< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Malheur à moi! me voilà comme celui qui ramasse du chaume en la moisson, ou qui cueille un grappillon de la vendange, n'ayant pas à lui une seule grappe pour en manger les prémices; malheur à mon âme!
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
Car le juste a péri sur la terre; et parmi les hommes il n'en est pas qui marche droit. Tous sont en justice pour avoir versé le sang; et chacun d'eux accable son prochain sous l'oppression.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
Et leurs mains sont prêtes à faire le mal. le prince exige; le juge dit des paroles douces; et voici le désir de son âme: Je prendrai leurs biens,
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
comme le ver qui ronge, marchant décemment au jour de la visite. Malheur! Tes vengeances, Seigneur, sont venues, et maintenant vont venir leurs lamentations.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Ne vous fiez pas à vos amis, n'espérez pas en vos princes; garde-toi même de ton épouse, et ne lui confie quoi que ce soit.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
Car le fils outragera le père; la fille se révoltera contre sa mère, la bru contre sa belle-mère; l'homme aura pour ennemis tous ceux de sa maison.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
Pour moi, je regarderai le Seigneur; j'attendrai le Dieu mon Sauveur, et mon Dieu m'exaucera.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Ne m'insulte pas, ô mon ennemie, parce que je suis tombée, je me relèverai; car, si je suis à terre dans les ténèbres, le Seigneur m'éclairera.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
Parce que j'ai péché contre le Seigneur, je supporterai Sa colère jusqu'à ce qu'Il ait reconnu juste ma cause. Et alors Il me rendra justice, et Il me ramènera à la lumière, et je verrai Son équité.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Et mon ennemie verra cela; et elle sera couverte de honte, celle qui dit maintenant: Où est le Seigneur ton Dieu? Mes yeux la regarderont alors, et elle sera foulée aux pieds comme la boue des rues.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
Voici le jour où l'on enduit la brique; ce jour sera celui de ta destruction, et ce jour-là tes lois seront effacées,
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
et tes villes seront mises au niveau du sol; elles seront partagées entre les Assyriens; et tes forteresses seront partagées, depuis Tyr jusqu'au fleuve, d'une mer à l'autre, et d'une montagne à l'autre.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Et ta terre et tous ceux qui l'habitent seront désolés, à cause des fruits de leur convoitise.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Ta verge à la main, Seigneur, pais les brebis de Ton héritage, qui d'elles-mêmes se sont abritées dans la forêt du Carmel. Elles trouveront leur pâture en Basan et Galaad, comme aux jours d'autrefois,
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
comme aux jours où Tu nous as fait sortir d'Égypte. Vous verrez des prodiges;
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
et les gentils les verront aussi, et ils en seront confondus malgré toute leur puissance, ils se mettront la main sur la bouche, et leurs oreilles n'entendront plus.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
Ils lécheront la terre comme les serpents qui rampent dans la poussière; ils seront pleins de trouble dans l'enceinte de leurs remparts; ils seront hors d'eux-mêmes, à cause du Seigneur notre Dieu, et ils auront peu de Lui.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Qui donc est Dieu comme Toi, qui ôtes les péchés, et passes sous silence les impiétés de ce qui reste de Ton héritage! Le Seigneur n'a point maintenu le témoignage de Sa colère; Il Se complaît en Sa miséricorde;
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
Il reviendra; Il aura compassion de nous; Il submergera nos iniquités; Il jettera nos péchés au fond de la mer.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
Il fera des dons à Jacob, en vérité; Il sera miséricordieux envers Abraham, comme Il l'a juré à nos pères aux jours d'autrefois.

< Mika 7 >