mój! dla tego, a nie wymazuj dobroczynności moich, którem czynił przy domu Boga mego, i przy obrzędach jego.
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
W oneż dni widziałem w Judzie tłoczących prasy w sabat, i noszących snopy, które kładli na osły, także i winne grona, i figi, i wszelki ciężar, a przynoszących do Jeruzalemu w dzień sabatu, i zgromiłem ich onegoż dnia, którego sprzedawali żywność.
16 Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
Także Tyryjczycy, którzy mieszkali w niem, przynosili ryby, i rozmaite towary, a sprzedawali w sabat synom Judy, i w Jeruzalemie.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
Przetożem zgromił przełożonych w Judzie, mówiąc do nich: Cóż to jest za nieprawość, której się dopuszczacie, gwałcąc dzień sabatu?
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
Izali nie toż czynili ojcowie wasi, przez co Bóg nasz przywiódł na nas to wszystko złe, i na to miasto? A wy przyczyniacie gniewu na Izraela, gwałcąc sabat.
19 Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
A gdy okrył cień bramy Jeruzalemskie przed sabatem, rozkazałem zamknąć wrota, i nie kazałem ich otwierać, aż po sabacie; a niektórych z sług moich postawiłem w bramach, żeby nie wnoszono żadnych brzemion w dzień sabatu.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
Przetoż zostali przez noc kupcy, i sprzedawający towary rozmaite przed miastem Jeruzalemskiem, raz i drugi.
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
Przeciwko którym oświadczyłem się, i rzekłem do nich: Przecz wy zostawacie przez noc za murem? Uczynicieli to więcej, ściągnę rękę na was. A tak od onego czasu nie przychodzili w sabat.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
I rozkazałem Lewitom, aby się oczyścili, a przyszedłszy strzegli bram, i święcili dzień sabatu. I dlatego wspomnij na mię, o Boże mój! a bądź mi miłościw według obfitości miłosierdzia twego.
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
W tychże dniach ujrzałem też Żydów, którzy sobie pojęli żony Azotyckie, Ammonickie, Moabskie.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
A synowie ich na poły mówili po azotycku, nie umiejąc mówić po żydowsku, ale według języka swego narodu.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
Przetożem ich zgromił, i przeklinałem ich, i biłem niektórych z nich, a rwałem ich za włosy, i poprzysiągłem ich przez Boga, aby nie dawali córek swoich synom ich, ani brali córek ich synom swym i sobie.
26 Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
Izaliż nie przez to zgrzeszył Salomon, król Izraelski? choć między wieloma narodami nie było króla jemu podobnego, który był miły Bogu swemu, tak, że go Bóg postanowił królem, nad wszystkim Izraelem, przecież i tego przywiodły niewiasty cudzoziemskie do grzechu.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
A wam izali pozwolimy, żebyście się dopuszczali tej wielkiej złości, a występowali przeciwko Bogu naszemu pojmując żony cudzoziemskie?
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
Lecz jeden z synów Jojady, syna Elijasyba, kapłana najwyższego, był zięciem Sanballata Horończyka, i wygnałem go od siebie.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
Wspomnijże na to, o Boże mój! przeciw tym, którzy plugawią kapłaństwo, i umowę kapłańską i Lewitską.
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
Przetożem ich oczyścił od wszelkiego cudzoziemca, i postanowiłem porządki kapłanom i Lewitom, każdemu w pracy jego,
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
I ku noszeniu drew do ofiar, czasów postanowionych, także i pierwocin. Wspomnijże na mię, Boże mój! ku dobremu.

< Nehemia 13 >