< Nehemia 12 >
1 Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
and these [the] priest and [the] Levi which to ascend: rise with Zerubbabel son: child Shealtiel and Jeshua Seraiah Jeremiah Ezra
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amariah Malluch Hattush
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
Shecaniah Rehum Meremoth
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
Mijamin Maadiah Bilgah
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Shemaiah and Joiarib Jedaiah
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
Sallu Amok Hilkiah Jedaiah these head: leader [the] priest and brother: male-relative their in/on/with day Jeshua
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
and [the] Levi Jeshua Binnui Kadmiel Sherebiah Judah Mattaniah upon praise he/she/it and brother: male-relative his
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
and Bakbukiah (and Unni *Q(K)*) brother: male-relative their to/for before them to/for charge
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
and Jeshua to beget [obj] Joiakim and Joiakim to beget [obj] Eliashib and Eliashib [obj] Joiada
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
and Joiada to beget [obj] Jonathan and Jonathan to beget [obj] Jaddua
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
and in/on/with day Joiakim to be priest head: leader [the] father to/for Seraiah Meraiah to/for Jeremiah Hananiah
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
to/for Ezra Meshullam to/for Amariah Jehohanan
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
(to/for Mallichi *Q(K)*) Jonathan to/for Shebaniah Joseph
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
to/for Harim Adna to/for Meraioth Helkai
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
(to/for Iddo *Q(K)*) Zechariah to/for Ginnethon Meshullam
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
to/for Abijah Zichri to/for Miniamin to/for Moadiah Piltai
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
to/for Bilgah Shammua to/for Shemaiah Jehonathan
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
and to/for Joiarib Mattenai to/for Jedaiah Uzzi
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
to/for Sallai Kallai to/for Amok Eber
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
to/for Hilkiah Hashabiah to/for Jedaiah Nethanel
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
[the] Levi in/on/with day Eliashib Joiada and Johanan and Jaddua to write head: leader father and [the] priest upon royalty Darius [the] Persian
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
son: descendant/people Levi head: leader [the] father to write upon scroll: book Chronicles [the] day and till day Johanan son: child Eliashib
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
and head: leader [the] Levi Hashabiah Sherebiah and Jeshua son: child Kadmiel and brother: male-relative their to/for before them to/for to boast: praise to/for to give thanks in/on/with commandment David man [the] God custody to/for close custody
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
Mattaniah and Bakbukiah Obadiah Meshullam Talmon Akkub to keep: guard gatekeeper custody in/on/with storehouse [the] gate
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
these in/on/with day Joiakim son: child Jeshua son: child Jozadak and in/on/with day Nehemiah [the] governor and Ezra [the] priest [the] secretary
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
and in/on/with dedication wall Jerusalem to seek [obj] [the] Levi from all place their to/for to come (in): bring them to/for Jerusalem to/for to make: do dedication and joy and in/on/with thanksgiving and in/on/with song cymbal harp and in/on/with lyre
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
and to gather son: descendant/people [the] to sing and from [the] talent around Jerusalem and from village Netophathite
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
and from Beth-gilgal [the] Beth-gilgal and from land: country Geba and Azmaveth for village to build to/for them [the] to sing around Jerusalem
30 Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
and be pure [the] priest and [the] Levi and be pure [obj] [the] people and [obj] [the] gate and [obj] [the] wall
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
and to ascend: establish [obj] ruler Judah from upon to/for wall and to stand: appoint [emph?] two thanksgiving great: large and procession to/for right: south from upon to/for wall to/for gate [the] Dung (Gate)
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
and to go: follow after them Hoshaiah and half ruler Judah
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
and Azariah Ezra and Meshullam
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
Judah and Benjamin and Shemaiah and Jeremiah
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
and from son: descendant/people [the] priest in/on/with trumpet Zechariah son: child Jonathan son: child Shemaiah son: child Mattaniah son: child Micaiah son: child Zaccur son: child Asaph
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
and brother: male-relative his Shemaiah and Azarel Milalai Gilalai Maai Nethanel and Judah Hanani in/on/with article/utensil song David man [the] God and Ezra [the] secretary to/for face: before their
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
and upon gate [the] Fountain (Gate) and before them to ascend: rise upon step city David in/on/with ascent to/for wall from upon to/for house: home David and till gate [the] Water (Gate) east
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
and [the] thanksgiving [the] second [the] to go: walk to/for opposite and I after her and half [the] people from upon to/for [the] (Broad) Wall from upon to/for tower [the] (Tower of) the Ovens and till [the] (Broad) Wall [the] Broad
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
and from upon to/for gate Ephraim (Gate) and upon gate [the] (Gate of) Yeshanah and upon gate [the] Fish (Gate) and (Hananel) Tower (Tower of) Hananel and (Hananel) Tower [the] (Tower of) the Hundred and till gate [the] Sheep (Gate) and to stand: stand in/on/with gate [the] (Gate of the) Guard
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
and to stand: stand two [the] thanksgiving in/on/with house: temple [the] God and I and half [the] ruler with me
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
and [the] priest Eliakim Maaseiah Miniamin Micaiah Elioenai Zechariah Hananiah in/on/with trumpet
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
and Maaseiah and Shemaiah and Eleazar and Uzzi and Jehohanan and Malchijah and Elam and Ezer and to hear: proclaim [the] to sing and Jezrahiah [the] overseer
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
and to sacrifice in/on/with day [the] he/she/it sacrifice great: large and to rejoice for [the] God to rejoice them joy great: large and also [the] woman and [the] youth to rejoice and to hear: hear joy Jerusalem from distant
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
and to reckon: overseer in/on/with day [the] he/she/it human upon [the] chamber to/for treasure to/for contribution to/for first: beginning and to/for tithe to/for to gather in/on/with them to/for land: country [the] city portion [the] instruction to/for priest and to/for Levi for joy Judah upon [the] priest and upon [the] Levi [the] to stand: appoint
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
and to keep: obey charge God their and charge [the] purifying and [the] to sing and [the] gatekeeper like/as commandment David Solomon son: child his
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
for in/on/with day David and Asaph from front: old (head: leader *Q(K)*) [the] to sing and song praise and to give thanks to/for God
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.
and all Israel in/on/with day Zerubbabel and in/on/with day Nehemiah to give: give portion [the] to sing and [the] gatekeeper word: because day: daily in/on/with day: daily his and to consecrate: dedicate to/for Levi and [the] Levi to consecrate: dedicate to/for son: descendant/people Aaron