< Nehemia 12 >
1 Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
Torej to so duhovniki in Lévijevci, ki so prišli gor z Zerubabélom, Šealtiélovim sinom in Ješúom: Serajá, Jeremija, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amarjá, Malúh, Hatúš,
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
Šehanjá, Rehúm, Meremót,
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
Mijamín, Maadjá, Bilgá,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Šemajá, Jojaríb, Jedajája,
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
Salú, Amók, Hilkijá, Jedajája. Ti so bili vodje duhovnikov in njihovih bratov v dneh Ješúa.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
Poleg tega Lévijevci: Ješúa, Binúj, Kadmiél, Šerebjá, Juda in Matanjá, ki je bil nad zahvaljevanjem, on in njegovi bratje.
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
Tudi Bakbukjá in Uní, njihova brata, sta bila njim nasproti na stražah.
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
Ješúa je zaplodil Jojakíma, Jojakím je zaplodil tudi Eljašíba, Eljašíb je zaplodil Jojadá,
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
Jojadá je zaplodil Jonatana in Jonatan je zaplodil Jadúa.
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
V dneh Jojakíma so bili duhovniki, vodja očetov: od Serajáma Merajá, od Jeremija Hananjá,
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
od Ezra Mešulám, od Amarjá Johanán,
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
od Melicuja Jonatan, od Šebanjá Jožef,
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
od Haríma Adná, od Merajóta Helkáj,
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
od Idója Zaharija, od Ginetóna Mešulám,
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
od Abíja Zihrí, od Minjamína, od Moadjája Piltáj,
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
od Bilgája Šamúa, od Šemajája Jehonatan,
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
in od Jojaríba Matenáj, od Jedajája Uzí,
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
od Salája Kaláj, od Amóka Eber,
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
od Hilkijá Hašabjá, od Jedajája, Netanél.
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
Lévijevci v dneh Eljašíba, Jojadája, Johanána in Jadúa so bili zabeleženi vodje očetov, tudi duhovniki, do kraljevanja Perzijca Dareja.
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
Lévijevi sinovi, vodje očetov so bili zapisani v kroniški knjigi, celo do dni Eljašíbovega sina Johanána.
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
Vodje Lévijevcev: Hašabjá, Šerebjá in Kadmiélov sin Ješúa z njihovimi brati nasproti njih, da hvalijo in da se zahvaljujejo, glede na zapoved Davida, Božjega moža, straža nasproti straži.
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
Matanjá in Bakbukjá, Obadjá, Mešulám, Talmón, Akúb so bili vratarji, ki so varovali stražo pri pragovih velikih vrat.
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
Ti so bili v dneh Jojakíma, sina Ješúa, sinú Jocadákovega in v dneh voditelja Nehemija in preroka Ezra, pisarja.
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
Ob posvetitvi jeruzalemskega obzidja so iskali Lévijevce iz vseh njihovih krajev, da jih privedejo v Jeruzalem, da ohranjajo posvetitev z veseljem, tako z zahvaljevanjem kakor s petjem, s cimbalami, plunkami in harfami.
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
Sinovi pevcev so se zbrali skupaj, tako iz ravne dežele okoli Jeruzalema kakor iz vasi Netófčanov,
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
tudi iz hiše Gilgála in iz gebskih in azmávetskih polj, kajti pevcem so zgradili vasi okoli Jeruzalema.
30 Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
Duhovniki in Lévijevci so očistili sebe, očistili ljudstvo in velika vrata ter obzidje.
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
Potem sem na obzidje privedel Judove prince in določil dve veliki skupini tistih, ki so dajali zahvalo, od katerih je ena odšla na desno roko, po obzidju, h Gnojnim velikim vratom.
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
Za njimi je odšel Hošajá in polovica Judovih princev
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
Azarjá, Ezra, Mešulám,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
Juda, Benjamin, Šemajá in Jeremija.
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
Nekateri izmed duhovnikovih sinov s trobentami, namreč Zeharjá, sin Jonatana, sinú Šemajá, sinú Matanjá, sinú Mihajája, sinú Zahúrja, sinú Asáfa
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
in njegovi bratje: Šemajá, Azarél, Milaláj, Gilaláj, Maáj, Netanél, Juda in Hananí z glasbenimi instrumenti Davida, Božjega moža in pisar Ezra pred njimi.
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
Pri Studenčnih velikih vratih, ki so bila nasproti njim, so se po stopnicah Davidovega mesta povzpeli ob vzponu obzidja, nad Davidovo hišo, celo do Vodnih velikih vrat proti vzhodu.
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
Druga skupina izmed tistih, ki so dajali zahvalo, pa je šla nasproti njim in jaz za njimi in polovica ljudstva na zidu od onstran stolpa talilnih peči, celo do širokega zidu
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
in nad Efrájimovimi velikimi vrati, nad Starimi velikimi vrati, nad Ribjimi velikimi vrati in [mimo] stolpa Hananéla in stolpa Mea, torej do Ovčjih velikih vrat in so mirno obstali pri Jetniških velikih vratih.
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
Tako sta stali dve skupini izmed tistih, ki so dajali zahvalo v Božji hiši ter jaz in polovica vladarjev z menoj
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
in duhovniki: Eljakím, Maasejája, Minjamín, Mihajá, Eljoenáj, Zeharjá in Hananjá s trobentami
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
ter Maasejája, Šemajá, Eleazar, Uzí, Johanán, Malkijája, Elám in Ecer. Pevci so glasno peli z Jizrahjájem, njihovim nadzornikom.
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
Ta dan so darovali tudi veliko klavnih daritev in se veselili, kajti Bog jih je pripravil, da se veselijo z veliko radostjo. Tudi žene in otroci so se veselili, tako da je bilo veselje iz Jeruzalema slišati celo od daleč.
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
Ob tistem času so bili nekateri določeni nad sobe za zaklade, za daritve, za prve sadove in za desetine, da zberejo vanje iz mestnih polj deleže od postave za duhovnike in Lévijevce, kajti Juda se je veselil zaradi duhovnikov in Lévijevcev, ki so čakali.
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
Tako pevci kakor vratarji so varovali službo svojega Boga in službo očiščevanja, glede na zapoved Davida in njegovega sina Salomona.
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
Kajti v dneh Davida in Asáfa, so bili tam od davnine vodje pevcev s pesmimi hvaljenja in zahvaljevanja Bogu.
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.
Ves Izrael je v dneh Zerubabéla in v dneh Nehemija dal deleže pevcem in vratarjem, vsak dan njegov delež. Svete stvari pa so posvetili Lévijevcem in Lévijevci so jih posvetili Aronovim otrokom.