< Nehemia 13 >

1 Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
On the day that it was read aloud in [the] scroll of Moses in [the] ears of the people and it was found written in it that not he will come an Ammonite and a Moabite in [the] assembly of God until perpetuity.
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
For not they had met [the] people of Israel with food and with water and he had hired on it Balaam to curse it and he turned God our the curse into blessing.
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
And it was when heard they the law and they separated every person of mixed ancestry from Israel.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
And before from this Eliashib the priest [was] appointed over [the] store-room of [the] house of God our [one] near to Tobiah.
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
And he made for him a room large and there people were before putting the grain offering the frankincense and the utensils and [the] tithe of the grain the new wine and the fresh oil [the] commandment of the Levites and the singers and the gatekeepers and [the] contribution of the priests.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
And in all this not I was in Jerusalem for in year thirty and two of Artaxerxes [the] king of Babylon I had gone to the king and to [the] end of days I requested leave of absence from the king.
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
And I came to Jerusalem and I perceived! the evil thing which he had done Eliashib for Tobiah by making for him a room in [the] courtyards of [the] house of God.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
And it was displeasing to me exceedingly and I threw! all [the] articles of [the] household of Tobiah the outside from the room.
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
And I said! and people purified the store-rooms and I brought back! there [the] utensils of [the] house of God the grain offering and the frankincense.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
And I perceived! that [the] portions of the Levites not it had been given and they had fled each one to own field his the Levites and the singers [who] did the work.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
And I contended! with the officials and I said! why? has it been neglected [the] house of God and I assembled them and I made stand them at place their.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
And all Judah they brought [the] tithe of the grain and the new wine and the fresh oil to the storerooms.
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
And I appointed as treasurers! over [the] storerooms Shelemiah the priest and Zadok the scribe and Pedaiah one of the Levites and [was] on hand their Hanan [the] son of Zaccur [the] son of Mattaniah for reliable they were thought and [was] on them to distribute to brothers their.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
Remember! to me O God my on this and may not you wipe out loyalti my which I have done in [the] house of God my and in services its.
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
In the days those I saw in Judah - [some who] trod winepresses - on the sabbath and [some who] brought heaps of grain and [some who] loaded [them] on donkeys and also wine grapes and figs and every load and [some who] brought [them] Jerusalem on [the] day of the sabbath and I protested on [the] day sold they food.
16 Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
And the Tyrians [who] they dwelt in it [were] bringing fish and every merchandise and [were] selling [it] on the sabbath to [the] people of Judah and in Jerusalem.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
And I contended! with [the] nobles of Judah and I said! to them what? [is] the thing evil this which you [are] doing and [are] profaning [the] day of the sabbath.
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
¿ Not thus did they do ancestors your and he brought God our on us all the trouble this and on the city this and you [are] increasing anger toward Israel by profaning the sabbath.
19 Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
And it was just when they became dark [the] gates of Jerusalem before the sabbath and I said! and they were closed the doors and I said! that not people will open them until after the sabbath and some of servants my I stationed at the gates not it will come a load on [the] day of the sabbath.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
And they passed [the] night the traders and [the] sellers of every merchandise from [the] outside of Jerusalem a time and two [times].
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
And I warned! them and I said! to them why? [are] you passing [the] night before the wall if you will do [it] again a hand I will stretch out on you from the time that not they came on the sabbath.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
And I said! to the Levites that they will be purifying themselves and coming guarding the gates to keep holy [the] day of the sabbath also this remember! to me O God my and have mercy! on me according to [the] greatness of covenant loyalty your.
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
Also - in the days those I saw the Jews [who] they had married women (Ashdodite Ammonite *Q(k)*) Moabite.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
And children their half [were] speaking Ashdodite and not they [were] knowing to speak [in] Judean and according to [the] language of people and people.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
And I contended with them and I cursed them and I struck some of them men and I pulled out beard their and I made take an oath them by God if you will give daughters your to sons their and if you will take any of daughters their for sons your and for yourselves.
26 Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
¿ Not on these did he sin Solomon [the] king of Israel and among the nations many not he was a king like him and loved by God his he was and he made him God king over all Israel also him they caused to sin the wives foreign.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
And to you ¿ is it heard to do all the evil great this to act unfaithfully against God our by marrying wives foreign.
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
And one of [the] sons of Joiada [the] son of Eliashib the priest great [was] a son-in-law of Sanballat the Horonite and I drove away him from with me.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
Remember! to them O God my on [the] defilement of the priesthood and [the] covenant of the priesthood and the Levites.
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
And I purified them from all foreignness and I assigned! duties to the priests and to the Levites each one in own work his.
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
And for [the] offering of the wood at times appointed and for the first-fruits remember! to me O God my for good.

< Nehemia 13 >