< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Woe! to me for I have become like gathering of summer fruit like gleanings of [the] grape harvest there not [is] a cluster of grapes to eat early fig[s] it craves appetite my.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
He has perished [the] faithful from the land and [is] an upright [person] among humankind there not all of them for blood they lie in wait each brother his they hunt a net.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
[are] on Evil both hands to do [it] well the official [is] asking and the judge (for bribe *L(abh)*) and the great [person] [is] speaking [the] craving of self his he and they weave it.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
Good person their [is] like a thorn-bush an upright [person] more than a thorn hedge [the] day of watchmen your punishment your it has come now it will be confusion their.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
May not you believe in a neighbor may not you trust in a close friend from [she who] lies of bosom your guard [the] openings of mouth your.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
For a son [is] treating with contempt a father a daughter [is] arising on mother her a daughter-in-law on mother-in-law her [are the] enemies of a person [the] people of own household his.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
And I for Yahweh I will watch I will wait for [the] God of salvation my he will hear me God my.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
May not you rejoice O enemy my to me for I have fallen I will arise for I sit in darkness Yahweh [will be] light of me.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
[the] indignation of Yahweh I will bear for I have sinned to him until that he will conduct case my and he will do justice my he will bring out me to the light I will look on righteousness his.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
And she will see enemy my and it will cover her shame [she] who says to me where [is]? he Yahweh God your eyes my they will look on her now she will become a trampling place like [the] mud of [the] streets.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
A day to build walls your a day that it will be far a boundary.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
A day that and to you someone will come from Assyria and [the] cities of Egypt and from Egypt and to [the] River and sea from sea and mountain the mountain.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
And it will become the earth a desolation on inhabitants its from [the] fruit of deeds their.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Shepherd people your with rod your [the] flock of inheritance your [who] dwell alone a forest in [the] midst of a garden-land let them graze Bashan and Gilead like [the] days of antiquity.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
Like [the] days coming out you from [the] land of Egypt I will show him wonders.
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
They will see nations so they may be ashamed from all strength their they will put a hand on a mouth ears their they will be deaf.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
They will lick up dust like snake like [things which] crawl of [the] earth they will quake from strongholds their to Yahweh God our they will be in dread and they may be afraid from you.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Who? [is] a God like you [who] forgives iniquity and [who] passes over transgression to [the] remnant of inheritance his not he keeps hold of for ever anger his for [is one] desirous of covenant loyalty he.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
He will return he will have compassion on us he will subdue iniquities our so you may cast in [the] depths of [the] sea all sins their.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
You will give faithfulness to Jacob covenant loyalty to Abraham which you swore to fathers our from days of antiquity.

< Mika 7 >