< Nehemia 1 >

1 Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia: Katika mwezi wa Kisleu katika mwaka wa ishirini, wakati nilikuwa ngomeni katika jumba la kifalme la Shushani,
Paroles de Néhémias, fils de Helchias. Et il arriva au mois de Casleu, en l’année vingtième, que j’étais dans le château de Suse.
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, alikuja kutoka Yuda akiwa na watu wengine, nami nikawauliza kuhusu mabaki ya Wayahudi wale walionusurika kwenda uhamishoni na pia kuhusu Yerusalemu.
Et Hanani, un de mes frères, vint, lui et des hommes de Juda; et je les interrogeai sur ceux des Juifs, qui étaient restés de la captivité, et qui vivaient encore, et sur Jérusalem.
3 Wakaniambia, “Wale walionusurika kwenda uhamishoni, wale ambao wamerudi kwenye lile jimbo, wako katika taabu kubwa na aibu. Ukuta wa Yerusalemu umebomoka, na malango yake yamechomwa moto.”
Et ils me répondirent: Ceux qui sont restés et qui ont été laissés de la captivité là dans la province, sont dans une grande affliction et dans l’opprobre; et le mur de Jérusalem est tombé, et ses portes ont été brûlées au feu.
4 Niliposikia mambo haya, niliketi, nikalia. Kwa siku kadhaa niliomboleza na kufunga na kuomba mbele za Mungu wa mbinguni.
Lorsque j’eus ouï de telles paroles, je m’assis, je pleurai, et je gémis durant plusieurs jours; je jeûnais, et je priais devant la face du Dieu du ciel.
5 Kisha nikasema: “Ee Bwana, Mungu wa mbinguni, mkuu na mwenye kuogofya, ambaye hulishika agano lake la upendo na wale wampendao na kutii amri zake,
Et je dis: Je vous prie. Seigneur, Dieu du ciel, fort, grand et terrible, qui gardez l’alliance et la miséricorde avec ceux qui vous aiment et qui gardent vos commandements,
6 tega masikio yako, na ufungue macho yako, ili usikie maombi ya mtumishi wako anayoomba mbele yako usiku na mchana kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli. Ninaungama dhambi zetu sisi Waisraeli, pamoja na zangu na za nyumba ya baba yangu, tulizotenda dhidi yako.
Que vos oreilles deviennent attentives et vos yeux, ouverts pour en cendre la prière de votre serviteur, que je fais aujourd’hui devant vous, nuit et jour, pour les enfants d’Israël, vos serviteurs; et je confesse les péchés des enfants d’Israël, par lesquels ils ont péché contre vous: moi et la maison de mon père, nous avons péché.
7 Tumetenda uovu sana mbele zako. Hatukutii amri, maagizo na sheria ulizompa Mose mtumishi wako.
Nous avons été séduits par la vanité, et nous n’avons pas gardé votre commandement, vos cérémonies, et les ordonnances que vous avez prescrites à Moïse, votre serviteur.
8 “Kumbuka agizo ulilompa Mose mtumishi wako, ukisema, ‘Kama mkikosa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa,
Souvenez-vous de la parole que vous avez confiée à Moïse, votre serviteur, disant: Lorsque vous aurez transgressé, moi je vous disperserai parmi les peuples:
9 lakini mkinirudia na kutii amri zangu, ndipo hata kama watu wenu walio uhamishoni wako mbali sana katika miisho ya dunia, nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina langu.’
Et si vous revenez à moi, et que vous gardiez mes préceptes, et que vous les accomplissiez, quand même vous auriez été emmenés jusqu’aux extrémités du ciel, je vous rassemblerai de là, et je vous ramènerai au lieu que j’ai choisi pour que mon nom y habite.
10 “Hawa ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa nguvu zako kuu na mkono wako wenye nguvu.
Et ceux-ci sont vos serviteurs et votre peuple, que vous avez rachetés par votre grande force et par votre main puissante.
11 Ee Bwana, tega sikio lako na usikie maombi ya huyu mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako wanaofurahia kuliheshimu Jina lako. Nipe leo, mimi mtumishi wako, mafanikio kwa kunipa kibali mbele ya mtu huyu.” Kwa maana nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.
Je vous conjure, Seigneur, que votre oreille soit attentive à la prière de votre serviteur, et à la prière de vos serviteurs, qui veulent craindre votre nom; et dirigez votre serviteur aujourd’hui, et donnez-lui miséricorde devant cet homme: car moi j’étais l’échanson du roi.

< Nehemia 1 >