< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
woe! to/for me for to be like/as gathering summer like/as gleaning vintage nothing cluster to/for to eat early fig to desire soul: appetite my
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
to perish pious from [the] land: country/planet and upright in/on/with man nothing all their to/for blood to ambush man: anyone [obj] brother: compatriot his to hunt net
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
upon [the] bad: evil palm to/for be good [the] ruler to ask and [the] to judge (in/on/with recompense *L(abh)*) and [the] great: large to speak: speak desire soul: appetite his he/she/it and to weave her
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
pleasant their like/as briar upright from hedge day to watch you punishment your to come (in): come now to be confusion their
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
not be faithful in/on/with neighbor not to trust in/on/with tame from to lie down: lay down bosom: embrace your to keep: guard entrance lip your
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
for son: child be senseless father daughter to arise: attack in/on/with mother her daughter-in-law in/on/with mother-in-law her enemy man human house: household his
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
and I in/on/with LORD to watch to wait: wait to/for God salvation my to hear: hear me God my
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
not to rejoice enemy my to/for me for to fall: fall to arise: rise for to dwell in/on/with darkness LORD light to/for me
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
rage LORD to lift: bear for to sin to/for him till which to contend strife my and to make: do justice: judgement my to come out: send me to/for light to see: see in/on/with righteousness his
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
and to see: see enemy my and to cover her shame [the] to say to(wards) me where? he LORD God your eye my to see: see in/on/with her now to be to/for trampling like/as mud outside
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
day to/for to build wall your day [the] he/she/it to remove statute: allotment
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
day he/she/it and till you to come (in): come to/for from Assyria and city Egypt and to/for from Egypt and till River and sea from sea and mountain: mount [the] mountain: mount
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
and to be [the] land: country/planet to/for devastation upon to dwell her from fruit deed their
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
to pasture people your in/on/with tribe: staff your flock inheritance your to dwell to/for isolation wood in/on/with midst plantation to pasture Bashan and Gilead like/as day forever: antiquity
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
like/as day to come out: come you from land: country/planet Egypt to see: see him to wonder
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
to see: see nation and be ashamed from all might their to set: put hand upon lip ear their be quiet
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
to lick dust like/as serpent like/as to crawl land: soil to tremble from perimeter their to(wards) LORD God our to dread and to fear: revere from you
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
who? God like you to lift: forgive iniquity: crime and to pass upon transgression to/for remnant inheritance his not to strengthen: strengthen to/for perpetuity face: anger his for delighting kindness he/she/it
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
to return: again to have compassion us to subdue iniquity: crime our and to throw in/on/with depth sea all sin their
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
to give: do truth: faithful to/for Jacob kindness to/for Abraham which to swear to/for father our from day front: old

< Mika 7 >