< Mika 7 >
1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Misery é meu! Na verdade, sou como quem recolhe as frutas de verão, como respigadores da vinha. Não há cacho de uvas para comer. Minha alma deseja comer o figo primitivo.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
O homem piedoso pereceu fora da terra, e não há ninguém de pé entre os homens. Todos eles ficam à espera de sangue; cada homem caça seu irmão com uma rede.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
Suas mãos estão sobre o que é mau para fazê-lo de forma diligente. O governante e o juiz pedem um suborno. O homem poderoso dita o desejo maligno de sua alma. Assim, eles conspiram juntos.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
O melhor deles é como um brier. A mais erguida é pior que uma sebe de espinhos. O dia de seus vigilantes, mesmo a sua visita, chegou; agora é o momento de sua confusão.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Não confie em um vizinho. Não deposite confiança em um amigo. Com a mulher deitada em seu abraço, tenha cuidado com as palavras de sua boca!
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
Para o filho desonra o pai, a filha se levanta contra sua mãe, a nora contra sua sogra; Os inimigos de um homem são os homens de sua própria casa.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
Mas, quanto a mim, vou olhar para Yahweh. Vou esperar pelo Deus da minha salvação. Meu Deus vai me ouvir.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Não se regozije contra mim, meu inimigo. Quando eu cair, eu irei me levantar. Quando eu sentar na escuridão, Yahweh será uma luz para mim.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
Eu suportarei a indignação de Yahweh, porque eu pequei contra ele, até que ele me peça e execute o julgamento por mim. Ele me trará para a luz. Eu verei sua retidão.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Então meu inimigo o verá, e vergonha a cobrirá quem me disse, “Onde está Yahweh seu Deus?” Meus olhos a verão. Agora ela será pisoteada como a lama das ruas.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
Um dia para construir suas paredes! Naquele dia, ele estenderá seus limites.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
Naquele dia eles virão até você da Assíria e das cidades do Egito, e do Egito até o rio, e de mar a mar, e de montanha a montanha.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
No entanto, a terra ficará desolada por causa daqueles que nela habitam, pelo fruto de seus atos.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Pastoreie seu pessoal com seu pessoal, o rebanho de sua herança, que habitam sozinhos em uma floresta. Deixe-os se alimentar no meio de terras férteis de pastagem, em Bashan e Gilead, como nos velhos tempos.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
“Como nos dias de sua saída da terra do Egito, Vou mostrar-lhes coisas maravilhosas”.
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
As nações verão e se envergonharão de todas as suas forças. Eles colocarão sua mão na boca. Seus ouvidos ficarão surdos.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
Eles vão lamber o pó como uma serpente. Como coisas rastejantes da terra, elas sairão tremendo de suas covas. Eles virão com medo para Yahweh nosso Deus, e terá medo por sua causa.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Quem é um Deus como você, que perdoa a iniqüidade, e passa por cima da desobediência do remanescente de sua herança? Ele não retém sua raiva para sempre, porque ele se deleita em amar a bondade.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
Ele terá novamente compaixão de nós. Ele pisará nossas iniquidades sob os pés. Você lançará todos os seus pecados nas profundezas do mar.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
Você vai dar a verdade a Jacob, e misericórdia para com Abraão, como você jurou a nossos pais desde os tempos antigos.