< Nahumu 1 >

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
Prédiction à Ninive, livre de la vision de Nahum, Elcéséen.
2 Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
Dieu est jaloux, le Seigneur Se venge, le Seigneur Se venge avec colère, le Seigneur tire vengeance de ceux qui Lui sont opposés; Il extermine Ses ennemis.
3 Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
Le Seigneur est longanime, Sa force est grande; mais le Seigneur ne laissera pas impuni celui qu'Il n'a pas encore puni; Sa voie est dans la destruction et les ébranlements; et les nuages sont la poussière de Ses pieds.
4 Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
C'est Lui qui menace la mer et qui la dessèche; c'est Lui qui change en désert tous les fleuves. Basan et le Carmel ont défailli, et les fleurs du Liban se sont fanées.
5 Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
Par Lui, les montagnes ont tressailli et les collines ont tremblé; devant Sa face toute la terre a reculé, et ceux qui l'habitent
6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
Qui soutiendra le regard de Sa fureur? Qui résistera aux transports de Son courroux? Sa colère ronge les fondations; les rochers se fendent devant Lui.
7 Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
Le Seigneur est doux pour ceux qui L'attendent au jour de la tribulation; Il connaît ceux qui Le révèrent.
8 lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
Il détruira votre voie par une inondation; les ténèbres poursuivent ceux qui se lèvent contre Lui et Le haïssent.
9 Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
Pourquoi vos pensées sont-elles contre le Seigneur? Lui seul mène toutes choses à leur fin; Il ne S'y prendra pas à deux fois pour vous briser.
10 Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
Et celui-là sera dévasté jusqu'aux fondations, il sera dévoré par la flamme comme l'if aux rameaux entrelacés, comme le chaume tout à fait desséché.
11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
De toi, ô Ninive, sortira contre le Seigneur une pensée méchante et ennemie.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
Or voici ce que dit le Seigneur, souverain Maître des grandes eaux. Ils seront séparés pareillement, et l'on n'entendra plus parler de toi.
13 Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
Et maintenant, Mon peuple, Je vais briser loin de toi sa verge, et rompre tes liens.
14 Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
Voici ce que sur toi, Ninive, a prescrit le Seigneur: Ta renommée ne sera plus semée au loin; Je détruirai dans le temple de ton dieu les images sculptées ou jetées en fonte; Je vais comme en courant préparer ton sépulcre.
15 Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.
Voici sur les montagnes les pieds de Celui qui apporte la bonne nouvelle et qui annonce la paix. Juda, célèbre tes fêtes, accomplis tes vœux, car tes ennemis ne passeront plus sur ta terre, encouragés par ta décrépitude. Tout est fini pour eux, ils ont été retranchés.

< Nahumu 1 >