< Mika 7 >
1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
我有禍了! 因為我變成了一個夏季搜摘果實,採集殘餘葡萄的人,卻沒有一粒葡萄可吃,也沒有我心思所想望的早熟的無花果。
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
虔敬人從地上消逝了,人間竟沒有一個正直人;人人都潛伏著要流人血,各以羅網獵取自己的弟兄。
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
他們的手善於作惡,官員貪求賄賂,法官勒索酬金,權貴只隨自己的心願發言,他們顛倒了一切。
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
他們中最好的人也不過相似荊棘,最正直的人也不過相似有刺的籬笆。你的守望者所宣佈的懲罰之日已經到了;現在他們必要驚惶。
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
你們不要信賴鄰里;不要倚靠朋友,連對躺在你懷中的妻子,也也要堅守口舌,
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
因為兒子要侮辱自己的父親,女兒要反抗自己的母親,兒媳要違抗自己的婆母:人的仇敵就是自己的家人。
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
至於我,我要仰望上主,寄望於拯救我的天主;天主必要俯聽我。
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
我的仇敵! 你不要因我遭難而高興;我雖然跌倒,必再起來;我雖坐在黑暗中,但上主是我的光明。
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
因為我得罪了上主,我必須承擔上主的義怒,直到衪審判我的案件,為我主持公道,衪必領 進入光明,我必能目睹衪的正義。
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
我的仇敵見了,必要蒙受羞辱,因為他曾對我說:「上主你的天主在哪裏﹖」我的眼必要看見他,有如街上的污泥被人踐踏。
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
必有一天,要重建你的城垣;那一天,你的地界必要擴展;
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
那一天,從亞述到埃及,從提洛到幼發的河,從這海到那海,從這山到那山的人民,都要向你歸來;
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
其餘的地域,必因其中居民行為的惡果,變為一片荒涼。
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
上主,求你拿你的牧杖牧放你的人民──獨留在草莽中,在田園間,作你基業的羊群;讓他們在巴商和基肋阿得獲得豢養,一如昔日。
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
上主一如讓我們在你出離埃及的時日內,見到奇蹟;
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
讓異民見了,感到自己一籌莫展,棎自慚愧,用手掩口,雙耳變聾。
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
他們將舔土如蛇,像上爬行的爬蟲,戰戰兢兢地從他們洞穴裏爬出來,向你,上主我們的天主,表示尊敬敬畏。
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
哪裏有神相似你,赦免罪惡,寬宥他的基業──遺民的過錯,不堅時憤怒於永遠,反而喜愛仁慈﹖
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
你必再憐憫我們,將我們的邪惡踏於足下,將我們的一切罪過投入海底。
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
你必按照你昔日向我們祖先所發了的誓,對雅各伯表示忠信,對亞巴郎施行仁慈。