< Nehemia 12 >

1 Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
Et ce sont ici les sacrificateurs et les lévites qui montèrent avec Zorobabel, fils de Shealthiel, et Jéshua: Seraïa, Jérémie, Esdras,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amaria, Malluc, Hattush,
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
Shecania, Rehum, Merémoth,
4 Ido, Ginethoni, Abiya,
Iddo, Guinnethoï, Abija,
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
Mijamin, Maadia, Bilga,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Shemahia, et Joïarib, Jedahia,
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
Sallu, Amok, Hilkija, Jedahia. Ce sont là les chefs des sacrificateurs et de leurs frères, aux jours de Jéshua.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
Et les lévites: Jéshua, Binnuï, Kadmiel, Shérébia, Juda, Matthania, qui avait la direction des louanges, lui et ses frères.
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
Et Bakbukia, et Unni, leurs frères, vis-à-vis d’eux dans leurs fonctions.
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
Et Jéshua engendra Joïakim, et Joïakim engendra Éliashib, et Éliashib engendra Joïada,
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
et Joïada engendra Jonathan, et Jonathan engendra Jaddua.
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
Et aux jours de Joïakim étaient sacrificateurs, chefs des pères: de Seraïa, Meraïa; de Jérémie, Hanania;
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
d’Esdras, Meshullam; d’Amaria, Jokhanan;
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
de Meluki, Jonathan; de Shebania, Joseph;
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
de Harim, Adna; de Meraïoth, Helkaï;
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
d’Iddo, Zacharie; de Guinnethon, Meshullam;
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
d’Abija, Zicri; de Minjamin [et] Moadia, Piltaï;
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
de Bilga, Shammua; de Shemahia, Jonathan;
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
et de Joïarib, Mathnaï; de Jedahia, Uzzi;
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
de Sallaï, Kallaï; d’Amok, Éber;
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
de Hilkija, Hashabia; de Jedahia, Nethaneël.
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
Quant aux lévites, les chefs des pères furent inscrits aux jours d’Éliashib, de Joïada, et de Jokhanan et de Jaddua, et les sacrificateurs, jusqu’au règne de Darius, le Perse.
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
Les fils de Lévi, chefs des pères, furent inscrits dans le livre des chroniques, jusqu’aux jours de Jokhanan, fils d’Éliashib.
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
Et les chefs des lévites: Hashabia, Shérébia, et Jéshua, fils de Kadmiel, et leurs frères vis-à-vis d’eux, pour louer [et] pour rendre grâces selon le commandement de David, homme de Dieu, les uns en fonction à côté des autres.
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
Matthania et Bakbukia, Abdias, Meshullam, Talmon, Akkub, faisaient la garde comme portiers aux magasins des portes.
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
Ceux-ci [vivaient] aux jours de Joïakim, fils de Jéshua, fils de Jotsadak, et aux jours de Néhémie, le gouverneur, et d’Esdras, le sacrificateur, le scribe.
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
Et lors de la dédicace de la muraille de Jérusalem, on envoya chercher les lévites de tous leurs lieux [d’habitation], pour les amener à Jérusalem, pour faire la dédicace avec joie, avec des louanges et des chants, [avec] des cymbales, des luths et des harpes.
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
Et les fils des chantres s’assemblèrent, tant de la plaine [du Jourdain], des environs de Jérusalem, que des hameaux des Netophathites,
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
et de la maison de Guilgal, et des campagnes de Guéba et d’Azmaveth; car les chantres s’étaient bâti des hameaux dans les environs de Jérusalem.
30 Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
Et les sacrificateurs et les lévites se purifièrent, et ils purifièrent le peuple, et les portes, et la muraille.
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
Et je fis monter les chefs de Juda sur la muraille, et je plaçai deux grands chœurs en processions, à droite, sur le mur, vers la porte du fumier;
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
et après eux marchaient Hoshahia et la moitié des chefs de Juda,
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
et Azaria, Esdras et Meshullam,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
Juda et Benjamin, et Shemahia et Jérémie,
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
et des fils des sacrificateurs avec des trompettes: Zacharie, fils de Jonathan, fils de Shemahia, fils de Matthania, fils de Michée, fils de Zaccur, fils d’Asaph,
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
et ses frères, Shemahia, et Azareël, Milalaï, Guilalaï, Maaï, Nethaneël, Juda, et Hanani, avec des instruments de musique de David, homme de Dieu; et Esdras, le scribe, devant eux.
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
Et à la porte de la fontaine, vis-à-vis d’eux, ils montèrent les degrés de la ville de David, par la montée de la muraille, au-dessus de la maison de David, et jusqu’à la porte des eaux, vers le levant.
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
Et le second chœur marcha à l’opposé sur la muraille, et moi après lui, ainsi que la moitié du peuple, depuis la tour des fours jusqu’à la muraille large,
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
et au-dessus de la porte d’Éphraïm, et près de la porte du vieux [mur], et de la porte des poissons, et de la tour de Hananeël, et de la tour de Méa, jusqu’à la porte des brebis; et ils s’arrêtèrent à la porte de la prison.
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
Et les deux chœurs s’arrêtèrent dans la maison de Dieu, et moi, et la moitié des chefs avec moi,
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
et les sacrificateurs Éliakim, Maascéïa, Minjamin, Michée, Élioénaï, Zacharie, Hanania, avec des trompettes;
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
et Maascéïa, et Shemahia, et Éléazar, et Uzzi, et Jokhanan, et Malkija, et Élam, et Ézer. Et les chantres firent entendre [leur voix], et Jizrakhia les dirigeait.
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
Et ils offrirent ce jour-là de grands sacrifices, et se réjouirent, car Dieu les avait réjouis d’une grande joie; et les femmes aussi et les enfants se réjouirent; et la joie de Jérusalem s’entendait au loin.
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
Et des hommes furent préposés, ce jour-là, sur les chambres des trésors pour les offrandes élevées, pour les prémices, et pour les dîmes, afin d’y recueillir, des champs des villes, les portions assignées par la loi aux sacrificateurs et aux lévites; car Juda se réjouissait à cause des sacrificateurs et des lévites qui se tenaient là;
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
et, ainsi que les chantres et les portiers, ils gardaient ce que leur Dieu leur avait donné à garder, et ce qu’ils avaient à garder pour la purification, selon le commandement de David [et] de Salomon, son fils.
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
Car autrefois, aux jours de David et d’Asaph, il y avait des chefs pour diriger les chantres et les chants de louanges et les cantiques d’actions de grâces à Dieu.
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.
Et aux jours de Zorobabel, et aux jours de Néhémie, tout Israël donnait les portions des chantres et des portiers, chaque jour ce qu’il fallait, et on mettait à part pour les lévites, et les lévites mettaient à part pour les fils d’Aaron.

< Nehemia 12 >