< Nahumu 2 >

1 Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi. Linda ngome, chunga barabara, jitieni nguvu wenyewe, kusanya nguvu zako zote!
Nadciąga niszczyciel przeciwko tobie! Strzeż miejsc obronnych, obserwuj drogę, wzmocnij biodra i zbierz wszystkie [swe] siły.
2 Bwana atarudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli, ingawa waangamizi wamewaacha ukiwa na wameharibu mizabibu yao.
PAN bowiem odwrócił pychę Jakuba jak pychę Izraela, gdyż złupili ich grabieżcy i zniszczyli ich latorośle.
3 Ngao za askari wake ni nyekundu, mashujaa wamevaa nguo nyekundu. Chuma kwenye magari ya vita chametameta, katika siku aliyoyaweka tayari, mikuki ya mierezi inametameta.
Tarcza jego mocarzy czerwona, jego wojownicy ubrani w szkarłat, rydwany będą jak płonące pochodnie w dniu jego przygotowania, a jodły będą strasznie się trząść.
4 Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani, yakikimbia nyuma na mbele uwanjani. Yanaonekana kama mienge ya moto; yanakwenda kasi kama umeme.
Rydwany po ulicach będą szaleć i na rynku skrzypieć. Z wyglądu będą podobne do pochodni, jak błyskawice będą pędzić.
5 Anaita vikosi vilivyochaguliwa, lakini bado wanajikwaa njiani. Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wa mji, ile ngao ya kuwakinga imetayarishwa.
Wezwie swoich mocarzy; zatoczą się w swoim pochodzie, pospieszą się do murów, obrona będzie przygotowana.
6 Malango ya mto yamefunguliwa wazi, na jumba la kifalme limeanguka.
Bramy przy rzekach otworzą się i pałac się rozpłynie;
7 Imeagizwa kwamba mji uchukuliwe na upelekwe uhamishoni. Vijakazi wake wanaomboleza kama hua na kupigapiga vifua vyao.
A Chusab zostanie uprowadzona do niewoli, jej służące będą ją prowadzić, jęcząc jak gołębie i bijąc się w piersi.
8 Ninawi ni kama dimbwi, nayo maji yake yanakauka. Wanalia, “Simama! Simama!” Lakini hakuna anayegeuka nyuma.
A Niniwa od swego początku [była] jak sadzawka wód, ale uciekną. [I choć ktoś powie]: Stójcie, stójcie! – [nikt] jednak się nie obejrzy.
9 Chukueni nyara za fedha! Chukueni nyara za dhahabu! Wingi wake hauna mwisho, utajiri kutoka hazina zake zote!
Rabujcie srebro, rabujcie złoto, bo nie ma końca bogactwo i przepych wszystkich kosztowności.
10 Ameharibiwa, ametekwa nyara, ameachwa uchi! Mioyo inayeyuka, magoti yanalegea, miili inatetemeka, na kila uso umebadilika rangi.
Pusta, opróżniona i spustoszona! Serce topnieje, trzęsą się kolana, czuć ból w biodrach wszystkich [ludzi], a twarze wszystkich czernieją.
11 Liko wapi sasa pango la simba, mahali ambapo waliwalisha watoto wao, ambapo simba dume na simba jike walikwenda na ambapo wana simba walikwenda bila kuogopa chochote?
Gdzie jest jaskinia lwów i pastwisko lwiąt, dokąd chodziły lew, ten wielki lew, oraz lwięta, a nie było nikogo, kto by [je] straszył.
12 Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake, alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake, akijaza makao yake kwa alivyoua na mapango yake kwa mawindo.
Lew już dosyć rozszarpał [ofiar] dla swych lwiąt i zadusił [je] dla swoich lwic, napełniał łupem swoje jaskinie, a zdobyczą swoje legowiska.
13 Bwana Mwenye Nguvu Zote anatangaza, “Mimi ni kinyume na ninyi. Magari yenu ya vita nitayateketeza kwa moto, na upanga utakula wana simba wako. Sitawaachia mawindo juu ya nchi. Sauti za wajumbe wako hazitasikika tena.”
Oto jestem przeciwko tobie, mówi PAN zastępów, spalę na proch twoje rydwany i twoje lwięta pożre miecz. Wykorzenię z ziemi twój łup i nie będzie już słychać głosu twoich posłów.

< Nahumu 2 >