< Mika 1 >

1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
Parole du Seigneur, qui fut adressée à Michée le Morasthite, dans les jours de Joathan, d’Achaz, et d’Ezéchias, rois de Juda, parole relative à ce qu’il a vu touchant Samarie et Jérusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Ecoutez, vous tous, peuples, et que la terre soit attentive, ainsi que sa plénitude; et que le Seigneur Dieu soit témoin contre vous, le Seigneur du fond de son temple saint.
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Parce que voici que le Seigneur sortira de son lieu; et il descendra et foulera aux pieds les hauteurs de la terre.
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
Et les montagnes seront consumées sous lui; et les vallées se fendront et disparaîtront comme la cire à la face de la flamme, comme les eaux qui coulent sur une pente.
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
Tout cela à cause du crime de Jacob et des péchés de la maison d’Israël. Quel est le crime de Jacob? N’est-ce pas Samarie? et quelles sont les hauteurs de Juda? n’est-ce pas Jérusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
Et je rendrai Samarie comme un monceau de pierres qu’on ramasse dans le champ, lorsqu’on plante une vigne; je ferai rouler ses pierres dans la vallée, et ses fondements, je les découvrirai.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
Et toutes ses images taillées au ciseau seront brisées, et tous les dons qu’elle a reçus seront brûlés par le feu, et toutes ses idoles, je les livrerai à la destruction, parce qu’elles ont été acquises avec les salaires d’une prostituée, et elles deviendront le salaire d’une prostituée.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
Sur cela je me lamenterai, et je hurlerai; j’irai dépouillé et nu; je ferai des hurlements comme ceux des dragons, et des cris lugubres comme ceux des autruches:
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Parce que sa plaie est désespérée, qu’elle s’est étendue jusqu’à Juda, elle a pénétré jusqu’à la porte de mon peuple, jusqu’à Jérusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Ne l’annoncez pas dans Geth, ne donnez pas un libre cours à vos larmes; dans la maison de poussière, couvrez-vous de poussière.
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Et passez confuse d’ignominie, belle habitation. Elle n’est pas sortie, celle qui habite sur la limite; la maison voisine, qui s’est soutenue, recevra de vous un sujet de lamentation.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
Parce qu’elle est devenue faible pour le bien, celle qui habite au milieu des amertumes; parce que le mal est descendu du Seigneur à la porte de Jérusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Le bruit du quadrige est un objet de stupeur pour l’habitant de Lachis; la source du péché de la fille de Sion, c’est qu’en toi se sont trouvés les crimes d’Israël.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
À cause de cela, elle enverra des messagers à l’héritage de Geth; mais c’est une maison de mensonge pour tromper les rois d’Israël.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
Je t’amènerai encore l’héritier, à toi qui habites à Marésa; jusqu’à Odollam, la gloire d’Israël viendra.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Coupe ta chevelure, tonds-toi au sujet des fils de tes délices; sois entièrement chauve comme l’aigle; parce qu’ils ont été emmenés captifs loin de toi.

< Mika 1 >