< Mika 1 >
1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
La parole de l'Éternel qui fut adressée à Michée, de Moréseth, dans les temps de Jotham, d'Achaz et d'Ézéchias, rois de Juda, laquelle lui fut révélée touchant Samarie et Jérusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Écoutez, vous tous les peuples! sois attentive, ô terre avec tout ce qui y est! et que le Seigneur, l'Éternel, soit témoin contre vous, qu'il soit témoin, le Seigneur, de son saint temple!
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Car voici, l'Éternel va sortir de son séjour et descendre et s'avancer sur les hauteurs de la terre;
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
et les montagnes se dissoudront sous ses pas, et les vallées se fondront, comme la cire en présence du feu, comme des eaux versées sur une pente:
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
tout cela, pour le crime de Jacob et le péché de la maison d'Israël! D'où vient le crime de Jacob? n'est-ce pas de Samarie? et d'où les hauts lieux de Juda? n'est-ce pas de Jérusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
Aussi ferai-je de Samarie un tas de pierres dans un champ, une plantation de vigne, et précipiterai-je ses pierres dans la vallée, et mettrai-je ses fondements à nu;
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
et toutes ses images seront brisées, et tout le salaire de ses prostitutions brûlé au feu; et je saccagerai toutes ses idoles; car avec le salaire de ses prostitutions elle les a rassemblées et elles redeviendront salaire de prostitution.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
C'est pourquoi je gémis et me lamente, je vais sans chaussure ni vêtement; je me lamente comme le chacal et suis lugubre comme l'autruche.
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Mortel, en effet, est le coup qui la frappe, car il atteint jusques à Juda, pénètre jusqu'aux portes de mon peuple, à Jérusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
A Gath n'en dites rien! et à Acco ne pleurez pas! à Beth-léaphra je me roule dans la poudre!
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Émigre, habitante de Saphir, nue et honteuse! L'habitante de Tsaanan n'ose sortir; le deuil de Bethetsel vous prive de son abri.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
Car l'habitante de Maroth est inquiète de son salut, car de par l'Éternel la calamité est parvenue aux portes de Jérusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Attelle ton char aux coursiers, habitante de Lachis! tu fus un principe de péché pour la fille de Sion, car en toi se sont trouvées les défections d'Israël.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
Tu devras pour cela renoncer à Moréseth-Gath; les maisons d'Achsib seront une déception pour les rois d'Israël.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
Je ramènerai contre toi le conquérant, habitante de Marésa, la gloire d'Israël fuira jusques à Adullam.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Rase ta tête, coupe ta chevelure à cause de tes enfants chéris! rends-toi aussi chauve que le vautour; car ils s'en vont loin de toi captifs.