< Mika 7 >
1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Woe is me! for I am as the last of the summer fruits, as the grape gleanings of the vintage; there is no cluster to eat; nor first-ripe fig which my soul desireth.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
The godly man is perished out of the earth, and the upright among men is no more; they all lie in wait for blood; they hunt every man his brother with a net.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
Their hands are upon that which is evil to do it diligently; the prince asketh, and the judge is ready for a reward; and the great man, he uttereth the evil desire of his soul; thus they weave it together.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
The best of them is as a brier; the most upright is worse than a thorn hedge; the day of thy watchmen, even thy visitation, is come; now shall be their perplexity.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Trust ye not in a friend, put ye not confidence in a familiar friend; keep the doors of thy mouth from her that lieth in thy bosom.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
For the son dishonoureth the father, the daughter riseth up against her mother, the daughter-in-law against her mother-in-law; a man's enemies are the men of his own house.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
'But as for me, I will look unto the LORD; I will wait for the God of my salvation; my God will hear me.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Rejoice not against me, O mine enemy; though I am fallen, I shall arise; though I sit in darkness, the LORD is a light unto me.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
I will bear the indignation of the LORD, because I have sinned against Him; until He plead my cause, and execute judgment for me; He will bring me forth to the light, and I shall behold His righteousness.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Then mine enemy shall see it, and shame shall cover her; who said unto me: Where is the LORD thy God? Mine eyes shall gaze upon her; now shall she be trodden down as the mire of the streets.'
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
'The day for building thy walls, even that day, shall be far removed.'
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
There shall be a day when they shall come unto thee, from Assyria even to the cities of Egypt, and from Egypt even to the River, and from sea to sea, and from mountain to mountain.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
And the land shall be desolate for them that dwell therein, because of the fruit of their doings.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Tend Thy people with Thy staff, the flock of Thy heritage, that dwell solitarily, as a forest in the midst of the fruitful field; let them feed in Bashan and Gilead, as in the days of old.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
'As in the days of thy coming forth out of the land of Egypt will I show unto him marvellous things.'
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
The nations shall see and be put to shame for all their might; they shall lay their hand upon their mouth, their ears shall be deaf.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
They shall lick the dust like a serpent; like crawling things of the earth they shall come trembling out of their close places; they shall come with fear unto the LORD our God, and shall be afraid because of Thee.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Who is a God like unto Thee, that pardoneth the iniquity, and passeth by the transgression of the remnant of His heritage? He retaineth not His anger for ever, because He delighteth in mercy.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
He will again have compassion upon us; He will subdue our iniquities; and Thou wilt cast all their sins into the depths of the sea.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
Thou wilt show faithfulness to Jacob, mercy to Abraham, as Thou hast sworn unto our fathers from the days of old.