< Mika 1 >

1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
La parole de l'Eternel qui fut [adressée] à Michée Morasite au temps de Jotham, Achaz, et Ezéchias, Rois de Juda, laquelle lui [fut adressée] dans une vision, contre Samarie et Jérusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Vous tous peuples, écoutez; et toi terre, sois attentive, et que tout ce qui est en elle [écoute]; et que le Seigneur l'Eternel soit témoin contre vous, le Seigneur, [dis-je, sortant] du palais de sa sainteté.
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Car voici, l'Eternel s'en va sortir de son lieu, il descendra, et marchera sur les lieux hauts de la terre;
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
Et les montagnes se fondront sous lui, et les vallées se fendront, elles seront comme de la cire devant le feu, et comme des eaux qui coulent en une descente.
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
Tout ceci arrivera à cause du crime de Jacob, et à cause des péchés de la maison d'Israël. [Or] quel est le crime de Jacob? N'est-ce pas Samarie? Et quels sont les hauts lieux de Juda? N'est-ce pas Jérusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
C'est pourquoi je réduirai Samarie [comme] en un monceau de pierres [ramassées] dans les champs [où l'on veut planter des vignes]; et je ferai rouler ses pierres dans la vallée, et je découvrirai ses fondements.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
Et toutes ses images taillées seront brisées, tous les salaires de sa prostitution seront brûlés au feu, et je mettrai tous ses faux dieux en désolation; parce qu'elle les a entassés par le moyen du salaire de sa prostitution, ils serviront de salaire à une prostituée.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
C'est pourquoi je me plaindrai, et je hurlerai; je m'en irai dépouillé et nu; je ferai une lamentation comme celle des dragons, et je mènerai un deuil comme celui des chats-huants.
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Car il n'y a pas une de ses plaies qui ne soit incurable, chacune d'elles est venue jusqu'en Juda, et [l'ennemi] est parvenu jusqu'à la porte de mon peuple, jusqu'à Jérusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Ne l'annoncez point dans Gath, ne pleurez nullement; vautre-toi sur la poussière dans la maison d'Haphra.
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Habitante de Saphir passe, ayant ta nudité toute découverte; l'habitante de Tsaanan n'est point sortie pour la complainte de la maison d'Esel; on apprendra de vous à se tenir dans la maison.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
Car l'habitante de Maroth aura été dans l'angoisse pour [son] bien; parce que le mal est descendu de par l'Eternel sur la porte de Jérusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Attelle le cheval au chariot, habitante de Lakis, [toi qui] es le commencement du péché de la fille de Sion; car en toi ont été trouvés les crimes d'Israël.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
C'est pourquoi donne des présents à cause de Moreseth de Gath; les maisons d'Aczib mentiront aux Rois d'Israël.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
Je te ferai aussi venir un héritier, habitante de Maresa; et la gloire d'Israël viendra jusqu'à Hadullam.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Arrache tes cheveux, et te fais tondre à cause de tes fils qui font tes délices; arrache tout le poil de ton corps comme un aigle [qui mue], car ils sont emmenés prisonniers [loin] de toi.

< Mika 1 >