< Nehemia 11 >
1 Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
Now the leaders of the people lived in Jerusalem. Yet truly, the remainder of the people cast lots, so that they might choose one part in ten who were to live in Jerusalem, the holy city, and nine parts for the other cities.
2 Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
Then the people blessed all the men who freely offered themselves to live in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
And so these are the leaders of the province, who were living in Jerusalem, and in the cities of Judah. Now each one lived in his possession, in their cities: Israel, the priests, the Levites, the temple servants, and the sons of the servants of Solomon.
4 ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
And in Jerusalem, there lived some of the sons of Judah, and some of the sons of Benjamin: of the sons of Judah, Athaiah, the son of Aziam, the son of Zechariah, the son of Amariah, the son of Shephatiah, the son of Mahalalel, of the sons of Perez;
5 Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
Maaseiah, the son of Baruch, the son of Colhozeh, the son of Hazaiah, the son of Adaiah, the son of Joiarib, the son of Zechariah, the son of a Silonite.
6 Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
All these sons of Perez lived in Jerusalem, four hundred sixty-eight strong men.
7 Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
Now these are the sons of Benjamin: Sallu, the son of Meshullam, the son of Joed, the son of Pedaiah, the son of Kolaiah, the son of Maaseiah, the son of Ithiel, the son of Jeshaiah;
8 na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
and after him Gabbai, Sallai. These were nine hundred twenty-eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
And Joel, the son of Zichri, was their foremost leader. And Judah, the son of Hassenuah, was second over the city.
10 Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
And from the priests, there were Jedaiah, the son of Joiarib, Jachin,
11 Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
Seraiah, the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, the ruler of the house of God,
12 pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
and their brothers, who were doing the works of the temple: eight hundred twenty-two. And Adaiah, the son of Jeroham, the son of Pelaliah, the son of Amzi, the son of Zachariah, the son of Pashhur, the son of Malchijah,
13 na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
and his brothers, the leaders among the fathers: two hundred forty-two. And Amassai, the son of Azarel, the son of Ahzai, the son of Meshillemoth, the son of Immer,
14 na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
and their brothers, who were very powerful: one hundred twenty-eight. And their foremost leader was Zabdiel, the son of the powerful.
15 Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
And from the Levites, there were Shemaiah, the son of Hasshub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, the son of Bunni,
16 Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
and Shabbethai and Jozabad, who were over all the works which were exterior to the house of God, from among the leaders of the Levites.
17 Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
And Mattaniah, the son of Mica, the son of Zabdi, the son of Asaph, was the leader of praise and confession in prayer, with Bakbukiah, second among his brothers, and Abda, the son of Shammua, the son of Galal, the son of Jeduthun.
18 Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
All the Levites in the holy city were two hundred eighty-four.
19 Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
And the gatekeepers, Akkub, Talmon, and their brothers, who guarded the doorways, were one hundred seventy-two.
20 Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
And the remainder of Israel, the priests and the Levites, were in all the cities of Judah, each one in his own possession.
21 Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
And the temple servants were living at Ophel, with Ziha and Gishpa, of the temple servants.
22 Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
And the director of the Levites in Jerusalem was Uzzi, the son of Bani, the son of Hashabiah, the son of Mattaniah, the son of Mica. The singing men in the ministry of the house of God were from the sons of Asaph.
23 Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
In fact, there was a precept of the king about them, and an order among the singing men, throughout each day.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
And Pethahiah, the son of Meshezabel, from the sons of Zerah, the son of Judah, was at the hand of the king concerning every word of the people,
25 Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
and in the houses throughout all their regions. Some of the sons of Judah lived at Kiriatharba and in its daughter villages, and at Dibon and in its daughter villages, and at Jekabzeel and in its vicinity,
26 katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
and at Jeshua, and at Moladah, and at Bethpelet,
27 katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
and at Hazarshual, and at Beersheba and in its daughter villages,
28 katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
and at Ziklag, and at Meconah and in its daughter villages,
29 katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
and at Enrimmon, and at Zorah, and at Jarmuth,
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and in their villages, at Lachish and its regions, and at Azekah and in its daughter villages. And they dwelt from Beersheba as far as the valley of Hinnom.
31 Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
But the sons of Benjamin lived from Geba, at Michmash, and Aija, and Bethel and in its daughter villages,
32 katika Anathothi, Nobu na Anania,
to Anathoth, Nob, Ananiah,
33 katika Hazori, Rama na Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim,
34 katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
Hadid, Zeboim, and Neballat, Lod,
35 katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
and Ono, the valley of craftsmen.
36 Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.
And some of the Levites were apportioned with Judah and Benjamin.