< Nahumu 1 >

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
Une révélation sur Ninive. Le livre de la vision de Nahoum l'Elkoshite.
2 Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
Yahvé est un Dieu jaloux et vengeur. Yahvé se venge et il est plein de colère. Yahvé se venge de ses adversaires, et il entretient sa colère contre ses ennemis.
3 Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
Yahvé est lent à la colère et grand en puissance, et il ne laisse pas le coupable impuni. Yahvé agit dans le tourbillon et dans la tempête, et les nuages sont la poussière de ses pieds.
4 Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
Il repousse la mer et la met à sec, il assèche tous les fleuves. Le Basan et le Carmel dépérissent. La fleur du Liban dépérit.
5 Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
Devant lui, les montagnes tremblent, et les collines se fondent. La terre tremble en sa présence, Le monde et tous ceux qui l'habitent.
6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
Qui peut résister à sa colère? Qui peut supporter l'ardeur de sa colère? Sa colère se répand comme un feu, et les rochers se brisent sous ses coups.
7 Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
Yahvé est bon, il est une forteresse au jour de la détresse, et il connaît ceux qui se réfugient en lui.
8 lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
Mais, par une inondation débordante, il détruira sa demeure, et il poursuivra ses ennemis dans les ténèbres.
9 Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
Que complotez-vous contre Yahvé? Il l'anéantira. L'affliction ne se lèvera pas une seconde fois.
10 Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
Car, empêtrés comme des épines, ivres comme de leur boisson, ils sont consumés comme du chaume sec.
11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
Il en est sorti de vous un qui médite le mal contre Yahvé, qui conseille la méchanceté.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
Yahvé dit: « Même s'ils sont en pleine force et aussi nombreux, ils seront abattus et disparaîtront. Je t'ai humilié, mais je ne t'humilierai plus.
13 Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
Maintenant, je briserai son joug de dessus toi, et je romprai tes liens. »
14 Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
Yahvé a donné un ordre à ton sujet: « Aucun descendant ne portera plus ton nom. De la maison de vos dieux, j'exterminerai l'image gravée et l'image en fusion. Je ferai votre tombeau, car vous êtes vils. »
15 Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.
Voici, sur les montagnes, les pieds de celui qui apporte de bonnes nouvelles, qui publie la paix! Garde tes fêtes, Juda! Accomplis tes vœux, car le méchant ne passera plus par toi. Il est exterminé.

< Nahumu 1 >