< Mika 1 >

1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
HERRENS Ord, som, i de Dage da Jotam, Akaz og Ezekias var Konger i Juda, kom til Mika fra Moresjet, og som han skuede om Samaria og Jerusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Alle I Folkeslag, hør, lyt til, du Jord, med din Fylde, at den Herre HERREN kan staa som Vidne blandt eder, Herren fra sit hellige Tempel.
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Thi se, fra sit Sted gaar HERREN ud, stiger ned, skrider frem over Jordens Høje;
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
under ham smelter Bjerge, og Dale slaar dybe Revner, som Voks, der smelter i Ilden, som Vand, gydt ned ad en Skrænt —
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
alt dette for Jakobs Brøde, for Israels Huses Synder. Hvem voldte Jakobs Brøde? Mon ikke Samaria? Hvem voldte Judas Synd? Mon ikke Jerusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
Samaria gør jeg til Grushob, dets Mark til Vingaardsjord; jeg styrter dets Sten i Dalen, dets Grundvolde bringer jeg for Lyset.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
Dets Billeder sønderslaas alle, dets Skøgeløn brændes i Ild; jeg tilintetgør alle dets Afguder; thi af Skøgeløn er de samlet, til Skøgeløn bliver de atter.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
Derfor vil jeg klage og jamre, gaa nøgen med bare Fødder, istemme Klage som Sjakaler, jamrende Skrig som Strudse:
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Ulægeligt er HERRENS Slag, thi det naar til Juda, til mit Folks Port rækker det hen, til Jerusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Forkynd det ikke i Gat, græd ikke i Bokim! Vælt jer i Støvet i Bet-Leafra!
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Der stødes i Horn for eder, Sjafirs Borgere; ej gaar Za'anans Borgere ud af deres By. Bet-Ezels Lod bliver Klage, Hug og Ve;
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
og hvor kan Marots Indbyggere haabe paa Lykke? Thi Ulykke kom ned fra HERREN til Jerusalems Porte.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Spænd Hestene for Vognen, I, som bor i Lakisj! Syndens Begyndelse var du for Zions Datter; ja, Israels Overtrædelser fandtes i dig.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
Giv derfor Moresjet-Gat en Skilsmissegave! En svigtende Bæk er Akzibs Huse for Israels Konger.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
End sender jeg eder en Ransmand, Maresjas Borgere! Til Adullam skal Israels Herlighed komme.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Klip dig skaldet over dine elskede Børn, bredskaldet som en Grib; thi de bortføres fra dig.

< Mika 1 >