< Nehemia 13 >
1 Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
En ce jour-là, on lut à haute voix au peuple le livre de Moïse, et on y trouva écrit: Que les Ammonites et les Moabites ne devaient jamais entrer dans l'Église de Dieu.
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
Parce qu'ils n'étaient point venus au-devant d'Israël avec du pain et de l'eau, et qu'ils avaient salarié Balaam pour le maudire; mais, notre Dieu changea la malédiction en bénédiction.
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
Et lorsqu'ils eurent ouï la loi, tous ceux qui s'étaient mêlés à Israël en furent séparés.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
Or, avant cela, Eliasib, le prêtre, très-proche allié de Tobias, demeurait dans le trésor du temple de notre Dieu.
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
Et il s'était fait faire un vaste magasin dans le lieu où l'on déposait jadis les offrandes, l'encens, les vases, la dîme du blé, du vin et de l'huile, ce qui était dû aux lévites, aux chantres et aux portiers, et les prémices destinées aux prêtres.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
Et, en ce temps-là, je n'étais pas à Jérusalem. Car, dans la trente- deuxième année du règne d'Arthasastha, roi de Babylone, j'étais allé auprès du roi. Et, un certain nombre de jours étant accompli, je demandai au roi la permission de partir.
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
Et je revins à Jérusalem, et je reconnus le mal qu'avait fait Eliasib avec Tobias en lui faisant un magasin dans le parvis du temple de Dieu.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
Et cela me parut très-mal; et je jetai hors du magasin tous les meubles de la maison de Tobias.
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
Et je parlai, et on purifia le magasin, et j'y fis replacer les vases du temple, les offrandes et l'encens.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
Et je reconnus qu'on n'avait plus donné la part des lévites, de sorte que les lévites et les chantres faisant œuvre au temple s'étaient enfuis chacun en sa terre.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
Et je fis des reproches aux officiers, et je leur dis: D'où vient que le temple du Seigneur est abandonné? Puis, je rassemblai les lévites et les Chantres, et je les rétablis dans leurs fonctions.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
Alors, tout Juda apporta dans les trésors la dîme du froment; de l'huile et du vin,
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
Entre les mains de Sélémias le prêtre, de Sadoc le scribe, et de Phadaïa, l'un des lévites. Et ils avaient auprès d'eux Anan, fils de Zacchur, fils de Matthanias; car ils étaient réputés fidèles, et ils furent chargés de faire les distributions à leurs frères.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
Souvenez-vous de moi, ô mon Dieu, à cause de cela; que mes bonnes œuvres dans le temple du Seigneur Dieu ne soient point effacées.
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
En ces jours-là, je vis que dans Juda quelques-uns pressuraient le vin le jour du sabbat; je vis que d'autres transportaient des gerbes, que d'autres encore chargeaient leurs ânes de vin, de grappes, de figues, de toutes sortes de fardeaux, et qu'ils les conduisaient à Jérusalem le jour du sabbat. Et je les avertis des jours où ils pouvaient trafiquer.
16 Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
Et des gens s'étaient établis à Jérusalem, apportant du poisson, vendant toutes sortes de marchandises aux Juifs, le jour du sabbat.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
Et je réprimandai les fils de Juda de condition libre, et je leur dis: Quelle est cette mauvaise action que vous faites, en profanant le jour du sabbat?
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
N'est-ce point là ce que faisaient vos pères? n'est-ce point la cause de tous les malheurs dont notre Dieu les à frappés, eux et notre ville? Et vous, n'attirerez-vous pas un surcroît de colère sur Israël en profanant le sabbat?
19 Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
Or, quand les portes de Jérusalem furent rétablie, la veille d'un sabbat, je parlai, et on ferma les portes; je parlai, et on ne les ouvrit qu'après le sabbat, et je mis de mes serviteurs à chaque porte pour qu'on ne pût introduire des fardeaux le jour du sabbat.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
Et tous les marchands passèrent la nuit en plein air, et ils vendirent une ou deux fois hors de Jérusalem.
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
Et je les avertis, et je leur dis: Pourquoi passez-vous la nuit devant les remparts? Si vous recommencez, j'étendrai la main sur vous. Depuis lors, ils ne vinrent plus le jour du sabbat.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
Et je dis aux lévites qui s'étaient purifiés, et qui étaient venus garder les portes, de sanctifier le jour du sabbat: à cause de cela, souvenez-vous de moi, mon Dieu, et épargnez-moi, selon la plénitude de votre miséricorde.
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
Or, en ces jours-là, je vis que des Juifs avaient épousé des femmes d'Azot, et des Ammonites et des Moabites.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
Et leurs fils parlaient à demi la langue d'Azot, et ils ne savaient point parler juif.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
Et je les réprimandai, et je les maudis, et j'en frappai quelques-uns, et je leur rasai la tête, et je leur fis jurer devant Dieu de ne point donner leurs filles aux fils des étrangers, et de ne point faire épouser par leurs fils des filles étrangères, disant:
26 Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
N'est-ce pas là le péché de Salomon, roi d'Israël? Il n'y avait point son pareil parmi les rois des nations: il aimait Dieu, Dieu lui avait donné le royaume entier d'Israël, et les femmes étrangères le pervertirent.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
Que nous n'apprenions plus que vous faites ce péché; que vous violez l'alliance avec notre Dieu; que vous épousez des femmes étrangères.
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
Or, l'un des fils de Joad, le grand prêtre Elisab, était gendre de Sanaballat l'Horonite; je le chassai loin de moi.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
Souvenez-vous d'eux, ô Seigneur, à cause de la violation du sacerdoce, et de votre alliance, touchant les prêtres et les lévites.
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
Et je les purifiai de leur contact avec des étrangères, et je réglai les services journaliers des prêtres et des lévites,
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
Et l'offrande du bois des holocaustes au temps prescrit, lorsque l'on taille la vigne. Souvenez-vous de moi, ô mon Dieu, dans votre mansuétude.