< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
La misère est à moi! En effet, je suis comme celui qui cueille les fruits d'été, comme des glanes de la vigne. Il n'y a pas de grappe de raisin à manger. Mon âme désire manger la figue précoce.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
L'homme pieux a péri sur la terre, et il n'y a personne de droit parmi les hommes. Ils sont tous à l'affût du sang; chaque homme chasse son frère avec un filet.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
Leurs mains sont sur ce qui est mauvais pour le faire avec diligence. Le souverain et le juge demandent un pot-de-vin. L'homme puissant dicte le mauvais désir de son âme. Ainsi, ils conspirent ensemble.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
Le meilleur d'entre eux est comme un ronceau. Le plus droit est pire qu'une haie d'épines. Le jour de vos gardiens, même votre visite, est arrivée; c'est maintenant le temps de leur confusion.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Ne faites pas confiance à un voisin. Ne faites pas confiance à un ami. Avec la femme allongée dans vos bras, faites attention aux mots de votre bouche!
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
Car le fils déshonore le père, la fille se soulève contre sa mère, la belle-fille contre sa belle-mère; les ennemis d'un homme sont les hommes de sa propre maison.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
Mais moi, je me tournerai vers Yahvé. J'attendrai le Dieu de mon salut. Mon Dieu m'entendra.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Ne te réjouis pas contre moi, mon ennemi. Quand je tomberai, je me relèverai. Quand je serai assis dans les ténèbres, Yahvé sera pour moi une lumière.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
Je supporterai la colère de Yahvé, parce que j'ai péché contre lui, jusqu'à ce qu'il plaide ma cause et exécute le jugement pour moi. Il m'amènera à la lumière. Je verrai sa justice.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Alors mon ennemi le verra, et la honte couvrira celle qui m'a dit, « Où est Yahvé ton Dieu? » Mes yeux la verront. Maintenant, elle sera foulée aux pieds comme la boue des rues.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
Un jour pour construire vos murs! Ce jour-là, il repoussera vos limites.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
En ce jour-là, ils viendront à toi de l'Assyrie et des villes d'Égypte, et depuis l'Égypte jusqu'au fleuve, et d'une mer à l'autre, et de montagne en montagne.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Mais le pays sera dévasté à cause de ceux qui l'habitent, pour le fruit de leurs actions.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Fais paître ton peuple avec ton bâton, le troupeau de votre héritage, qui vivent seuls dans une forêt. Laissez-les se nourrir au milieu de pâturages fertiles, en Basan et en Galaad, comme au temps jadis.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
« Comme à l'époque de votre sortie du pays d'Égypte, Je leur montrerai des choses merveilleuses. »
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
Les nations verront et auront honte de toute leur puissance. Ils poseront leur main sur leur bouche. Leurs oreilles seront sourdes.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
Ils lécheront la poussière comme un serpent. Comme des êtres rampants de la terre, ils sortiront en tremblant de leur tanière. Ils viendront avec crainte vers Yahvé notre Dieu, et auront peur à cause de vous.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Qui est un Dieu comme toi, qui pardonne l'iniquité? et passe sous silence la désobéissance du reste de son héritage? Il ne garde pas sa colère pour toujours, parce qu'il se complaît dans la bonté.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
Il aura de nouveau pitié de nous. Il foulera nos iniquités aux pieds. Tu jetteras tous leurs péchés dans les profondeurs de la mer.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
Tu donneras la vérité à Jacob, et la miséricorde à Abraham, comme tu l'as juré à nos pères dès les premiers jours.

< Mika 7 >