< Mika 7 >
1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Ya-oe kai aih he, khohal cangah bang maila, misurbit loh a yoep hnukah, a su aka om pawt bangla ka om. Thaihloe caak hamla ka hinglu loh a ngaidam.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
Khohmuen lamkah hlangcim he milh coeng tih hlang lakli ah aka thuem khaw tal coeng. A pum la thii te a rhongngol thil uh tih hlang loh a manuca te yaehtaboeih la a mae uh.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
A kut rhoi tah boethae dongah lohna coeng. Mangpa loh lai sahnah ham a bih tih lai a tloek. A hinglu loh talnah thui hamla haam tih amah neh tingtong uh.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
Amih kah a then te hling banghui ni. Aka thuem khaw vonghling lakah nah. Khohnin he nang aka tawt tih nang aka ngoldoelh hamla pai coeng. Amih kah tingtongnah khaw om coeng.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Na hui te tangnah uh boel lamtah khoboei dongah khaw pangtung uh boeh. Na rhang dongkah aka yalh taengah khaw na ka thohka te tuem.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
Capa loh a napa a hoo tih a canu loh a manu taengah, a langa loh a mani taengah tlai. Hlang loh a imkhui kah hlang rhoek te a thunkha nah.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
Tedae kai tah BOEIPA te ka dawn tih kamah kah khangnah Pathen te ka lamtawn dongah ka ol he ka Pathen loh a hnatun ni.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Ka thunkha loh kai soah na kohoe boeh. Ka cungku cakhaw ka thoo pueng ni. Hmaisuep ah ka ngol cakhaw BOEIPA tah kai ham vangnah la om.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
Amah taengah ka tholh coeng dongah BOEIPA kah thintoek he ka phueih mai bitni. Ka tuituknah a oelh tih ka tiktamnah a saii. Kai he vangnah khuila kai n'khuen vetih a duengnah te ka hmuh pueng ni.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Kai taengah, “Na Pathen BOEIPA te melae?,” aka ti ka thunkha rhoek loh a hmuh vaengah yah loh anih a thing bitni. Anih te ka mik loh a hmuh vaengah tol kah tangnong bangla cawtkoi ham om pawn ni.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
Na vongtung thoh hamla khohnin pai vetih te khohnin ah tah khotlueh a suem ni.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
Te khohnin vaengah tah Assyria neh Egypt khopuei lamkah khaw, Egypt neh tuiva, tuitunli lamkah khaw, tuitunli neh tlang, tlang lamkah khaw nang taengla ham pha ni.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Amih khoboe thaihtae lamloh amah khosa rhoek kongah diklai khaw khopong la poeh ni.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Na pilnam te na caitueng neh luem puei laeh. Na rho boiva he duup bueng ah ni kho a sak. Khosuen tue kah bangla Bashan neh Gilead kah cangphil cangngol lakli ah khaw luem uh saeh.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
Egypt kho lamkah na sunglat tue vaengkah bangla khobaerhambae te kan tueng ni.
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
Namtom loh a hmuh uh vetih amamih kah thayung thamal boeih te a yah uh puei ni. A kut te a ka dongah a puei uh vetih a hna paang uh ni.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
Rhul bangla laipi a laeh uh ni. Diklai kah aka kawl uh bangla a puep lamloh tlai uh ni. Mamih kah Pathen BOEIPA taengah birhih uh vetih nang te n'rhih uh ni.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Pathen namah bangla thaesainah aka phuei tih a rho a meet ham boekoeknah aka hmil he unim aka om? A thintoek te a yoeyah la pom pawt vetih a sitlohnah ni a. omtoem eh.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
Mael vetih mamih n'haidam ni. Mamih kathaesainah khaw a khoh ni. Amih kah tholhnah cungkuem te tuitunli kah laedil la na voeih bitni.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
Hlamat kum lamloh a pa rhoek taengah na toemngam bangla oltak he Jakob taengah, sitlohnah he Abraham taengah na paek ni.