< Nehemia 12 >
1 Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
Ovo su svećenici i leviti koji su došli sa Zerubabelom, sinom Šealtielovim, i Ješuom: Seraja, Jeremija, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amarja, Maluk, Hatuš,
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
Šekanija, Rehum, Meremot,
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
Mijamin, Maadja, Bilga,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Šemaja, Jojarib, Jedaja,
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
Salu, Amok, Hilkija i Jedaja. To su bili glavari svećenički i njihova braća za Ješuina vremena.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
A leviti: Ješua, Binuj, Kadmiel, Šerebja, Juda i Matanija - ovaj potonji i njegova braća ravnali su hvalospjevima.
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
Bakbukja i Uni i braća njihova izmjenjivali su se s njima u službi.
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
Ješua rodi Jojakima; Jojakim rodi Elijašiba, a Elijašib Jojadu;
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
Jojada rodi Jonatana, a Jonatan rodi Jaduu.
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
U Jojakimovo vrijeme glavari svećeničkih obitelji bijahu: Serajine obitelji Meraja; Jeremijine Hananja;
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
Ezrine Mešulam; Amarjine Johanan;
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
Malukove Jonatan; Šebanijine Josip;
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
Harimove Adna; Meremotove Helkaj;
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
Idove Zaharija; Ginetonove Mešulam;
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
Abijine Zikri; Minjaminove ...; obitelji Moadjine Piltaj;
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
Bilgine Šamua; Šemajine Jonatan;
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
Jojaribove Matenaj; Jedajine Uzi;
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
Saluove Kelaj; Amokove Eber;
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
Hilkijine Hašabja; Jedajine Netanel.
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
U vrijeme Elijašiba, Jojade, Johanana i Jadue bili su popisani glavari levitskih obitelji i svećenici sve do kraljevanja Darija Perzijanca.
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
Sinovi Levijevi: glavari obitelji bili su zabilježeni u Knjizi ljetopisa, do vremena Johanana, sina Elijašibova.
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
Glavari levitski bili su: Hašabja, Šerebja, Ješua, Binuj, Kadmiel, a njihova braća, koja su stajala prema njima da pjevaju naizmjenično pohvale i zahvalnice prema uredbama Davida, Božjeg čovjeka,
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
bijahu: Matanija, Bakbukja i Obadja. A Mešulam, Talmon i Akub, vratari, čuvali su stražu kod skladišta blizu vrata.
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
Ti su živjeli u vrijeme Jojakima, sina Ješue, sina Josadakova, i u vrijeme upravitelja Nehemije i književnika svećenika Ezre.
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
Kad je bila posveta jeruzalemskoga zida, potražili su levite svugdje gdje su stanovali da ih dovedu u Jeruzalem te proslave posvetu radošću, zahvalnicama i pjesmom uz cimbale, harfe i citre.
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
I skupiše se pjevači, sinovi Levijevi, iz kraja oko Jeruzalema, iz netofatskih sela,
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
iz Bet Hagilgala, iz Gebe i polja Azmaveta: jer su pjevači sebi sagradili sela oko Jeruzalema.
30 Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
Svećenici i leviti očistili su sebe, a zatim su očistili narod, vrata i zid.
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
Tada sam izveo judejske knezove na zid i sastavio dva velika zbora. Prvi je išao desno niza zid, prema Smetlišnim vratima;
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
za njima su išli Hošaja i polovina judejskih knezova -
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
Azarja, Ezra i Mešulam,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
Juda, Benjamin, Šemaja i Jeremija,
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
a od svećeničkih sinova s trubljama: Zaharija, sin Jonatana, sina Šemaje, sina Matanije, sina Mikaje, sina Zakura, sina Asafa,
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
s braćom njihovom Šemajom, Azarelom, Milalajem, Gilalajem, Maajem, Netanelom, Judom, Hananijem, s glazbalima Davida, Božjega čovjeka. A Ezra, književnik, išao je pred njima.
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
Kod Izvorskih vrata popeli su se njima nasuprot kraj stepenica Davidova grada, zidnim usponom od Davidove palače sve do Vodenih vrata na istoku.
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
Drugi zbor, a za njim ja i polovica narodnih knezova, išao je nalijevo zidom i Pećkom kulom sve do Tržnog zida,
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
pa onda iznad Efrajimovih vrata, Starih vrata, Ribljih vrata, Hananelove kule, kule Meaha, sve do Ovčjih vrata. Zaustavili su se kod Zatvorskih vrata.
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
Potom su oba zbora zauzela mjesto u Domu Božjem. Tako i ja i sa mnom polovica odličnika,
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
svećenici Elijakim, Maaseja, Minjamin, Mikaja, Elijoenaj, Zaharija, Hananija s trubama,
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
zatim Maaseja, Šemaja, Eleazar, Uzi, Johanan, Malkija, Elam i Ezer. Pjevači su pjevali pod ravnanjem Jizrahjinim.
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
Toga su dana prinesene velike žrtve, ljudi su dali oduška radosti, jer ih je Bog ispunio velikom radošću, veselile se i žene i djeca. I radost Jeruzalema čula se nadaleko.
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
U to su vrijeme postavljeni ljudi da nadziru spremišta prinosa, prvina, desetina i da s polja uz gradove sabiru dijelove koje Zakon dodjeljuje svećenicima i levitima. Jer su se Judejci radovali svećenicima i levitima koji su bili u službi.
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
Oni su vršili službu Bogu svome i službu očišćenja - kao i pjevači i vratari - prema odredbi Davida i njegova sina Salomona.
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
Jer od Davidovih i Asafovih dana, od davnine, postoje pjevački glavari i pjesme pohvalne i zahvalnice Bogu.
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.
Zato je sav Izrael u vrijeme Zerubabela i u Nehemijino vrijeme dan za danom davao dijelove određene za pjevače i vratare. Davali su levitima posvećene darove, a leviti su davali sinovima Aronovim.