< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Alas for me! for I am become as one gathering straw in harvest, and as [one gathering] grape-gleanings in the vintage, when there is no cluster for me to eat the first-ripe fruit: alas my soul!
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
For the godly is perished from the earth; and there is none among men that orders [his way] aright: they all quarrel even to blood: they grievously afflict every one his neighbour:
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
they prepare their hands for mischief, the prince asks [a reward], and the judge speaks flattering words; it is the desire of their soul:
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
therefore I will take away their goods as a devouring moth, and as one who acts by a [rigid] rule in a day of visitation. Woe, woe, thy times of vengeance are come; now shall be their lamentations.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Trust not in friends, and confide not in guides: beware of thy wife, so as not to commit anything to her.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
For the son dishonours his father, the daughter will rise up against her mother, the daughter-in-law against her mother-in-law: those in his house [shall be] all a man's enemies.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
But I will look to the Lord; I will wait upon God my Saviour: my God will hearken to me.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Rejoice not against me, mine enemy; for I have fallen [yet] shall arise; for though I should sit in darkness, the Lord shall be a light to me.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
I will bear the indignation of the Lord, because I have sinned against him, until he make good my cause: he also shall maintain my right, and shall bring me out to the light, [and] I shall behold his righteousness.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
And she that is mine enemy shall see it, and shall clothe herself with shame, who says, Where [is] the Lord thy God? mine eyes shall look upon her: now shall she be for trampling as mire in the ways.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
[It is] the day of making of brick; that day shall be thine utter destruction, and that day shall utterly abolish thine ordinances.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
And thy cities shall be levelled, and parted among the Assyrians; and thy strong cities shall be parted from Tyre to the river, and from sea to sea, and from mountain to mountain.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
And the land shall be utterly desolate together with them that inhabit it, because of the fruit of their doings.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Tend thy people with thy rod, the sheep of thine inheritance, those that inhabit by themselves the thicket in the midst of Carmel: they shall feed in the land of Basan, and in the land of Galaad, as in the days of old.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
And according to the days of thy departure out of Egypt shall ye see marvellous [things].
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
The nations shall see and be ashamed; and at all their might they shall lay their hands upon their mouth, their ears shall be deafened.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
They shall lick the dust as serpents crawling on the earth, they shall be confounded in their holes; they shall be amazed at the Lord our God, and will be afraid of thee.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Who is a God like thee, cancelling iniquities, and passing over the sins of the remnant of his inheritance? and he has not kept his anger for a testimony, for he delights in mercy.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
He will return and have mercy upon us; he will sink our iniquities, and they shall be cast into the depth of the sea, [even] all our sins.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
He shall give blessings truly to Jacob, and mercy to Abraam, as thou swarest to our fathers, according to the former days.

< Mika 7 >